mi mwenyewe sihitaji, karibuni wadau
View attachment 134831 $120 View attachment 134832 $220 View attachment 134833 $380 - 400
Unapokusudia kufungua biashara yako jambo la msingi angalia vifaa ambavyo havitakuletea maumivu ya kichwa soon, bora fanya kitu ambacho kikusahaulisha ununuzi wa dhana mara kwa mara hasi biashara yako inatulia.
Kwa barbashop jambo la msingi ni ununuzi wa zana hizo hapo juu, vitu vingine vinapatikana kwa bei rahisi na upatikanaji wake nirahisi.
Binafsi huwa nawafikishia watu bidhaa kama hizi wanaozihitaji, ninachofanya si kuwauzia, ila kwa ufafanuzi wote bei na manunusi, tax na usafirishaji kisha kuna ongezeko la komisheni yangu ya 5-10 % inategemea na gharama za bidhaa. Hakuna cha bei ya masikilizano hizo nibe toka kwa wauzaji.
mi mwenyewe sihitaji, karibuni wadau
Ningependa kujua ni biashara ipi inalipa zaidi kati ya biashara ya saloon ya kawaida ya kike au ya kiume katika maeneo ya miji midogo(Mikoani na wilayani) kwa kuzingatia Mtaji wa chini wa kuanzisha, Gharama za Uendeshaji, Wingi wa wateja, Changamoto, Pato na Faida.
Pia ningependa kufahamu ni wapi vifaa muhimu vyenye ubora vya saloon za kike na kiume kama Machine za kukaushia nywele(Dryer), Hair Steamer, Sterizer nk. zinapatikana na gharama zake zikoje.
Naamini topic hii itakuwa msaada kwa watu wengi sana.
Bila ya shaka wala hofu salon ya kike ndiyo inayolipa zaidi kuliko ya kiume iwapo utafanya yafuatayo -
Kwanza hakikisha unapata location mzuri kwa biashara yako kulingana na mtaji wako.
Pili hakikisha unapata profesional staffs wenye kuiheshimu kazi na wawe waaminifu.
Tatu hakikisha mnatoa huduma bora na siyo bora huduma umbeya na uswahili swahili ni mwiko.
Kuhusu faniture na vitu vidogo vidogo nenda RUDIUM(fire kariakoo) SH AMON(posta) na LEILA COSMETICS(kisutu,opposite Sewa Haji Hospital)
Angalizo: ili pesa yako irudi na uone faida salon ya kike inahitaji uangalizi na ufuatiliaji wa hali ya juu sana
vinginevyo hesabu maumivu makali sana.
Heshima kwenu.
Naomba kama kuna mtu ana uzoefu na saloon za kunyoa anipe uzoefu, tena zile za 1000 kichwa maana kwa hesabu zangu nikilipa chumba 40,000/50,000 na nikiongea na kinyozi anipe 10,000 kila siku na nikaiboresha si nitapata?
au mnanishauri vip?
Tembelea wadau wa sekta hiyo hapo mtaani kwako watakupa ushauri mzuri zaidi...