Biashara ya Nguo za Mtumba: Ushauri na Muongozo wa Kuifanya kwa Mafanikio

Watu wasikukatishe tamaa ndg, tena mimi si kwa rafiki wala jirani, nilianza mtumba, kwa kununua bero moja tu pale mnazi mmoja, faida ikatoka karibu sawa na bei ya baro nikarudia.

Nguo za kike zinalipa, mashuka na viatu, za kiume suruali na mashati ila wanaume wanakamatika kiurahs ukiwafikishia maeneo yao ya kazi au kwa kufuatwa.

Nimewai kwenda Uganda, najua vizur pia huko, anzia nyumbani uimarike kibiashara, japo mimi nimeajiriwa serikalini lakn nafanya sana mtumba. Na ivi sasa naanza likizo june, nitaendelea na mtumba kama kawa.

Mil 3 ni nyingi, suala la kununua bero na au za kuotea za kutundika/mnada ni wewe tu na upendo wako, za bero lazima ukute na marapurapu ndani, ingawa huwa tunauza cheap, na hazikosi wavaaji au wanunuzi, za kuotea utauza zote bila kuacha rapurapu lkn je? Unauzoefu wa kuotea nguo? Yani ukiiona tu unapoint? Maana mnakuwa wengi kayika ku point na wwngi ni wazoefu.

Hapo inahtaji mtu anaeona nguo tu nakujua hii ni sumu la sivo utaotea zote takataka au zinazokuvutia wewe binafs alafu zisivutie wateja.

Sehemu ya kupoint nguo ni ilala Boma, alifajir saa kumi na moja, baadae hakuna soko asbh meza ni za wanaouza kawaida kwa wapita njiA

Uliza swali kwa kile sikuandika nitakujibu.

Dresses za kike bero ya bei ya juu ni 380000/= kwa zile za kg 45, lakn unakuta bero ya top hadi 170000/= zinatofautiana kuanzia 150000/= mpk 400000/= hapo ndio juu sana kwa beri ya kilogram 45 na ukienda utaonesha hapa grade B hapa 1
Note: bero zinauzwa kwa kilogram, bei nilioweka ni. Kwa kg 45 ambazo mara nyingu utakuta nguo hadi 200

Bero za mil 1 ni kilograms 100 nk

Kuna maduka wana nguo uhakika. Naweza kukupa namba private nikakuunganisha.

Jaribu usikatishwe tamaa.
Kaka naomba hiyo namba
 
Duh haya mambo mpaka leo Bado ni vilevile Kama 2010?? Hasa Uganda?
 
Sawa ila nguo hizo ndizo zinanunuliwa sana maeneo hayo, lakini nitalifanyia kazi wazo lako.
Pole sana ila inategemea unauza nguo Grade gani? kwa mfano mimi nauzia Mkoani ila nikifungua belo moja nina uhakika wa kupata faida kwa mfano nikifungua belo la Geade II la viblauzi/sket labda nimenunua 450,000 nina uhakika wa kuuza nikapata 900,000 hadi 1,000,000 kwahiyo hapo faida ni nusu kwa nusu. nikitoa gharama za usafiri ambayo ni kama 25,000 mpaka linifikie. Na silipiii frem nafungulia nyumbani nawajulisha watu kwenye magroup ya whattsapp wanakuja siku nafungua home. Zinazobaki mtu akihitaji nampa boda anampelekea kwenye begi kama ni Ofisini anachagua then anarudisha zilizobaki na kwa mkoa nilipo Ofisi zipo karibu karibu hivyo nauli ya Boda haizidi 1000. Zikibaki za mwisho kabisa napeleka mnadani naziuza kwa bei ya chini. Au frem unalipia bei kubwa sana?
 
Ushauri wangu, lete hiyo mitumba tz 70% iwe ya kiume na 60% ya kike! na kwakua unaanza lete grade 1, ili ujenge good will na wateja! wahindi wanacho kifanya wanaleta grade tofauti kisha wanachanganya ili kupata super profit! Uzuri mmoja ni kuwa, ukileta mali nzuri. Mteja mmoja akifungua na kuona ni mzuri, huwaambia wenzake na wote huja kwako.

Kizuri kingine ni kuwa, kuna watu wana hela zao chini..Wao wanasubiri wasikie fulani kafungua mali nzuri na inakimbia, yeye anakufuata, kisha anakupa hela ya belo zote ulizonazo store kisha yeye anauza rejareja kama wewe ila anakuwa kaongeza elfu kumi au ishirini kwa belo! kwenye hii biashara, umakini mkubwa ni ubora wa hizo nguo na jinzi sio jinzi tu ziwe za kisasa, sio chupa (juu pana, chini inabana, hutouza)! nilishwahi kuingiza nguo frm tz zamani from usa via charlestone port via s.carolina, zilinikata kwa kweli.

Hakikisha kwenye huo mtumba, hakuna sox wala chupi. TBS watakupa shida bandarini.

Kama unaweza, mkuu badala ya nguo za mitumba weka mitumba ya viatu vya kiume, au changanya nguo za mtumba na viatu vya mtumba ili upime biashara! open shoes, canvas, mukasin, sendoz raba n.k! Kikweli biashara ya viatu vya mtumba inakimbia kupita maelezo.

Huna haja ya kuwa na duka au stoo kariakoo...wewe ukitangaza tu una viatu vya mtumba hasa vya kiume na kama utaweka kidogo vya kike visiwe kokoko, watu wananunua mali yote kwa siku moja! Ukiwa mvivu, utawauzia kontena lote, faida utaiona lakini ni kidogo sana ukilinganisha na watakachoenda kupata wao.

Kila siku asubuhi saa kumi uwe ushafika kariaokoo (mchikichini) na baloo tatu au nne hivi na kuhakikishia mpaka inafika kwenye saa moja asubuhi, unakuwa umemaliza mali yoote na unarudi home na furushi la kimango! Kule unakodisha meza kwa huo muda ni shilingi 5,000/- na vijana waaminifu wapo wa kukusaidia kulinda na kupiga debe, wewe kazi yako ni kupokea hela!

Kinachofanyika ni kuwa a day before upeleke hizo balo za viatu kariaokoo, unaita vijana wanatenganisha viatu vya kushoto na kulia, kwahiyo ukifika mchikichini asbuh unamwaga eiza vya kulia unabaki na vya kushoto and vice vser! Akikipenda kiatu unamtajia bei, bkoz kila kiatu kina bei yake, anakupa hela huku ameshika kimoja alicholipia! wakati wakufunga biashara, unampa mguu uliobakia.

Ofkoz, hadi mida hiyo lazima kuna pea kadhaa zinakuwa hazijapata wanunuzi, good news ni kuwa pembeni kuna watu kibao wanasubiri muhesabiane in a flat rate vyote vilivyobaki...ana ku'cash wewe unarudi na hela home saa moja asbh, na kuandaa mazingira ya kesho!

You can send mtu wako pale mchikichini, mida hiyo asbuhi akathibitishe nilio kwambia!
Nakushukuru sana kaka MUNGU akujalie zaidi
 
Naomba Connection ya kuagiza viatu vya mtumba vya watoto. viwe ni viatu vikali vya ngozi. China naona viatu vyao siyo vizuri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom