Based on true story: Mahaba yalivyonipeleka kwenye Jamii za Siri Ulimwenguni

Roca fella

JF-Expert Member
May 13, 2023
1,249
2,341
Ni miaka 7 Sasa tangu atangulie mbele za haki mama huyu wa kizungu anaitwa, Charlotte Nelson William.
ee6b52c9edc34ea81eedba40e91bbbed.jpg

Charlotte Nelson William, enzi za uhai wake katika jumuiya ya Freemason nchini uingereza.

Miaka ya nyuma niliwahi kufanya kazi za ufundi gari, lakini nikiwa Kama kibarua wa muda, yaani day worker. Sasa nilipigiwa simu na moja wa vijana ambao walikuwa wananipa kazi hizo, akanieleza Kuna kazi ya kurekebisha gari ya mwingereza Aina ya Land Rover discovery. Maeneo ya Serena hotel jijini dar es salaam.

Nikafika eneo la tukio, nikakutana na huyu mama Charlotte hapo Serena hotel, akanieleza tatizo la gari yake, nami nikafanya ufundi wangu, nikafanikiwa kutengeza ilikuwa ni tatizo dogo tu, ila wenzetu hukwepa usumbufu usio wa tija.
Wakati nasubiri nikabidhi gari na nipokee pesa, akaja yule mama was kizungu, akakagua gari akanipa hongera Sana akanishukuru kumkamilishia jambo lake,
Akanilipa pesa, akanieleza unaitwa nani, nikamjibu, una umri gani, nikamjibu. Akaingia kwenye gari na kuchukua business card yake na kunipa akiomba ni mtafute.

Usiku nilimtafuta yule mama kwa njia ya WhatsApp tukawasiliana, hivyo kila Mara tulijenga mazoea ya kuwasiliana. Siku moja akanipa mwaliko katika ukumbi ya 9744 iliyo jijini dar es salaam na kuniambia nivae nguo nyeusi ikipendeza shati jeusi, suruali nyeusi, soksi na kiatu cheusi, nikimaliza tukutane Serena hotel twende mpaka hiyo ukumbi 9744.

Bila hiyana nikajiandaa nikavaa Kama nilivyo ambiwa, nikaenda Serena hotel, tulikutana pamoja na wazungu wengine wakiwa katika vazi la nguo nyeusi wote. Tulienda na gari wote tukielekea huko ukumbi 9744, muda huo ni saa 12 jioni, tulifika tukapokelewa vizuri kila wenye kadi waonyesha mlangoni, ambao hatuna tulivaa vitambulisho vyao shingoni, tukaonyeshwa pa kukaa wageni na wenyeji wakaa kivyao kulingana na vyeo vyao muda huo tupo ndani ya ukumbi 9744.
Huku tukiendelea kusubiri watu wengine wakaribishwe kwenye mwaliko. Saa 1 usiku ukumbi ulijaa watu wanawake kwa wanaume, tulikaribishwa kula chakula Cha usiku hapo ukumbi namba 9744,
Chakula kilikuwa kitamu Sana, walijua vyema upishi, lakini Cha kushangaza huu mwaliko si bure Bali unahitaji ugharimie yaani ulipie bili, chakula nilicho kula bili ilikuwa elfu 25000/- nikalipia bili, huku wageni na wenyeji wakisubiri maelekezo mengine kwa mkuu wao wa ukumbi namba 9744 jijini dar es salaam.

MKASA HUU UTAENDELEA.........

Muendelezo sehemu ya pili - Sehemu ya 2
 
Karibu saana
Ni miaka 7 Sasa tangu atangulie mbele za haki mama huyu wa kizungu anaitwa, Charlotte Nelson William.
View attachment 2648960
Charlotte Nelson William, enzi za uhai wake katika jumuiya ya Freemason nchini uingereza.

Miaka ya nyuma niliwahi kufanya kazi za ufundi gari, lakini nikiwa Kama kibarua wa muda, yaani day worker. Sasa nilipigiwa simu na moja wa vijana ambao walikuwa wananipa kazi hizo, akanieleza Kuna kazi ya kurekebisha gari ya mwingereza Aina ya Land Rover discovery. Maeneo ya Serena hotel jijini dar es salaam.

Nikafika eneo la tukio, nikakutana na huyu mama Charlotte hapo Serena hotel, akanieleza tatizo la gari yake, nami nikafanya ufundi wangu, nikafanikiwa kutengeza ilikuwa ni tatizo dogo tu, ila wenzetu hukwepa usumbufu usio wa tija.
Wakati nasubiri nikabidhi gari na nipokee pesa, akaja yule mama was kizungu, akakagua gari akanipa hongera Sana akanishukuru kumkamilishia jambo lake,
Akanilipa pesa, akanieleza unaitwa nani, nikamjibu, una umri gani, nikamjibu. Akaingia kwenye gari na kuchukua business card yake na kunipa akiomba ni mtafute.

Usiku nilimtafuta yule mama kwa njia ya WhatsApp tukawasiliana, hivyo kila Mara tulijenga mazoea ya kuwasiliana. Siku moja akanipa mwaliko katika ukumbi ya 9744 iliyo jijini dar es salaam na kuniambia nivae nguo nyeusi ikipendeza shati jeusi, suruali nyeusi, soksi na kiatu cheusi, nikimaliza tukutane Serena hotel twende mpaka hiyo ukumbi 9744.

Bila hiyana nikajiandaa nikavaa Kama nilivyo ambiwa, nikaenda Serena hotel, tulikutana pamoja na wazungu wengine wakiwa katika vazi la nguo nyeusi wote. Tulienda na gari wote tukielekea huko ukumbi 9744, muda huo ni saa 12 jioni, tulifika tukapokelewa vizuri kila wenye kadi waonyesha mlangoni, ambao hatuna tulivaa vitambulisho vyao shingoni, tukaonyeshwa pa kukaa wageni na wenyeji wakaa kivyao kulingana na vyeo vyao muda huo tupo ndani ya ukumbi 9744.
Huku tukiendelea kusubiri watu wengine wakaribishwe kwenye mwaliko. Saa 1 usiku ukumbi ulijaa watu wanawake kwa wanaume, tulikaribishwa kula chakula Cha usiku hapo ukumbi namba 9744,
Chakula kilikuwa kitamu Sana, walijua vyema upishi, lakini Cha kushangaza huu mwaliko si bure Bali unahitaji ugharimie yaani ulipie bili, chakula nilicho kula bili ilikuwa elfu 25000/- nikalipia bili, huku wageni na wenyeji wakisubiri maelekezo mengine kwa mkuu wao wa ukumbi namba 9744 jijini dar es salaam.

MKASA HUU UTAENDELEA.........
Unitag ukiendelea
 
Back
Top Bottom