AXIS OF EVIL: TANESCO/Mkono Advocates/Rex Attorneys/IPTL/Richmond/Dowans

mmakonde

JF-Expert Member
Dec 26, 2009
965
66
Katika kipindi cha miaka mitano tu iliyopita, serikali imetumia zaidi ya Sh. 23 bilioni kujitetea, kwa kulipa makampuni ya uwakili. Gharama hizi zinaongezeka mwaka hadi mwaka kufuatia kesi kuchukua muda mrefu na hata kufumuka kwa kesi mpya.

Sehemu ya mabilioni hayo ya shilingi imelipwa kwa makampuni ya wanasheria ya Mkono and Company Advocates ya Tanzania na Hunton and William ya Marekani kwa kutetea TANESCO iliyoshitakiwa na kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL).


Mabilioni mengine yamelipwa kwa makampuni ya mawakili ya Rex Attorney ya Tanzania na Reed Smith ya Uingereza kwa kutetea TANESCO katika kesi iliyofunguliwa na kampuni ya Richmond Development Company (LLC).


Rex Attorneys na Reed Smith wamelipwa au watalipwa pia mabilioni ya shilingi kwa kutetea TANESCO katika shauri lililofunguliwa na makampuni ya Dowans Holdings S.A na Dowans Tanzania Limited (DTL) katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa kibiasha (ICC).


Nyaraka zinaonyesha kuwa tayari Mkono and Company Advocates na Hunton and William wamelipwa na TANESCO kiasi cha dola 11,818,542.89 (sawa na karibu Sh. 17 bilioni).


Kampuni ya Mkono and Company Advocates inamilikiwa na mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono.


Aidha, kampuni ya Mkono imelipwa pia kiasi cha Sh. 8.5 milioni kwa kusimamia shauri lililofunguliwa na benki ya Standard Chartered Bank ya Hong Kong dhidi ya serikali katika shauri la kukatisha mkataba wa IPTL. Serikali na IPTL waliingia mkataba mwaka 1994.


Nyaraka zinaonyesha kuwa Rex Attoney na mwenzake walilipwa kiasi cha dola 3,574,351.51 (karibu Sh. 5 .2 bilioni) katika shauri lililofunguliwa na makampuni ya Dowans Holdings S.A na Dowans Tanzania Limited (DTL) katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa kibiasha (ICC).


Mawakili hao pia wamelipwa dola 860,056.71 (karibu sawa na shilingi 1.2 bilioni) kwa kazi ya kutetea TANESCO dhidi ya kesi iliyofunguliwa na kampuni ya Richmond Development Company (LLC) na kusikilizwa katika Falme za Kiarabu.


Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja mwezi mmoja baada ya mbunge wa Bumbuli (CCM), January Makamba kuibua kile kilichoitwa, "taarifa juu ya upatikanaji wa umeme nchini," ambapo tarehe 3 Februari 2011 alitaka waziri wa nishati na madini, William Ngeleja kueleza hatua zinazochukuliwa na TANESCO katika kukabiliana na mgawo wa umeme na mzigo wa kesi unaolikabili.


Katika barua hiyo, Makamba anasema, "Katika viambatanisho vya hukumu ya ICC, kama ilivyosajiliwa mahakama kuu ya Tanzania zipo nyaraka zinazoonyesha kwamba mwanasheria aliyeishauri TANESCO kuvunja mkataba na Dowans – kwa kusema kwamba siyo mkataba halali na kwamba hakuna madhara ya kisheria kuuvunja – ndiye huyohuyo pia aliyeshauri benki ya Stanbink kutoa mkopo wa dola za 120 kwa Dowans – kwa kusema kwamba ni kampuni halali, inakopesheka na ina mkataba halali na TANESCO."


