FairPlayer
JF-Expert Member
- Feb 27, 2006
- 4,145
- 716
Na nyie mna wivu. Lol
Mkuu hapo nilipokolezea pamenifanya nitafakari sana. Unataka kusema pamoja na taaluma yake ya kisheria na kulipwa mabilioni yote hayo bado kashindwa kwenda mahakamani kujitetea kwa tuhuma alizopewa kwenye ile list of shame? Nashindwa kuamini kabisa juu ya hili!
Thanks 4 the info, unaeleweka vizuri tu mkuu - nakushauri kafundishe sheria vyuoni unaonekana ni mwalimu mzuri tu au chukua usajili wa uwakili binafsi kichwa chako kinachemka sana kifanyie kazi usilaze damu. Mimi ni mdau wa sayansi sio sheria, CHEERS.inategemea na hatua mliyopo, ila kama kuna room for appeal, basi wakili atakata rufaa, ila kama hakuna room for appeal, anaweza omba review au revision, ila kama mteja ameshindwa kesi kutokana na uzembe wa wakili, kuna venues nyingine kwa mteja kufanya ili apate haki yake kutokana na wakili mzembe, ila kushidwa pia ni sehemu ya law suits, ukienda mahakamani hakuna uhakika 100% wa kushinda kesi, ukishatoa fees ndio tayari umetoa, kwani wakili tayari alikuwakilisha wewe hata katika kushindwa kwako..nadhani nimekuelimisha kidogo kama bado au wewe ni mdau wa sheria unaweza nikosoa na kuja na yako
Symbion mbona hawajatajwa, kunani?
You are right Babu.Kuhusu Robert Mboma ni usanii mtupu wa nyani hacheki kundulu.
Sijui Meremeta na zile scandal za vifaa vya jeshi liiishia wapi.
Mpaka hapo tutakapopata list ya wanazo huko USWISWI,hatutajua mengi.Hawa magamba wanalinda,pesa za ufisadi zinazunguka tu,they have no mercy at all.
Jamani nani ataistop hii rot?Nani mwenye uchungu na Wananchi/walipa kodi wa Tanzania?
TANESCO haizalishi pesa,ni sisi wananchi tunaolipa kodi.Nani hapo Tanesco anaamua kuingia mikataba feki,halafu wanaojiita Wanasheria wa hapa bongo kushirikiana na Wanasheria wa nje(Hunton&William ya USA) ] ni wizi mtupu..
The game still on!
Wanamtandao wako mbioni tena kuingia Ikulu!
Kwa sasa wameanza kuvaa ngozi za kondoo huku wakitoa ahadi wakisema watawakimbiza watanzania kimaendeleo katika speed ya 120Km/h.
Hizi ni gharama za ujinga na upumbavu wetu!
Baada ya miaka mitano tutarudi tena hapa kupiga kelele bila maamuzi ya kulisaidia taifa!
Hii ndiyo Tanzania?
Wanamtandao wana akili sana...ndio maana wanaweza kutuibia...ukipingana nao hukawii kulala milele.
Wametulia ukawa, wanakikosi kazi ambacho kipo vizuri
Kuna watanzania wenzetu wamekaririshwa kwamba ccm yote ni mbovu. Kwamba magufuli ni mbovu pia kwasababu yuko ccm. Kwamba lowasa alikuwa fisad akiwa ccm lakin kwasababu yuko chadema ufisadi wake wote kwisha kabisa.
Wanachokifanya hao jamaa zetu ni kuimba kama kasuku hayo maneno. Kuongea mpaka na kutoa povu midomoni. Mpaka inakuwa aibu kusikiliza hoja zao.
Ni aibu kumsikia mtu na akili zake akisema mwizi wa miaka yote anakoma kuwa mwizi akiacha chama fulan kuhamia chama kingine
Ni aibu kumsikia mtu na akili zake akisema chama ndio huiba na sio watu wanaoiba. Yaani anasema ccm ndio inaiba na sio watu katka ccm kama lowasa wanaoiba. Sasa utashangaa. Chama kinaibaje?
Na mengine mengi
Watu wanajivua nguo hadharani kipind hiki.
Eeh Mungu saidia watu wako wanaokaribia kuteketea kwa kukosa maarifa
You are a fool who doesn't know that he is a fool.
Dah....sasa umejibu hoja gani? ...hapo ndio umeeneza sera za mabadiliko Lowasa....Lowasa Mabadiliko? ....
Kwa mpango huu wengi wetu tulikosea sana kuchagua fani ya kusoma. Tulijikita kwenye kozi ngumu wakati zile laini ndizo zinazoingia pesa kilaini