"Babu" na mseto wa kauli zake

Mohammed Hamad

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
3,988
1,304
Wote tumeshuhudia media inavyotupasha habari kila uchao kuhusu yanayojiri kule kijiji cha Semunge wilaya ya Loliondo. Babu amekuwa kwenye kurasa za mbele za magazeti yetu kila uchao na kutufanya kusahau mambo muhimu ya nchi. Hii ni faraja kwa baadhi ya watu kwani kwa kiasi fulani wamepumua na ni hasara kwa wale wengine kwani sasa hivi hakuna asikiae malalamiko yao watu wako bize na "babu".


Babu kazungumziwa sana na yeye kuzungumza nimeanzisha thread hii ili kila alichosema babu tuki quote then tu read between the lines.

Dawa hii ni lazima unywee hapa hapa na si mahala pengine na mtu anayetakiwa akunyweshe ni mimi tu
Mchungaji Masapila pia alisema kazi ambayo amekuwa akifanya kwa saa zaidi za 13 kila siku, haimsumbui akidai kwamba tayari alikwishamuuliza Mungu kwamba atawezaje kutoa tiba kwa watu wengi ilihali ni mzee na akaelezwa kuwa ataongezewa nguvu.
Naishukuru Serikali maana naona wananiunga mkono, hii ni dawa kutoka kwa Mungu na wala sio mti pekee na nilijua wakipima hawatakuta madhara yoyote kwani Mungu alikwishanieleza kuwa watapima wataalamu wa ndani na nje ya nchi dawa hii na watakuta haina madhara
Hakuna madhara kwa mgonjwa kuendelea na dawa zake za awali hata baada ya kunywa dawa yake na kwamba si vyema kuacha ghafla kutumia dawa hizo
 
Mimi nilimuuliza swali: Kwa mfano nimekuja hapo nina ukimwi, nimekunywa dawa na kupona, nimerudi nyumbani lakini kwa bahati mbaya nikapata kisukari, je naweza kuja kunywa dawa mara ya pili kwa ugonjwa huu mpya? Alisema "sina jibu" Kwa kadri nilivyooteshwa mtu atakunywa dawa hii mara moja tu; kwamba sasa uje mara ya pili kwa ugonjwa tofauti - sina jibu. Lakini Mungu si wa hivyo - yaani leo uje na ugonjwa sugu unywe dawa upone halafu upate tena ugonjwa mwingine sugu? Hakika Mungu si wa hivyo - ila ikitokea hivyo - sina jibu!

kazi ipo!

source:https://www.jamiiforums.com/jf-chit-chat/119766-hoja-ya-shossi-juu-ya-sh-500-ya-babu-17.html

"Nawaomba muwaheshimu viongozi wanaokuja hapa kwani mbali ya kuja kupata tiba wanafika kuona namna ya kuboresha hali ya mazingira ili tiba hii iweze kuwa endelevu," alikaririwa Babu akisema.
eti tiba ya Mungu isiporatibiwa na viongozi wa serikali haitakuwa endelevu!! tafakari huyu ni Mungu gani?

source:Waziri Simba aonja joto ya jiwe kwa Babu
 
simshabikii sana babu lakini kama source ya hizi quotes ni magazeti, then sina uhakika na credibility ya hizi quotes. for obvious reasons...

kama kuna video clips, zinaweza kusaidia zaidi....ziweke hapa ili tuzijadili.
 
simshabikii sana babu lakini kama source ya hizi quotes ni magazeti, then sina uhakika na credibility ya hizi quotes. for obvious reasons...

kama kuna video clips, zinaweza kusaidia zaidi....ziweke hapa ili tuzijadili.

Thomaso!!
 
{QUOTE=Miss Judith;1797201]kazi ipo!

source:https://www.jamiiforums.com/jf-chit-chat/119766-hoja-ya-shossi-juu-ya-sh-500-ya-babu-17.html

eti tiba ya Mungu isiporatibiwa na viongozi wa serikali haitakuwa endelevu!! tafakari huyu ni Mungu gani?

source:Waziri Simba aonja joto ya jiwe kwa Babu}

Kumbuka kuwa ya kaisali mpeni kaisali na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu, Lakini pia haiishii hapo tu tunahimizwa kuzitii mamlaka zote zilizopo duniani kwani mamlaka hizo zimewekwa na Mungu. Kwa mantiki hiyo sioni kama babu alikosea chochote.
 
simshabikii sana babu lakini kama source ya hizi quotes ni magazeti, then sina uhakika na credibility ya hizi quotes. for obvious reasons...

kama kuna video clips, zinaweza kusaidia zaidi....ziweke hapa ili tuzijadili.

Ni kauli zilizonukuliwa kwenye mahojiano kadha wa kadha na kusikiwa na watu wengi kupitia Television!
 
