Bashungwa amsimamisha Meneja wa TANROADS - Lindi, akuta mtaalam wa Falsafa na Wananchi wakisimamia ujenzi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemsimamisha kazi Meneja wa TANROADS Mkoa wa Lindi, Eng. Andrea Kasamwa kwa kushindwa kusimamia urejeshwaji wa miundombinu ya barabara na madaraja katika Wilaya ya Liwale Mkoani Lindi na kupelekea barabara kuu zinanounganisha wilaya hiyo na maeneo mengine kufungwa.

Waziri Bashungwa akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Deo Ndejembi ameshuhudia urejeshwaji wa barabara ya Liwale - Nangurukuru iliyosombwa na maji ikisimamiwa na Mtaalam mwenye taaluma ya Falsafa kwa kusaidiwa na Wananchi wakati Mkandarasi akiwa hayupo eneo la Kazi.
WhatsApp Image 2024-03-06 at 16.22.18_b8a81ddb.jpg

WhatsApp Image 2024-03-06 at 16.22.20_7b78acff.jpg

WhatsApp Image 2024-03-06 at 16.22.20_6c973469.jpg
Bashungwa amechukua hatua hiyo leo tarehe 06 Machi 2024 wakati akikagua mindombinu ya barabara katika Wilaya ya Liwale na kutoridhishwa na usimamizi wa kazi inayofanywa na Wakala wa Barabara (TANROADS) mkoa wa Lindi.

“Haiwezekani sisi tutoke Dodoma hadi huku Liwale kutokana na changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara iliyopo, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amelazimika kutoa Helikopta yake tufike huku, lakini hapa site hakuna Mkandarasi, mnaweka mtu aliyesoma falsafa kusimamia kazi ya ujenzi wa barabara”, ameeleza Bashungwa.
WhatsApp Image 2024-03-06 at 16.22.07_fd6e8b9a.jpg

WhatsApp Image 2024-03-06 at 16.22.06_ce874342.jpg
Aidha, Bashungwa amemuagiza Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Mohamed Besta, kuleta Wataalam na kuhakikisha ndani ya siku nne barabara zote kuu na madaraja yanayounganisha Wilaya ya Liwale na maeneo mengine katika mkoa huo ambayo hayapitiki yawe yamefunguliwa na kuendelea kutoa huduma kwa wananchi.

Kadhalika, Waziri Bashungwa amesema Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshatoa fedha ya kumtafuta Mkandarasi wa kujenga barabara ya Masasi - Nachingwea - Liwale km 175 kwa kiwango cha lami ili kumaliza changamoto inayoendelea kujitokeza ya kufungwa kwa barabara.

Bashungwa ameeleza kuwa Serikali itaanza kujenga kwa awamu barabara ya Nangurukuru - Liwale yenye urefu wa kilometa 230 kwa kiwango cha lami ambapo amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi kutenga fedha na kumtafuta Mkandarasi kwa ajili ya kuanza ujenzi kipande cha kilometa 10 kwa kiwango cha lami.

Kwa Upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack amesema ataendelea kufuatilia kwa ukaribu kazi zote ikiwemo urejeshwaji wa miundombinu katika Mkoa huo hasa Wilaya ya Liwale, Nachingwea na Ruangwa na hatasita kumchukulia hatua Mkandarasi na Mtaalam yoyote anayeshindwa kutekeleza majukumu yake ilasavyo

Naye, Mbunge wa Liwale, Zuberi Kuchauka ameishukuru Serikali kwa kuanza kuchukua hatua za kurejesha mawasiliano ya barabara kutokana na changamoto kubwa ya barabara na madaraja yanayounganisha wilaya ya Liwale na maeneo mengine kujaa maji na kupelekea kufungwa hadi sasa.
 
“Haiwezekani sisi tutoke Dodoma hadi huku Liwale kutokana na changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara iliyopo, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amelazimika kutoa Helikopta yake tufike huku, lakini hapa site hakuna Mkandarasi, mnaweka mtu aliyesoma falsafa kusimamia kazi ya ujenzi wa barabara”, ameeleza Bashungwa.
Mbarawa anasemaje
 
Back
Top Bottom