Askofu anamiliki HAMMER ya 250million!

Status
Not open for further replies.
wewe jamaa unaongea upuuzi mtupu, na umetumwa na shetani.angalia, watumishi wengine hao ukiwagusa, unakuwa unagusa mboni ya jicho la Mungu, unaweza ukajikuta unalaaniwa milele, imeandikwa "washindanao na Bwana watapondwa kabisa, Mungu akiwa upande wetu hakuna aliye juu yetu", hivyo ukianza kushindana na mtu wa Mungu, unashindana na Mungu mwenyewe na utapondwa kabisa hakika.

kama wana magari mazuri, waache, unajuaje kama Mungu ndo amewaambia wafanye hivo, ulitaka wavae kandambili zilizotoboka kama mashehe wenu? Mungu anasema mtenda kazi astahili posho lake, akifanyia kanisani, kuna share imewekwa kabisa itakayoenda moja kwa moja kwenye account yako. kama umekuwa na waumini wengi, ina maana share itakuwa kubwa, na unaweza kuitumia vyovyote upendavyo, kuhusu waumini, hakuna hata anayelalamika, huyo anayelalamika ni mnafiki mtumishi wa shetani na hajaokokoka na mwisho wake u karibu. WACHUNGAJI WENGINE wanapewa tu magari hayo. kuna mmoja ana makanisa Japan, yule wa Ubungo, gari alipewa na wajapani, makanisa ya kule yalimnunulia, kama ndo mnamsema yeye, kwasababu yeye ndo mwenye hio gari. ILE GARI ALIPEWA JAPAN, ana branch ya makanisa Korea, Japan na china, na anazungu dunia nzima kama beny hinn, watu wanaopona wanawapa magari na chochote anachotaka. fumba mdomo wako.

Unatetea ujinga hapa! Jesus' key messages on his entire life hapa duniani ilikuwa
Kuendesha hammer wakati kuna kondoo wanakufa njaa ni dhambi kubwa zaidi, Jesus said [FONT=Verdana, Helvetica, sans-serif]In Mark 10:25, "It is easier for a camel to go through the eye of a needle than for a rich man (bishop with hammer) to enter the kingdom of God."
[/FONT]
 
+ IMPORT DUTY (25%)+ EXCICE DUTY (10%) + VAT ( 18%)

About 55% Cummulative tax & Rate ya pesa ya Madafu ambayo ni 1330

Watu wangu wanaangamia kwa Kukosa Maarifa, Serikali Wezi, Viongozi wa Dini Wezi kila kitu WIZI MTUPU

Kwani hujui kuwa Makanisa ya msamaha wa kdoi. Pengine Mtumishi hajalipia hata ndururu ya ushuru!

Nadhani haya mambo ndo yalichangia Serikali kutaka kuondoa ushuru kwa Taasisi za Dini kwa madai kuwa baadhi ya Makanisa yanatumia nafasi hiyo vibaya.

Naamini TRA walimlipisha Mtumishi wa Mungu ushuru wote, maana katika hilo TRA wawe makini na kuangalia umuhimu wa bidhaa iliyoingizwa kwa Jamii au Kanisa badala ya kutoa tu ushuru
 
wewe jamaa unaongea upuuzi mtupu, na umetumwa na shetani.angalia, watumishi wengine hao ukiwagusa, unakuwa unagusa mboni ya jicho la Mungu, unaweza ukajikuta unalaaniwa milele, imeandikwa "washindanao na Bwana watapondwa kabisa, Mungu akiwa upande wetu hakuna aliye juu yetu", hivyo ukianza kushindana na mtu wa Mungu, unashindana na Mungu mwenyewe na utapondwa kabisa hakika.