{QUOTE=Miss Judith;1797201]kazi ipo!

source:https://www.jamiiforums.com/jf-chit-chat/119766-hoja-ya-shossi-juu-ya-sh-500-ya-babu-17.html

eti tiba ya Mungu isiporatibiwa na viongozi wa serikali haitakuwa endelevu!! tafakari huyu ni Mungu gani?

source:Waziri Simba aonja joto ya jiwe kwa Babu}

Kumbuka kuwa ya kaisali mpeni kaisali na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu, Lakini pia haiishii hapo tu tunahimizwa kuzitii mamlaka zote zilizopo duniani kwani mamlaka hizo zimewekwa na Mungu. Kwa mantiki hiyo sioni kama babu alikosea chochote.

suppose kwamba serikali imeamua kuipinga hii huduma, ina maana haitakuwa endelevu na mwishowe itakufa?

tangu uzaliwe hadi leo umeshaona huduma gani iliyoanzishwa na inayoungwa mkono na Mungu wa kweli imekufa kwa sababu ya kukosa uratibu wa serikali? kama unajua historia ya kanisa, nitajie ni lini huduma gani ya Mungu wa kweli ilikufa kwa sababu ilipingwa na serikali?

bado unapaswa kujiuliza tena kwa autulivu mkubwa: ni mungu gani huyu ambaye huduma yake isiporatibiwa na viongozi wa serikali haitakuwa endelevu na hatimaye itakufa?

ee Bwana umenichunguza na kunijua,

wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu


umezifahamu njia zangu zote
 
Babuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu

Hili eneo linakuwa finyu sasa kutokana na wingi wa watu wanaofika kupata tiba. Lazima tuhame na Mungu ameshanionyesha eneo ambalo huduma hii itahamia, ila nasubiri tangazo lake kujua ni lini nitahama

"Hapo kale wenyeji wa eneo hili hawakuwa na utamaduni wa kufanya maziko ya wafu, hivyo watu walipokufa walitupwa kwenye bonde hili," alisema.

Akijibu swali kwamba ni nini maoni yake kuhusu tiba hiyo kuhamishiwa eneo la wafu, Mchungaji Masapila alijibu kwa kifupi akisema; "Lilikuwa ni eneo la wafu, lakini Mungu anataka sasa pawe ni mahali pa ufufuo.

Naona "babu" karibu ataanza kufufua wafu teh teh teh teh................
 
Jamani wana JF. Mimi ninafanya kazi hapa Halmashauri ya Wilaya Ngoro2, makao makuu yake ni Loliondo. Kutoka hapa kwenda Sami=unge ni km 56Km hivi

Mi naomba tu niwaondoe dukuduku maana nyie mpo mbali na hapa.

Ni hivi, Hapa tulipo tulio wengi hatujaenda kwa babu kwa maana ya ule usemi "Nabii hakubaliki kwao". sisi tunaendelea kuwashangaa tu wapitaji wanaotokea kanda ya ziwa kwenda kwa babu maana njia ni hapa kwetu.

cha ajabu zaidi ni kwamba watu tunaendelea kugawanyika kila uchao maana kila siku tunasikia na kuona baadhi ya mabo mapya maana kila mtu anasema la kwake.
wengine wana mashaka na namna alivyoanza; kwamba, Wakuu wa makanisa hasa yale wanayojiita "makanisa ya kiroho" huko mijini kwenu DSM, Mwanza nk karibu wote wanatoka Mbeya (kasoro Rwakatare nk) wengine wote wanatokea Mbeya. watu wanahoji, je MBEYA tu ndiko Mungu anakoona kuwa kunafaa sana watu wa maajabu watokee?(ukizingatia babu naye ni mtu wa mbeya)

Je Mungu haoni mahala pengine??

Pili, babu haishi na familia yake hapo samunge, kaiacha Babati miaka mingi, mh, hii nayo ni sawa??

Tatu, babu ni mch.mstaafu, uliwahi kuona wapi manabii wa Mungu wote walioandikwwa kwenye Biblia wamefanya maajabu lakini kwa malipo? (hata kama ni kidogo?) walipewa bura lakini wakatoa bure pia, babu yeye analipisha kidogo 500/= ni sawa kibiblia? au ndo mambo mapya ya Mungu?

Nne, Babu anasema asipo kupa yeye dawa huponi, mbona kwenye biblia hata Yesu, nabii Elisha nk wenyewe walisema tu neno na mtu akapona hukohuko alipo?? hii ya babu ni mpya??

Tano, kama ni Mungu kweli, mbona ameruhusu na wengine wajitangaze kuwa wanatoa dawa kama ya babu?? Si angeacha tu babu aendelee kugawa dose??
Tutawatambuaje???????

