".....baba mbona hua ninafanya hivi kila siku...!?"

driller

JF-Expert Member
Aug 25, 2011
1,116
246
haya..haya...haya..hayaaaa!!! wanajamii..! kwanza nawatakia ..EID MUBBARAKH...

hii ni kali ya leo.. kama kawaida yangu mzee wa mitaani..! leo nimepata kitu flani bwana kilitokea mitaa ya mkoa wa tanga huko kwenye milima ya usambaa yani ilikua ni noma kinyama wazeeiya..!

kama ulikua hujui kua kati ya sehemu ambazo wajerumani wakati wa ukoloni walipapenda na hata sasa hivi kusema kweli wanapapenda sana..!
kiasi kwamba kupitia shirika lao la gtz ambalo sasa ni giz hua wakija mkoani tanga ni lazima wapitie lushoto kabla hawajakwea mapipa yao kwenda zao kwao...!
sasa katika jimbo moja la wilaya hiyo.. kuna hospitali flani ambayo waliijenga wao na wakajenga na nyumba za wafanyakazi hapo hospitalini..! well to make the long story short ni kwamba nyumba zote za wafanyakazi zinafanana...! vyoo vya zile nyumba vina dirisha moja ambalo liko juu ya flushing tank.. sasa kama unavyojua ndugu msomaji wabongo ni watu wa kurahisisha mambo sana..! jamaa akawa anaweka miswaki juu ya flushing tank karibu na dirisha...
sasa ilitokea choo kilikua na matatizo flani hivi ikawa wanasubiri spea za kutoka hospitalini coz zile nyumba zina fanyiwa matengenezo na hospitali na matatizo yale yaliwafanya wanafamilia kutokua na uwezo wa kutumia flushing tank.. yaani iliwabidi wawe wanamwaga maji ili kupeleka waste zao..! sasa walikua na mtoto mdogo pale ndani ambae alikua ni mvivu kufika pale dirishani kwenda kuichukua miswaki.. na kusema kweli miswaki ya familia nzima ilikua pale juu kwenye kakopo flani hivi..!
siku moja dogo yuko na dingi wanataka kupiga mswaki..! dingi akamuacha dogo achukue kwanza mswaki halafu yeye atachukua baadae..! dogo akaruka kidogo akagusa lile kopo na miswaki yoote ikadondoka kwenye tundu la choo.....NB; choo kilikua cha kukaa.....
then kwa mshangao dingi akawa ametulia tu anaona nini kinaendelea..
yule dogo akaokota miswaki yote na akachagua wa kwake na mingine akairudisha kwenye kopo na kuirudisha tena dirishani..!
yule dingi alikasirika akamuuliza yule dogo .." yani ndio unavyochukua miswaki hivyo..?"" dogo akamwambia mzee .."baba mbona hua nafanya hivi kila siku..!?" haaaaaapo sasaaaaaa weeeeeee....!
 
Back
Top Bottom