Anasema, "Ni mwanasheria huyohuyo aliyewakilisha TANESCO kwenye kesi iliyofunguliwa na Dowans, kesi ambayo ilitokana na ushauri wake, na baada ya hukumu ndiye huohuyo, kwa mujibu wa maelezo yako mheshimiwa waziri ya tarehe 6 Januari 2011, aliyetoa ushauri kwamba hakuna njia nyingine zaidi ya kuilipa Dowans."


Makamba alitaka serikali kueleza suala hilo kwa ufasaha ili kuondoa kile alichoita, "picha inayoweza kuonyesha serikali ilikosa umakini kwenye jambo hili zima na maadili hayakuzingatiwa."


Alisema itakuwa vema taarifa ya serikali ikieleza ni wanasheria gani waliotumiwa na TANESCO kwa kila hatua katika shauri lake Dowans kwa kuanzia kwenye ushauri na kabla ya kuvunjwa kwa mkataba.


Akijibu hoja za Makamba, Ngeleja anakiri kuwa benki ya Standard Chartered ya (Hong Kong) ambayo ni benki tanzu ya Standard Chartered ya Uingereza inayomiliki asilimia kubwa ya hisa za IPTL Tanzania Ltd., wameishitaki serikali kwa madai ya kutumia mitambo yake ya kuzalisha umeme kupitia Provisional Liquidator hivyo kukiuka Bilateral Investment Treaty (BIT) kati yake na serikali ya Uingereza.


Kesi hizo ni Na. ARB /10/20 iliyofunguliwa na Standard Chartered Bank (Hong Kong) dhidi ya TANESCO, tarehe 1 Oktoba 2010 na kesi Na.ARB/10/12 iliyofunguliwa tarehe 11 Juni 2010.


Katika shauri hilo, IPTL wanataka mahakama "iamuru serikali kutoa tamko la kukiri kukiuka mkataba wa uwekezaji wa kimataifa – Bilateral Investment Treaty (BIT) na kulipa fidia ya dola 118.6 milioni, pamoja na kulipa gharama zote za uwekezaji - capacity charges – ambazo shirika hilo hazijazilipa tokea mwaka 2007 pamoja na fidia ya dola 130 milioni."


Ngeleja anasema chimbuko la kesi hizo ni mgogoro wa awali kati ya Taneso na na IPTL ambao uliwasilishwa ICSID, Novemba mwaka 2007. Kesi zilizotajwa ziko katika hatua za awali na zinatarajiwa kuanza kusikilizwa Aprili mwaka huu.


Akijibu madai ya njia iliyotumika kupatikana kwa makampuni ya wanasheria, Ngeleja anasema "TANESCO iliona ni busara kuendelea kuwatumia mawakili walewale (Mkono and Company Advocates) kwa kuwa wana taarifa muhimu kuhusiana na kesi husika.


Anasema, "Kampuni ya Mkono ilianza kushughulikia shauri la IPTL tangu mwaka 2007 baada ya kupendekezwa na serikali kuwa washauri wa Kamati ya serikali ya ununuzi wa deni la IPTL. Kutokana na uelewa wa mawakili hao juu ya IPTL, ilionekana ni busara waendeshe kesi hiyo."


Kuhusu kampuni ya wanasheria ya Rex Attorney, Ngeleje anasema, ilipewa kazi ya ushauri baada ya ushindani uliohusisa kampuni tatu za FK Law Chambers, IMMA Advocates na Mkono. Anasema katika shauri la Dowans, TANESCO waliamua kuichukua tena Rex kwa ilikuwa na uzoefu na mkataba huo.


Katika shauri hilo, mahakama ya ICC imeamuru TANESCO kulipa kiasi cha dola 94 milioni (Sh. 134 bilioni) kutokana na kushindwa katika kesi hiyo.


Kwa mujibu wa uchunguzi wa MwanaHALISI, kampuni ya Mkono ililipwa na TANESCO – miezi miwili kabla ya uchaguzi, 19 Agosti 2010 kiasi cha dola 1,088,550.00 (karibu Sh.1.6 bilioni). Malipo hayo yalifanywa kupitia ankara Na. 124/10.


