Jamaa mmoja alikwenda hoteli hana pesa akataka apewe chakula, akakataliwa. Basi jamaa akawatisha alipowaambia nitafanya kama alivyofanya kaka yangu jana. Wale watu wakaogopa wakijua kwamba jamaa ni mkorofi au kaka yake baunsa, wakampa chakula. Alipomaliza wakamuuliza tuambie kaka yako alifanya nini jana, jamaa akawaambia alilala bila ya kula.