BENKI ya Dunia (WB) imeidhinisha Tanzania kupatiwa mkopo wa dola za Marekani 40 milioni sawa na zaidi ya Sh52 bilioni ili kufanikisha mradi wa ujenzi wa nyumba za kisasa kwa ajili ya Watanzania wenye kipato cha chini.
Benki hiyo, iliidhinisha fedha hizo mjini Washington, Marekani jana na kueleza kwamba zimetolewa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo (Ida).
Chombo hicho cha fedha duniani kilisambaza taarifa kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mradi huo utajenga nyumba za kisasa ili Watanzania wa kipato cha chini ambao mara nyingi wamekuwa wakishindwa kupata mikopo benki kwa sababu hawana mali isiyohamishika.
"Lengo la mradi huo ni kuwajengea uwezo wananchi, kuwawezesha kumiliki na kuishi kwenye nyumba bora," inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Msukumo mwingine wa kuidhinisha mabilioni hayo,
Taarifa hiyo, inaeleza kwamba benki ya dunia, iliidhinisha fedha hizo, kwa sababu wakazi wengi katika maeneo ya mijini, wanakabiliwa na matatizo ya makazi.
Inaeleza kwamba watu wengi wana matatizo ya makazi kutokana na kasi kubwa ya ongezeko la watu mjini na kusababisha ujenzi wa makazi holela bila kufuata utaratibu kwenye maeneo ambayo hayajapimwa.
"Kwa kuupa uwezo mradi wa ujenzi wa makazi, mkopo huu utawezesha wananchi uwezo wa kujiajiri wenyewe, kuongeza nafasi za ajira na hatimaye kuimarisha uchumi na kupunguza umasikini," alisema Mkurugenzi wa WB katika nchi za Uganda, Burundi na Tanzania, John Murray McIntire kwenye hafla ya kuidhinisha fedha hizo.
Source: Mwananchi.
Niliwahi kusema nyuma kuwa nilimsikia mshkaji akinambia jamaa (Nehemia Mchechu) aliteuliwa NHC aje kulisimamia hili dili naona mwezi unaandama pesa hizo zaja best wishes mzee. Tunasubiri kuona hizo nyumba za maskini zitakazojengwa.
Benki hiyo, iliidhinisha fedha hizo mjini Washington, Marekani jana na kueleza kwamba zimetolewa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo (Ida).
Chombo hicho cha fedha duniani kilisambaza taarifa kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mradi huo utajenga nyumba za kisasa ili Watanzania wa kipato cha chini ambao mara nyingi wamekuwa wakishindwa kupata mikopo benki kwa sababu hawana mali isiyohamishika.
"Lengo la mradi huo ni kuwajengea uwezo wananchi, kuwawezesha kumiliki na kuishi kwenye nyumba bora," inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Msukumo mwingine wa kuidhinisha mabilioni hayo,
Taarifa hiyo, inaeleza kwamba benki ya dunia, iliidhinisha fedha hizo, kwa sababu wakazi wengi katika maeneo ya mijini, wanakabiliwa na matatizo ya makazi.
Inaeleza kwamba watu wengi wana matatizo ya makazi kutokana na kasi kubwa ya ongezeko la watu mjini na kusababisha ujenzi wa makazi holela bila kufuata utaratibu kwenye maeneo ambayo hayajapimwa.
"Kwa kuupa uwezo mradi wa ujenzi wa makazi, mkopo huu utawezesha wananchi uwezo wa kujiajiri wenyewe, kuongeza nafasi za ajira na hatimaye kuimarisha uchumi na kupunguza umasikini," alisema Mkurugenzi wa WB katika nchi za Uganda, Burundi na Tanzania, John Murray McIntire kwenye hafla ya kuidhinisha fedha hizo.
Source: Mwananchi.
Niliwahi kusema nyuma kuwa nilimsikia mshkaji akinambia jamaa (Nehemia Mchechu) aliteuliwa NHC aje kulisimamia hili dili naona mwezi unaandama pesa hizo zaja best wishes mzee. Tunasubiri kuona hizo nyumba za maskini zitakazojengwa.