Kulupango
JF-Expert Member
- Mar 19, 2020
- 288
- 534
Karibu Benki zote hazina huduma ya vyoo kwa wateja hapa nchini, tunafahamu Benk ni kwajili ya kuweka hela na kutoa hela lakini ofisi nyingi vyoo ni vya watumishi tuu, sasa kama mabenki wateja ndiyo washirika wao kwanini vyoo vinakuwa ni tatizo kwao?
Je, wateja wao hawana mahitaji ya kwenda chooni, unakuta benki kuna foleni kubwa mtu anasimama karibu nusu saa, je haja ikimbana anakwenda wapi huyu mtu?
Mabenki yanatoa huduma za kifedha ikiwemo kukopesha wateja, tunafahamu kwamba kwa kila biashara yenye mkusanyiko ni lazima kuwe na hitaji la choo au huduma ya choo kwa wateja wao. Wanapaswa kuwekewa sheria wakati wa ujenzi wa ofisi zao kwasababu vyoo ni kwa ajili yao tu nasio wateja wao. Wakati ni sasa tunaomba Benki ziwe na vyoo. Haswa benki zenye foleni kubwa.
Mabenki mengi yamefanya huduma ya choo kwao hiyo ni huduma ya dharura! Ukihitaji wanakupeleka kwa usaidizi wa mlinzi ila tunashauri kuwepo choo cha umma mahsusi kwa wateja wao inabidi waboreshe miundombinu.
Benki nyingi hazina huduma hiyo yaani ukibanwa lazima utoke nje ukatafute huduma hiyo. Ofisi zao ni nzuri zimepambwa mfano wa nyumba lakini wanasahahu kabisa kuwa uzuri wa nyuma ni choo kwa wanaofika hapo.
Je, hakuna huduma ya choo kwasababu za kiusalama? Kwamba wezi wanaweza kupatumia kuandaa silaha za mashambulizi, basi vyema kuboresha mazingira vyoo viwe kando lakini vitambulike ni vyoo kwa ajili ya wateja wenu. Tunaomba Benki ziwe na huduma za choo kwa wateja wao wakati wateja wanapanga foleni kwa muda mrefu kusubiri huduma.
Kuna watu wengine hawezi kujizuia kuvumilia kukaa na haja ndogo au kubwa kwa muda mrefu na pia kukaa muda mrefu kuna wateja ambao ni wagonjwa. Shida huwa nifoleni basi ni vyema muongeze wahudumu na madirisha yote yafanye kazi, unakuta madirisha yapo sita lakini kazi inafanyika kwenye madirisha mawili, na huduma ya choo hakuna ilihali watu wanatumia muda mrefu.
Sehemu yoyote yenyewe mkusanyiko wa watu choo ni lazima, kubanwa haja hakuna muda lakini pia kuna dharura mtu kuugua! Ndio maana hata mabasi yanasimama njiani watu wanachimba dawa! Kama benki wanahofia usalama watafute namna kwani hiyo huduma haina mbadala!!
Wateja hulazimika kwenda kujikomba Komba kwa walinzi ili wasaidiwe japo kujisitiri kwa hajandogo nje ya benkI, na wakati mwingine nao maaskari kwa sababu za usalama huwa wanakataa kutoa ushirikiano kwa wateja na kwa mtu mwenye aibu anaweza kujikojolea, hivyo ni vema benkI zingekuwa na vyoo ndani vya wateja.
Ni kweli Benki nyingi hapa mjini zipo kwenye majengo yenye ofisi nyingi au zimepanga kwenye majengo yanayomilikiwa na watu au kampuni binafsi, Hali ya vyoo huwa ni kawaida. Benki zinatakiwa kuwa na vyoo rasmi kwa ajili ya wateja wao.
Kikawaida Benki zinatakiwa kutoa huduma kwa haraka siyo kuweka watu muda mrefu! Hivyo hitaji ya vyuo ni kidogo japo ni muhimu viwepo kwasababu benki zinachukua muda mrefu kutoa huduma. Ni vyema wawe na huduma hii kuzingatia na huduma wanazotoa ambapo watu hukusanyika na kusubiri huduma.
Unapotoa huduma kwa watu, na huduma ya choo ni lazima, kwa vile watu wanakaa muda mrefu wakisubiria huduma, hivyo, benki zilipaswa kutoa huduma. Huduma za Benki ni huduma za jamii, na kwenye jamii lazima kuwe na huduma za maliwato. Popote penye mkusanyiko wa watu huduma ya choo ni muhimu kibinaadamu, Ukipenda boga ppenda pamoja na ua lake.
