Natafuta marafiki wanaofanya biashara ya viatu vya mtumba

Bata Boy Official

JF-Expert Member
Sep 19, 2019
259
308
Habari wakuu?

Wanasema ndege wenye manyoya ya kufanana huruka pamoja. Na mimi pia naamini kwenye mzunguko wa watu wangu wa karibu nikiwa na watu wanaofanya kitu kama changu itanisaidia kukua.

Mimi nafanya biashara ya viatu vya mitumba lakini kwa sasa bado nipo hatua ya ku-pin-point(chambuu/kusagura) viatu karume. Bado sijafika hatua ya kununua Belo Zima.

Najua biashara ukiachilia mbali changamoto lakini pia zina siri nyingii sana na codes, ambazo kuzijua inahitaji kuwa karibu na wazoefu.

Namkaribisha mtu wa level na aina yoyote anayefanya biashara ya viatu vya mitumba. Ndoto na hamu yangu ni kukua na kuwa mfanya biashara mkubwa Mungu akitupa uhai.

PM yangu ipo wazi. Ukihitaji namba yangu pia ntakupatia.
 
Mimi pia niko nje ya Dar, huwa nauza mafua lakini nataka kubadilika niuze viatu vya ulaya ila sijui pa kuanzia. Viatu vya China / Korea vinatoa namba ndogo halafu vinabanduka sana kwenye jua. Viatu vya Ulaya vinatoa namba kubwa halafu vingi vimetumika sana. Mwenye kujua chimbo la viatu original ambavyo bell linatoa viatu vipya anicheck +255748763177
 
Back
Top Bottom