Katika hali isiyotarajiwa na inayotia shaka Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chadema Ndugu Godbless Lema amekutwa Bar akiwa amekaa na viongozi wa andamizi wa Chama Cha Mapinduzi katika Bar ya Family Pub mjini Arusha kuanzia saa tatu usiku na kuendelea huku wakiwa wenye furaha.Ikiwa haiujulikani ni kwa vipi jambo hili limetokea wakati Mgombea wa CCM Jakaya Kikwete akiwa mjini Arusha kwa ziara rasmi ya kampeni.
- Maswali ya kujiuliza ni kwa vipi mwenyekiti wa CCM Ndugu Jublate Kileo awepo Bar na Mgombea wa Chadema wakati ambao mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho akiwa bado mjini hapa?ina maana hawana mazungumzo ya mikakati ya kulitwaa jimbo au ndo mkakati ni kumchakachua GODLESS LEMA
- Je kwanini wawepo mda huo mahali hapo au ndo kuthibitisha kuwa Jublate hamuungi mkono Dr Batilda Buriani kwani alikuwa kundi la Felix Mrema?
- Ndo kusema sasa CCM wanataka kumchakachua Godless Lema arudishe kadi na kujitoa kugombea Ubunge hapa Arusha mjini?ni muda tu utakaosema.Nategemea sana wahusika wote watatoa ufafanuzi wa kina au kama walikuwa wana mazungumzo ya kawaida nani ajuaye