Ninaomba taasisi hizo ziangalie huduma hii na huduma hii iwe pia ni rafiki kwa walemavu. Benki nyingi hapa Tanzania huduma ya Choo hawaitambui kama ni moja Kati ya huduma kwa wateja.
Tunaelewa jambo hili, linagharimu pesa kutoa vyoo vya umma, itagharimu pesa kuvitengeneza, kuvifunga na kisha kuvitunza. Lakini mnaweza kugeuza fursa hii ikawa kama mradi wa hapo ofisini, kama taasisi zingine zinavyofanya, kutoa huduma kwa njia ya kulipia unapoenda kwenye choo, na pesa hizo zinasaidia kuendesha huduma hiyo hapo ofisini.
Hapo mtakuwa mmefanya kwa wema wa mioyo yenu. Na kudumisha nia njema ya wateja wenu.
Tunaelewa kwamba benki zinaweza kukosa nafasi ya kuchukua vyumba na kuvigeuza kuwa vyoo kwa wateja wao. Zaidi ya hayo, huenda benki zisitake kuhimiza wasio wateja kukaa katika majengo yao kwa muda mrefu. Baadhi ya benki pia huenda zisitake kulipia gharama za ziada zinazohusiana na kutunza vyoo vya umma. Inawezekana pia kwamba baadhi ya benki zinaweza kuwa na vyoo vya umma hapo awali lakini zimeviondoa kwa sababu ya matatizo ya matengenezo au matumizi mabaya.
Lakini hoja ni kwamba kama matatizo yote hayo yanafahamika Benki inashindwa vipi kuja na ufumbuzi wa utatuzi kunako shida hiyo?
Hii si haki. Hatungependa kushuhudia matukio ya wateja kupata aibu na kudhalilika hadharani. Uwepo wa huduma ya choo sio suala dogo kwa kweli, ni suala kubwa la kiafya ambalo linapaswa kushughulikiwa.
Benki nyingi katika hili zinawatesa wateja wao. Ninaona kuwa haiwezekani kwa ‘’wateja wanaoheshimiwa’’ kama benki zinavyowaita, kulazimika kukimbia katikati ya shughuli ili kutafuta vyoo sehemu za nje vilivyo karibu na jumba la benki.
Je, wateja wao hawana mahitaji ya kwenda chooni, unakuta benki kuna foleni kubwa mtu anasimama karibu nusu saa, je haja ikimbana anakwenda wapi huyu mtu?
Mabenki yanatoa huduma za kifedha ikiwemo kukopesha wateja, tunafahamu kwamba kwa kila biashara yenye mkusanyiko ni lazima kuwe na hitaji la choo au huduma ya choo kwa wateja wao. Wanapaswa kuwekewa sheria wakati wa ujenzi wa ofisi zao kwasababu vyoo ni kwa ajili yao tu nasio wateja wao. Wakati ni sasa tunaomba Benki ziwe na vyoo. Haswa benki zenye foleni kubwa.
Mabenki mengi yamefanya huduma ya choo kwao hiyo ni huduma ya dharura! Ukihitaji wanakupeleka kwa usaidizi wa mlinzi ila tunashauri kuwepo choo cha umma mahsusi kwa wateja wao inabidi waboreshe miundombinu.
Benki nyingi hazina huduma hiyo yaani ukibanwa lazima utoke nje ukatafute huduma hiyo. Ofisi zao ni nzuri zimepambwa mfano wa nyumba lakini wanasahahu kabisa kuwa uzuri wa nyuma ni choo kwa wanaofika hapo.
Je, hakuna huduma ya choo kwasababu za kiusalama? Kwamba wezi wanaweza kupatumia kuandaa silaha za mashambulizi, basi vyema kuboresha mazingira vyoo viwe kando lakini vitambulike ni vyoo kwa ajili ya wateja wenu. Tunaomba Benki ziwe na huduma za choo kwa wateja wao wakati wateja wanapanga foleni kwa muda mrefu kusubiri huduma.
Kuna watu wengine hawezi kujizuia kuvumilia kukaa na haja ndogo au kubwa kwa muda mrefu na pia kukaa muda mrefu kuna wateja ambao ni wagonjwa. Shida huwa nifoleni basi ni vyema muongeze wahudumu na madirisha yote yafanye kazi, unakuta madirisha yapo sita lakini kazi inafanyika kwenye madirisha mawili, na huduma ya choo hakuna ilihali watu wanatumia muda mrefu.
