ToniXrated
JF-Expert Member
- Sep 21, 2022
- 1,135
- 2,976
Amani iwe nanyi.
Nikiwa kama mdau wa michezo, napenda kuishauri kampuni ya habari ya AZAM kuhakikisha kuwa uwekezaji wao wanaoufanya katika tasnia ya michezo unaendana sambamba na kuwapa elimu ya msingi (basic education) watangazaji na wachambuzi wao.
Niipongeze kampuni ya Azam Media katika juhudi zake za kufufua michezo ya mpira,ndondi n.k ila inatakiwa ishirikiane na vyama vya michezo husika katika kuwapa elimu hawa watangazaji wao kina Baraka Mpenja,pascal kabombe,iddi salum,hashim ibwe,patrick Nyembera n.k kuhusiana na michezo wanayoitangaza.
Kama mtangazaji anatangaza kuhusu masuala ya mpira mathalani mechi basi awe na elimu ya awali kuhusiana na mpira na si kutangaza tu fulani kachukua boli kampa yule, mayele katetema, sakho kanyunyiza n.k
MaJuzi kuna tukio lilitokea kwenye boxing katika mechi ya Mandonga dhidi ya Salum Abeid, Mandonga aliangishwa chini ,Refa akawa anamtoa mpinzani wa mandonga asiendelee kumshambulia mandonga akiwa chini.Huku watangazaji wakawa wanapayuka kuwa refa hafai ,afungiwe n.k kwanza katika ethics za utangazaji huwezi kusema refa afungiwe kwasababu huna mamlaka hayo. Tunaona blunders zikifanywa na marefa wa Epl ila huwezi kumsikia mtangazaji kama Peter Drury akipayuka kuwa marefa wafungiwe n.k.
Hivyo basi kampuni ya Azam Media ihakikishe watangazaji wake wanapatiwa elimu juu ya michezo wanayoitangaza kabla hawajashika microphone au wahakikishe kuwa wanaweka mtangazaji namba mbili ambaye atakuwa akisaidiana na hawa watangazaji kuchambua aspects of the game kama sheria, masuala ya kimbinu n.k. kama wanavyofanya katika mataifa yaliyoendelea kimichezo huko ulaya na America.
Mechi za ulaya hutangazwa na watangazaji wawili , wa kwanza huwa ni mtangazaji wa kawaida ila mtangazaji wa pili ni lazima awe alicheza soka la kulipwa au ana taaluma ya ukocha mfano mzuri ni Andy Townsend anayefanya uchambuzi wakati mechi inaendelea. Ina maana ana uwezo wa kuelezea mabadiliko ya kimbinu yanayofanywa na makocha n.k
Hata katika boxing/basketball lazima wawepo watangazaji ambao walikuwa ni wachezaji hapo kabla au makocha. Mfano mzuri ni combination ya Jesse john na marehemu Mwalimu Kashasha.
Ni hayo tu.
Nikiwa kama mdau wa michezo, napenda kuishauri kampuni ya habari ya AZAM kuhakikisha kuwa uwekezaji wao wanaoufanya katika tasnia ya michezo unaendana sambamba na kuwapa elimu ya msingi (basic education) watangazaji na wachambuzi wao.
Niipongeze kampuni ya Azam Media katika juhudi zake za kufufua michezo ya mpira,ndondi n.k ila inatakiwa ishirikiane na vyama vya michezo husika katika kuwapa elimu hawa watangazaji wao kina Baraka Mpenja,pascal kabombe,iddi salum,hashim ibwe,patrick Nyembera n.k kuhusiana na michezo wanayoitangaza.
Kama mtangazaji anatangaza kuhusu masuala ya mpira mathalani mechi basi awe na elimu ya awali kuhusiana na mpira na si kutangaza tu fulani kachukua boli kampa yule, mayele katetema, sakho kanyunyiza n.k
MaJuzi kuna tukio lilitokea kwenye boxing katika mechi ya Mandonga dhidi ya Salum Abeid, Mandonga aliangishwa chini ,Refa akawa anamtoa mpinzani wa mandonga asiendelee kumshambulia mandonga akiwa chini.Huku watangazaji wakawa wanapayuka kuwa refa hafai ,afungiwe n.k kwanza katika ethics za utangazaji huwezi kusema refa afungiwe kwasababu huna mamlaka hayo. Tunaona blunders zikifanywa na marefa wa Epl ila huwezi kumsikia mtangazaji kama Peter Drury akipayuka kuwa marefa wafungiwe n.k.
Hivyo basi kampuni ya Azam Media ihakikishe watangazaji wake wanapatiwa elimu juu ya michezo wanayoitangaza kabla hawajashika microphone au wahakikishe kuwa wanaweka mtangazaji namba mbili ambaye atakuwa akisaidiana na hawa watangazaji kuchambua aspects of the game kama sheria, masuala ya kimbinu n.k. kama wanavyofanya katika mataifa yaliyoendelea kimichezo huko ulaya na America.
Mechi za ulaya hutangazwa na watangazaji wawili , wa kwanza huwa ni mtangazaji wa kawaida ila mtangazaji wa pili ni lazima awe alicheza soka la kulipwa au ana taaluma ya ukocha mfano mzuri ni Andy Townsend anayefanya uchambuzi wakati mechi inaendelea. Ina maana ana uwezo wa kuelezea mabadiliko ya kimbinu yanayofanywa na makocha n.k
Hata katika boxing/basketball lazima wawepo watangazaji ambao walikuwa ni wachezaji hapo kabla au makocha. Mfano mzuri ni combination ya Jesse john na marehemu Mwalimu Kashasha.
Ni hayo tu.