Aidha, kabla ya Mkono kuchukua kitita hicho cha fedha, tarehe 15 Julai 2009, TANESCO walilipa mwanasheria huyo kiasi cha dola 2,177,100.00 (karibu Sh. 3.7 bilioni). Fedha hizo zililipwa kupitia ankara Na. 069/09 kwa kile kilichoitwa kazi za usuluhishi kati ya TANESCO na IPTL.


Nayo Rex Attonery, imelipwa na TANESCO kiasi cha dola 47,552.25 kupitia ankara Na. 456/10 ya 28 Septemba 2010 kwa kazi za ushauri katika kesi Na. 15910 iliyofunguliwa na kampuni ya Richmond katika mahakama ya ICC dhidi ya TANESCO. Malipo mengine ya dola 472,000.00 yamefanyika 23 Juni 2010 kupitia ankara Na. 34/10 kwa ajili ya masuala ya usuluhishi katika kesi Na. 15910 kati ya TANESCO na Richmond. Dola 83,504.46 zililipwa tarehe 9 Aprili 2010 kama gharama za kukodishia chumba cha kusikilizia usulihushi kati ya TANESCO na Richmond kwa kesi hiyohiyo.
 
Jamani nani ataistop hii rot?Nani mwenye uchungu na Wananchi/walipa kodi wa Tanzania?

TANESCO haizalishi pesa,ni sisi wananchi tunaolipa kodi.Nani hapo Tanesco anaamua kuingia mikataba feki,halafu wanaojiita Wanasheria wa hapa bongo kushirikiana na Wanasheria wa nje(Hunton&William ya USA) na Reed Smith ya UK) kuikamua TANESCO mabillioni haya?

Ukiangalia hii axis of evil ,kuna Mkono(mbunge wa CCM),kuna Maajar wa REX Attorneys(our ambassador to USA),kuna Richmond ya Lowassa
na Dowans ya Rostam.

Hawa watu hawana shame kabisa !Wameamua kuiibia nchi waziwazi ,kwa kupata baraka toka serikali ya CCM.

Nchi yetu inastink sasa,tunahitaji mwokozi kuistop hii ROT.
 
Nchi hii inakamuliwa na tuliowaweka madarakani.
IPTL--Richmond--Dowans yote ni neema ya JK. Mkono-Tanesco, Mkono-IPTL, Mkono-BOT Mkono... Hivi hakuna wansheria wengine. I doubt kama JK hayumo among shareholders wa kampuni ya sheria ya Mkono.
 
Kwa mpango huu wengi wetu tulikosea sana kuchagua fani ya kusoma. Tulijikita kwenye kozi ngumu wakati zile laini ndizo zinazoingia pesa kilaini
 
Nchi hii inakamuliwa na tuliowaweka madarakani.
IPTL--Richmond--Dowans yote ni neema ya JK. Mkono-Tanesco, Mkono-IPTL, Mkono-BOT Mkono... Hivi hakuna wansheria wengine. I doubt kama JK hayumo among shareholders wa kampuni ya sheria ya Mkono.

Hawezi kuwa Partner kwenye taaluma ambayo hakusomea; punguza jazba inawezekana wala hausiki na hii mikataba kati ya Tanesco/BoT na wanasheria. Tatizo la kazi kama hizi hutegemea sana kesi inachukua muda gani kwani tozo hufanywa kulingana na muda halisi (effective time) wa mtu kwenye hiyo kesi na gharama za kusafiri
 
Vincent unazumguzia Tanzania,ambapo hakuna rule of law.
Kwa akili yako timamu hujui connection kati ya Maajar/JK???????