Sehemu yoyote yenyewe mkusanyiko wa watu choo ni lazima, kubanwa haja hakuna muda lakini pia kuna dharura mtu kuugua! Ndio maana hata mabasi yanasimama njiani watu wanachimba dawa! Kama benki wanahofia usalama watafute namna kwani hiyo huduma haina mbadala!!
Wateja hulazimika kwenda kujikomba Komba kwa walinzi ili wasaidiwe japo kujisitiri kwa hajandogo nje ya benkI, na wakati mwingine nao maaskari kwa sababu za usalama huwa wanakataa kutoa ushirikiano kwa wateja na kwa mtu mwenye aibu anaweza kujikojolea, hivyo ni vema benkI zingekuwa na vyoo ndani vya wateja.
Ni kweli Benki nyingi hapa mjini zipo kwenye majengo yenye ofisi nyingi au zimepanga kwenye majengo yanayomilikiwa na watu au kampuni binafsi, Hali ya vyoo huwa ni kawaida. Benki zinatakiwa kuwa na vyoo rasmi kwa ajili ya wateja wao.
Kikawaida Benki zinatakiwa kutoa huduma kwa haraka siyo kuweka watu muda mrefu! Hivyo hitaji ya vyuo ni kidogo japo ni muhimu viwepo kwasababu benki zinachukua muda mrefu kutoa huduma. Ni vyema wawe na huduma hii kuzingatia na huduma wanazotoa ambapo watu hukusanyika na kusubiri huduma.
Unapotoa huduma kwa watu, na huduma ya choo ni lazima, kwa vile watu wanakaa muda mrefu wakisubiria huduma, hivyo, benki zilipaswa kutoa huduma. Huduma za Benki ni huduma za jamii, na kwenye jamii lazima kuwe na huduma za maliwato. Popote penye mkusanyiko wa watu huduma ya choo ni muhimu kibinaadamu, Ukipenda boga ppenda pamoja na ua lake.
Ninaomba taasisi hizo ziangalie huduma hii na huduma hii iwe pia ni rafiki kwa walemavu. Benki nyingi hapa Tanzania huduma ya Choo hawaitambui kama ni moja Kati ya huduma kwa wateja.
Tunaelewa jambo hili, linagharimu pesa kutoa vyoo vya umma, itagharimu pesa kuvitengeneza, kuvifunga na kisha kuvitunza. Lakini mnaweza kugeuza fursa hii ikawa kama mradi wa hapo ofisini, kama taasisi zingine zinavyofanya, kutoa huduma kwa njia ya kulipia unapoenda kwenye choo, na pesa hizo zinasaidia kuendesha huduma hiyo hapo ofisini.
Hapo mtakuwa mmefanya kwa wema wa mioyo yenu. Na kudumisha nia njema ya wateja wenu.
Tunaelewa kwamba benki zinaweza kukosa nafasi ya kuchukua vyumba na kuvigeuza kuwa vyoo kwa wateja wao. Zaidi ya hayo, huenda benki zisitake kuhimiza wasio wateja kukaa katika majengo yao kwa muda mrefu. Baadhi ya benki pia huenda zisitake kulipia gharama za ziada zinazohusiana na kutunza vyoo vya umma. Inawezekana pia kwamba baadhi ya benki zinaweza kuwa na vyoo vya umma hapo awali lakini zimeviondoa kwa sababu ya matatizo ya matengenezo au matumizi mabaya.
Lakini hoja ni kwamba kama matatizo yote hayo yanafahamika Benki inashindwa vipi kuja na ufumbuzi wa utatuzi kunako shida hiyo?
Hii si haki. Hatungependa kushuhudia matukio ya wateja kupata aibu na kudhalilika hadharani. Uwepo wa huduma ya choo sio suala dogo kwa kweli, ni suala kubwa la kiafya ambalo linapaswa kushughulikiwa.
Benki nyingi katika hili zinawatesa wateja wao. Ninaona kuwa haiwezekani kwa ‘’wateja wanaoheshimiwa’’ kama benki zinavyowaita, kulazimika kukimbia katikati ya shughuli ili kutafuta vyoo sehemu za nje vilivyo karibu na jumba la benki.