Sita, saba nk, ngoja niishie hapo nisije nikawaondolea imani wana JF ambao walikuwa na mpango wa kuja!

kwa ujumla hili suala bado lina utata sana, niwaombe tu kwamba msome Mathayo 7, Luka 21, na Mathayo 24 mtaona namna Yesu mwenye alivyotahadharisha watu wake juu ya mabo haya hasa ukizingati hizi ni "siku za mwisho"

Nitaendelea kutoa ufafanuzi kadri mtakavyohitaji.
 
hahah, babu bado tu anaendelea kuota?

siku ile itakuja kama mwivi

Babu ndoto yake ni ndefu sanaaaaaa kama sinema ya kihindi kwahiyo kila aakikumbuka scene anasimulia tehe teh teh.............kuna sehemu walimnukuu alisema kiama bado siku 59 nikajiuliza kama kiama bado siku 59 wale watu wanaotaabika porini wanaenda kufanya nini wasiosubiri mwisho wa dunia na kujiweka busy kuupata uzima wa milele kuliko kuupata uzima wa miezi miwili.
 
Jamani wana JF. Mimi ninafanya kazi hapa Halmashauri ya Wilaya Ngoro2, makao makuu yake ni Loliondo. Kutoka hapa kwenda Sami=unge ni km 56Km hivi

Mi naomba tu niwaondoe dukuduku maana nyie mpo mbali na hapa.

Ni hivi, Hapa tulipo tulio wengi hatujaenda kwa babu kwa maana ya ule usemi "Nabii hakubaliki kwao". sisi tunaendelea kuwashangaa tu wapitaji wanaotokea kanda ya ziwa kwenda kwa babu maana njia ni hapa kwetu.

cha ajabu zaidi ni kwamba watu tunaendelea kugawanyika kila uchao maana kila siku tunasikia na kuona baadhi ya mabo mapya maana kila mtu anasema la kwake.
wengine wana mashaka na namna alivyoanza; kwamba, Wakuu wa makanisa hasa yale wanayojiita "makanisa ya kiroho" huko mijini kwenu DSM, Mwanza nk karibu wote wanatoka Mbeya (kasoro Rwakatare nk) wengine wote wanatokea Mbeya. watu wanahoji, je MBEYA tu ndiko Mungu anakoona kuwa kunafaa sana watu wa maajabu watokee?(ukizingatia babu naye ni mtu wa mbeya)

Je Mungu haoni mahala pengine??

Pili, babu haishi na familia yake hapo samunge, kaiacha Babati miaka mingi, mh, hii nayo ni sawa??

Tatu, babu ni mch.mstaafu, uliwahi kuona wapi manabii wa Mungu wote walioandikwwa kwenye Biblia wamefanya maajabu lakini kwa malipo? (hata kama ni kidogo?) walipewa bura lakini wakatoa bure pia, babu yeye analipisha kidogo 500/= ni sawa kibiblia? au ndo mambo mapya ya Mungu?

Nne, Babu anasema asipo kupa yeye dawa huponi, mbona kwenye biblia hata Yesu, nabii Elisha nk wenyewe walisema tu neno na mtu akapona hukohuko alipo?? hii ya babu ni mpya??

Tano, kama ni Mungu kweli, mbona ameruhusu na wengine wajitangaze kuwa wanatoa dawa kama ya babu?? Si angeacha tu babu aendelee kugawa dose??
Tutawatambuaje???????

Sita, saba nk, ngoja niishie hapo nisije nikawaondolea imani wana JF ambao walikuwa na mpango wa kuja!

kwa ujumla hili suala bado lina utata sana, niwaombe tu kwamba msome Mathayo 7, Luka 21, na Mathayo 24 mtaona namna Yesu mwenye alivyotahadharisha watu wake juu ya mabo haya hasa ukizingati hizi ni "siku za mwisho"

Nitaendelea kutoa ufafanuzi kadri mtakavyohitaji.

mpendwa, haya yote uliyoweka hapa leo tulishayyajadili hapa kwa siku kadhaa sasa na baadhi yetu tumekaribia kung'olewa macho na mashabiki wa babu. lakini hatuachi na tunaendelea kuyajadili hapa hadi ukweli ujulikane na kila mtu.

karibu sana katika mjadala unaoendelea na tunafarijika kupata mtu anayemjua babu na mazingira yake na hata familia yake

angalau leo tumejua kuwa babu katelekeza familia yake na kujichimbia kijijini samunge huku familia yake ikiteseka kwa kukosa mapenzi ya baba yao na labda hata mahitaji ya kimaisha na babu huyu hajali. kweli huyo mungu wake kiboko

basi kwa kuwa tumezungukwa na wingu kuwa la mashahidi namna hii,
na tuweke kando mzigo wa dhambi ile ituzingayo kwa upesi
 
Back
Top Bottom