kama wana magari mazuri, waache, unajuaje kama Mungu ndo amewaambia wafanye hivo, ulitaka wavae kandambili zilizotoboka kama mashehe wenu? Mungu anasema mtenda kazi astahili posho lake, akifanyia kanisani, kuna share imewekwa kabisa itakayoenda moja kwa moja kwenye account yako. kama umekuwa na waumini wengi, ina maana share itakuwa kubwa, na unaweza kuitumia vyovyote upendavyo, kuhusu waumini, hakuna hata anayelalamika, huyo anayelalamika ni mnafiki mtumishi wa shetani na hajaokokoka na mwisho wake u karibu. WACHUNGAJI WENGINE wanapewa tu magari hayo. kuna mmoja ana makanisa Japan, yule wa Ubungo, gari alipewa na wajapani, makanisa ya kule yalimnunulia, kama ndo mnamsema yeye, kwasababu yeye ndo mwenye hio gari. ILE GARI ALIPEWA JAPAN, ana branch ya makanisa Korea, Japan na china, na anazungu dunia nzima kama beny hinn, watu wanaopona wanawapa magari na chochote anachotaka. fumba mdomo wako.

Hee mbona kazi, kumbe ana branch ya makanisa mpaka japan, china na korea, hebu tujiulize jamani, vijiji vyetu vingapi vinahitaji kujengewa makanisa, barabara, shule, hospitali na kadhalika? Au hizo ni kazi za serikali tu? Wewe utaachaje kuhudumia kwanza wale wa nyumbani kwako wenye shida kupita kiasi uende kusaidia watu wenye uchumi mkubwa kama wa waasia kama sio unafuata maslahi? Na kama alipewa hiyo gari na wajapan, si angekuwa MTUMISHI BORA ZAIDI kama angewaambia ukweli kuwa, hii gari ni expensive mnaonaje tukinunua gari ya kawaida na kuwapa misaada watoto yatima wenye virusi vya ukimwi? Mnatapeliwa mkiwa macho kabisa...
 
naona tuje sasa kufika mahali hawa wahubiri wanaovuna wasikopanda wawe audited na kulipa kodi! kwani hiyo hela wanafanyia nini hata wasamehewe kodi? zipo tunazoona zinapata misaada tu hizo zisamehewe, but hawa wa kina Hummer etcmmmh ya kaisari muhimu na lazma!
 
Kazi kweli kweli viongozi wa dini!! Ukitaka kuwachambua baadhi yao, unaweza hata ugome kwenda kanisani. Ni kwa vile tu, tuna imani kuwa kuhudhuria kanisani na kushika neno la Mungu ni sehemu ya imani zeti na wala tusikwazike kwa matendo ya watumishi hao. Inasemwa "Usitizame matendo yao bali fuata neno la Mungu lisemavyo".

WoS, karibu sana and happy new year 2010. You disappeared for a while!!!! Ha ha. I always respect your contribution to this forum, so sincere!!


Kuwachambua Viongozi wa kisiasa wanaopata utajiri kwa njia za haramu ni halali, lakini kuwachambua Viongozi wa kanisa wanaotajirika kupitia michango ya waumini wao ambao wengi ni walalahoi ni haramu!...Kweli wajinga ndiyo waliwao!
 
wewe jamaa unaongea upuuzi mtupu, na umetumwa na shetani.angalia, watumishi wengine hao ukiwagusa, unakuwa unagusa mboni ya jicho la Mungu, unaweza ukajikuta unalaaniwa milele, imeandikwa "washindanao na Bwana watapondwa kabisa, Mungu akiwa upande wetu hakuna aliye juu yetu", hivyo ukianza kushindana na mtu wa Mungu, unashindana na Mungu mwenyewe na utapondwa kabisa hakika.