Je unaweza kuteuliwa kuwa balozi wa nchi fulani ,bila hata ya kuwa na credentials za Foreign affairs ?Ni bongo tu!
 
mwinyi_233.jpg


VIONGOZI walioingiza serikali katika mikataba mikubwa mitatu ya utata, wameliandalia taifa mzigo mkubwa wa madeni yasiyolipika hata katika miaka 50 ijayo, MwanaHALISI limeelezwa.

Wakati Dowans wanadai Sh. 94 bilioni, IPTL wanadai zaidi ya Sh. 248.6 bilioni kwa serikali/TANESCO kuvuruga mkataba wake. Mikataba yenye utata na inayotishia kuangamiza taifa ni ile ya kuzalisha umeme ya makampuni ya IPTL, Richmond na Dowans iliyosainiwa wakati wa utawala wa Rais Ali Hassani Mwinyi na rais Jakaya Kikwete.

Pamoja na makampuni hayo kukaba koo serikali na kuifikisha katika mahakama na tume mbalimbali za kimataifa za usuluhushi, gharama za serikali kujitetea zinaendelea kuongezeka. Katika kipindi cha miaka mitano tu iliyopita, serikali imetumia zaidi ya Sh. 23 bilioni kujitetea, kwa kulipa makampuni ya uwakili. Gharama hizi zinaongezeka mwaka hadi mwaka kufuatia kesi kuchukua muda mrefu na hata kufumuka kwa kesi mpya.

Sehemu ya mabilioni hayo ya shilingi imelipwa kwa makampuni ya wanasheria ya Mkono and Company Advocates ya Tanzania na Hunton and William ya Marekani kwa kutetea TANESCO iliyoshitakiwa na kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL). Mabilioni mengine yamelipwa kwa makampuni ya mawakili ya Rex Attorney ya Tanzania na Reed Smith ya Uingereza kwa kutetea TANESCO katika kesi iliyofunguliwa na kampuni ya Richmond Development Company (LLC).

Rex Attorneys na Reed Smith wamelipwa au watalipwa pia mabilioni ya shilingi kwa kutetea TANESCO katika shauri lililofunguliwa na makampuni ya Dowans Holdings S.A na Dowans Tanzania Limited (DTL) katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa kibiasha (ICC). Nyaraka zinaonyesha kuwa tayari Mkono and Company Advocates na Hunton and William wamelipwa na TANESCO kiasi cha dola 11,818,542.89 (sawa na karibu Sh. 17 bilioni). Kampuni ya Mkono and Company Advocates inamilikiwa na mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono.

Aidha, kampuni ya Mkono imelipwa pia kiasi cha Sh. 8.5 milioni kwa kusimamia shauri lililofunguliwa na benki ya Standard Chartered Bank ya Hong Kong dhidi ya serikali katika shauri la kukatisha mkataba wa IPTL. Serikali na IPTL waliingia mkataba mwaka 1994.

Nyaraka zinaonyesha kuwa Rex Attoney na mwenzake walilipwa kiasi cha dola 3,574,351.51 (karibu Sh. 5 .2 bilioni) katika shauri lililofunguliwa na makampuni ya Dowans Holdings S.A na Dowans Tanzania Limited (DTL) katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa kibiasha (ICC). Mawakili hao pia wamelipwa dola 860,056.71 (karibu sawa na shilingi 1.2 bilioni) kwa kazi ya kutetea TANESCO dhidi ya kesi iliyofunguliwa na kampuni ya Richmond Development Company (LLC) na kusikilizwa katika Falme za Kiarabu.

Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja mwezi mmoja baada ya mbunge wa Bumbuli (CCM), January Makamba kuibua kile kilichoitwa, "taarifa juu ya upatikanaji wa umeme nchini," ambapo tarehe 3 Februari 2011 alitaka waziri wa nishati na madini, William Ngeleja kueleza hatua zinazochukuliwa na TANESCO katika kukabiliana na mgawo wa umeme na mzigo wa kesi unaolikabili. Katika barua hiyo, Makamba anasema, "Katika viambatanisho vya hukumu ya ICC, kama ilivyosajiliwa mahakama kuu ya Tanzania zipo nyaraka zinazoonyesha kwamba mwanasheria aliyeishauri TANESCO kuvunja mkataba na Dowans – kwa kusema kwamba siyo mkataba halali na kwamba hakuna madhara ya kisheria kuuvunja – ndiye huyohuyo pia aliyeshauri benki ya Stanbink kutoa mkopo wa dola za 120 kwa Dowans – kwa kusema kwamba ni kampuni halali, inakopesheka na ina mkataba halali na TANESCO."

Anasema, "Ni mwanasheria huyohuyo aliyewakilisha TANESCO kwenye kesi iliyofunguliwa na Dowans, kesi ambayo ilitokana na ushauri wake, na baada ya hukumu ndiye huohuyo, kwa mujibu wa maelezo yako mheshimiwa waziri ya tarehe 6 Januari 2011, aliyetoa ushauri kwamba hakuna njia nyingine zaidi ya kuilipa Dowans."

Makamba alitaka serikali kueleza suala hilo kwa ufasaha ili kuondoa kile alichoita, "picha inayoweza kuonyesha serikali ilikosa umakini kwenye jambo hili zima na maadili hayakuzingatiwa." Alisema itakuwa vema taarifa ya serikali ikieleza ni wanasheria gani waliotumiwa na TANESCO kwa kila hatua katika shauri lake Dowans kwa kuanzia kwenye ushauri na kabla ya kuvunjwa kwa mkataba. Akijibu hoja za Makamba, Ngeleja anakiri kuwa benki ya Standard Chartered ya (Hong Kong) ambayo ni benki tanzu ya Standard Chartered ya Uingereza inayomiliki asilimia kubwa ya hisa za IPTL Tanzania Ltd., wameishitaki serikali kwa madai ya kutumia mitambo yake ya kuzalisha umeme kupitia Provisional Liquidator hivyo kukiuka Bilateral Investment Treaty (BIT) kati yake na serikali ya Uingereza. Kesi hizo ni Na. ARB /10/20 iliyofunguliwa na Standard Chartered Bank (Hong Kong) dhidi ya TANESCO, tarehe 1 Oktoba 2010 na kesi Na.ARB/10/12 iliyofunguliwa tarehe 11 Juni 2010.

Katika shauri hilo, IPTL wanataka mahakama "iamuru serikali kutoa tamko la kukiri kukiuka mkataba wa uwekezaji wa kimataifa – Bilateral Investment Treaty (BIT) na kulipa fidia ya dola 118.6 milioni, pamoja na kulipa gharama zote za uwekezaji - capacity charges – ambazo shirika hilo hazijazilipa tokea mwaka 2007 pamoja na fidia ya dola 130 milioni." Ngeleja anasema chimbuko la kesi hizo ni mgogoro wa awali kati ya Taneso na na IPTL ambao uliwasilishwa ICSID, Novemba mwaka 2007. Kesi zilizotajwa ziko katika hatua za awali na zinatarajiwa kuanza kusikilizwa Aprili mwaka huu.

Akijibu madai ya njia iliyotumika kupatikana kwa makampuni ya wanasheria, Ngeleja anasema "TANESCO iliona ni busara kuendelea kuwatumia mawakili walewale (Mkono and Company Advocates) kwa kuwa wana taarifa muhimu kuhusiana na kesi husika.

Anasema, "Kampuni ya Mkono ilianza kushughulikia shauri la IPTL tangu mwaka 2007 baada ya kupendekezwa na serikali kuwa washauri wa Kamati ya serikali ya ununuzi wa deni la IPTL. Kutokana na uelewa wa mawakili hao juu ya IPTL, ilionekana ni busara waendeshe kesi hiyo."