kama wana magari mazuri, waache, unajuaje kama Mungu ndo amewaambia wafanye hivo, ulitaka wavae kandambili zilizotoboka kama mashehe wenu? Mungu anasema mtenda kazi astahili posho lake, akifanyia kanisani, kuna share imewekwa kabisa itakayoenda moja kwa moja kwenye account yako. kama umekuwa na waumini wengi, ina maana share itakuwa kubwa, na unaweza kuitumia vyovyote upendavyo, kuhusu waumini, hakuna hata anayelalamika, huyo anayelalamika ni mnafiki mtumishi wa shetani na hajaokokoka na mwisho wake u karibu. WACHUNGAJI WENGINE wanapewa tu magari hayo. kuna mmoja ana makanisa Japan, yule wa Ubungo, gari alipewa na wajapani, makanisa ya kule yalimnunulia, kama ndo mnamsema yeye, kwasababu yeye ndo mwenye hio gari. ILE GARI ALIPEWA JAPAN, ana branch ya makanisa Korea, Japan na china, na anazungu dunia nzima kama beny hinn, watu wanaopona wanawapa magari na chochote anachotaka. fumba mdomo wako.

kwakweli wewe umedanganywa umeiva kabisaa hakuna wa kukupindua, ila jua na elewa wote huo ni ulafi,ubinafsi etc, why haendi kuweka kanisa kule ukerewe wanahitaji sana injili, why DAR? sababu kuna pesa etii?ahaa kumbe wazo ni kuhubiri penye pesa na si penye kiu ya neno la Mungu! Ole wenu!
 
kwakweli wewe umedanganywa umeiva kabisaa hakuna wa kukupindua, ila jua na elewa wote huo ni ulafi,ubinafsi etc, why haendi kuweka kanisa kule ukerewe wanahitaji sana injili, why DAR? sababu kuna pesa etii?ahaa kumbe wazo ni kuhubiri penye pesa na si penye kiu ya neno la Mungu! Ole wenu!

Spot on......hawa 'watumishi' wana ubinafsi pia.Mtu anaku offer HUMMER unakubali si ungemsahuri akupe AMBULANCE kama tatu badala yake ili usaidie jamii?TATIZO na wao wanataka kutanua na kuwaiga wale Wanaijeria wa TV....
 
Spot on......hawa 'watumishi' wana ubinafsi pia.Mtu anaku offer HUMMER unakubali si ungemsahuri akupe AMBULANCE kama tatu badala yake ili usaidie jamii?TATIZO na wao wanataka kutanua na kuwaiga wale Wanaijeria wa TV....

absolutely right!
 
Au angejenga DISPENSARY for that 250m na kuacha legacy ya milele...baada ya 5 years nani atalikumbuka hilo HUMMER lake?...lakini angalia ile SELIAN(???) HOSPITAL kule Umbulu kama sikosei au PERAMIHO MISSION HOSPITAL ndizo legacy zenyewe...for the time being I will remain with my MAINSTREAM CHURCH hata kama hawajui kuhubiri,lakini wana legacies na biblia ni ile ile haijabadilika
 
Ni kweli hata mie nimekutana nao na bado ninakutana nao wengi tu, ila sio sababu ya kuwaita wooote wezi, pili kumbuka wao pia ni binadamu, wengi wao kama kina Petro hawana maarifa sana ya kidunia kwa hiyo usichoke kuwaambia kwa upole kama wao wanavyokuhubiria injili kuwa hapa kwa uelewa wako mtumishi unakosea. mie ni rafiki mzuri tu wa hawa watu, kwa kweli wala sio haambiliki kama wengi wanavyotaka kuwaonyesha isipokuwa ni kukosa exposure tu mara nyingine na wako tayari kujifunza,


Kuna makanisa mengine siku hizi unakwenda kanisani unaishia kujutia usingizi wako tu uliouacha asubuhi. Yaani wanahubiri kuhusu utoaji! Nasikia kuna baadhi ya makanisa sasa hivi watu wanalazimishwa kupelea ''salary slips'' kama uthibitisho kwamba pesa ulizotoa ni sawa na 10% (fungu la kumi). Je hii imekaaje?

Nairobi kuna makasa mengi mpaka Halmashauri ya Jiji ilikuwa inafikiria kusitisha zoezi la kusajili makanisa. Naona hili wimbi sasa limeingia Tanzania.

Kwa mtazamo wangu, ni dhambi kutumia Injili kujipatia kipato kisichokuwa halali na kujilimbikizia mali.
 