Kuhusu kampuni ya wanasheria ya Rex Attorney, Ngeleje anasema, ilipewa kazi ya ushauri baada ya ushindani uliohusisa kampuni tatu za FK Law Chambers, IMMA Advocates na Mkono. Anasema katika shauri la Dowans, TANESCO waliamua kuichukua tena Rex kwa ilikuwa na uzoefu na mkataba huo. Katika shauri hilo, mahakama ya ICC imeamuru TANESCO kulipa kiasi cha dola 94 milioni (Sh. 134 bilioni) kutokana na kushindwa katika kesi hiyo. Kwa mujibu wa uchunguzi wa MwanaHALISI, kampuni ya Mkono ililipwa na TANESCO – miezi miwili kabla ya uchaguzi, 19 Agosti 2010 kiasi cha dola 1,088,550.00 (karibu Sh.1.6 bilioni). Malipo hayo yalifanywa kupitia ankara Na. 124/10. Aidha, kabla ya Mkono kuchukua kitita hicho cha fedha, tarehe 15 Julai 2009, TANESCO walilipa mwanasheria huyo kiasi cha dola 2,177,100.00 (karibu Sh. 3.7 bilioni). Fedha hizo zililipwa kupitia ankara Na. 069/09 kwa kile kilichoitwa kazi za usuluhishi kati ya TANESCO na IPTL.

Nayo Rex Attonery, imelipwa na TANESCO kiasi cha dola 47,552.25 kupitia ankara Na. 456/10 ya 28 Septemba 2010 kwa kazi za ushauri katika kesi Na. 15910 iliyofunguliwa na kampuni ya Richmond katika mahakama ya ICC dhidi ya TANESCO. Malipo mengine ya dola 472,000.00 yamefanyika 23 Juni 2010 kupitia ankara Na. 34/10 kwa ajili ya masuala ya usuluhishi katika kesi Na. 15910 kati ya TANESCO na Richmond. Dola 83,504.46 zililipwa tarehe 9 Aprili 2010 kama gharama za kukodishia chumba cha kusikilizia usulihushi kati ya TANESCO na Richmond kwa kesi hiyohiyo.

Source: Mwanahalisi
 
inavyoonekana hapa viongozi walioingiza nchi hii kwenye matatizo ni waislamu tu, kwa kuwa nchi hii imeongozwa na marais wanne( wawili wakristo na wawili waislamu) na hawa waislamu ndio wenye kuleta haya matatizo basi inabidi tusiwachague tena waislamu uongozi hasa nafasi ya urais milele.
 
Vincent unazumguzia Tanzania,ambapo hakuna rule of law.
Kwa akili yako timamu hujui connection kati ya Maajar/JK???????

Je unaweza kuteuliwa kuwa balozi wa nchi fulani ,bila hata ya kuwa na credentials za Foreign affairs ?Ni bongo tu!

Kwani kuna "specific qualification" mtu anatakiwa awe nayo ili aitwe mwanasiasa?
 
Gazeti la Mawio la siku ya leo limebeba habari kubwa chini ya kichwa cha habari "Nimrodi Mkono kufilisi nchi".Katika habari hiyo gazeti hilo limeripoti kuwa gharama hizo za sh 18 bilioni ni kwa ajili ya kulipia gharam za huduma za ushauri na utetezi dhidi ya kampuni ya Independent Power Limited.Gharama hizo ni mpaka kufikia April 13 mwaka huu.

My take:
Hii nchi ina viongozi au matapeli?!
 
Hizo hela zinakwenda CCM!
Huyu bwana kuna kupindi alilipwa allipwa milioni. 500 na BoT eti kutetea!!!!!!!!!

Ni fisadi mkubwa hata kushinda Lowassa
 
yumo kwenye ile list of shame , alitishia kwenda mahakamani lakini mpaka leo hata serikali ya mitaa hakwenda ! Tuyatokomeze magamba kwa nguvu zote , SHAME ON YOU NIMROD MKONO !
 
Back
Top Bottom