Kuna makanisa mengine siku hizi unakwenda kanisani unaishia kujutia usingizi wako tu uliouacha asubuhi. Yaani wanahubiri kuhusu utoaji! Nasikia kuna baadhi ya makanisa sasa hivi watu wanalazimishwa kupelea ''salary slips'' kama uthibitisho kwamba pesa ulizotoa ni sawa na 10% (fungu la kumi). Je hii imekaaje?

Nairobi kuna makasa mengi mpaka Halmashauri ya Jiji ilikuwa inafikiria kusitisha zoezi la kusajili makanisa. Naona hili wimbi sasa limeingia Tanzania.

Kwa mtazamo wangu, ni dhambi kutumia Injili kujipatia kipato kisichokuwa halali na kujilimbikizia mali.

Ufisadi uliokithiri umejaa ndani ya makanisa mengi mnaufumbia macho na kuogopa kuushikia mabango. Unyama wa hali ya juu unaofanywa na mapadri walio wengi kuwalawiti watoto wadogo wa kike na wa kiume na kutembea na wake za watu nao umekithiri lakini mnaogopa na kufumba macho dhidi ya unyama huo. Ni unafiki wa hali ya juu kujifanya kupigia kelele viongozi mafisadi na watu wa uraiani ambao wanalawiti watoto wadogo wa kike na wa kiume wakati huo huo mnaufumbia macho ufisadi na unyama uliokithiri unaotendwa na viongozi walio wengi ndani ya makanisa. Matumizi ya kifisadi yanayofanywa na mapadri kutokana na michango ya walalahoi. Mahesabu yao hayana ukaguzi wowote miaka nenda miaka rudi nab ado mnatetea michango ya mabilioni ya shilingi huku wao wakiishi maisha ya kifahari ya hali ya juu na waumini wakiwa hoi bin taabani. Fumbueni macho muyaone madhambi na unyama unaofanywa na viongozi wa makanisa na muanze kuwahoji msiwaone watakatifu sana kumbe hawana utakatifu wowote na wao wanatenda dhambi kama binadamu wengine wowote wale. Mapato ya kanisa nayo yaanze kukaguliwa ili kuhakikisha hakuna matumizi ya kifisadi yanayowaneemesha viongozi wa makanisa hayo.
 
Sasa nyie mnataka afanyeje wakati mnapeleka sadaka unaccounted for an audited huku serikali inampa tax examption? Siku hizi building or starting a church is lik starting a company or an ngo.
Kama hakutakuwa na watu wanayafanyia audit mahesabu ya haya makanisa people should expect more than hammers
 
Ufisadi uliokithiri umejaa ndani ya makanisa mengi mnaufumbia macho na kuogopa kuushikia mabango. Unyama wa hali ya juu unaofanywa na mapadri walio wengi kuwalawiti watoto wadogo wa kike na wa kiume na kutembea na wake za watu nao umekithiri lakini mnaogopa na kufumba macho dhidi ya unyama huo. Ni unafiki wa hali ya juu kujifanya kupigia kelele viongozi mafisadi na watu wa uraiani ambao wanalawiti watoto wadogo wa kike na wa kiume wakati huo huo mnaufumbia macho ufisadi na unyama uliokithiri unaotendwa na viongozi walio wengi ndani ya makanisa. Matumizi ya kifisadi yanayofanywa na mapadri kutokana na michango ya walalahoi. Mahesabu yao hayana ukaguzi wowote miaka nenda miaka rudi nab ado mnatetea michango ya mabilioni ya shilingi huku wao wakiishi maisha ya kifahari ya hali ya juu na waumini wakiwa hoi bin taabani. Fumbueni macho muyaone madhambi na unyama unaofanywa na viongozi wa makanisa na muanze kuwahoji msiwaone watakatifu sana kumbe hawana utakatifu wowote na wao wanatenda dhambi kama binadamu wengine wowote wale. Mapato ya kanisa nayo yaanze kukaguliwa ili kuhakikisha hakuna matumizi ya kifisadi yanayowaneemesha viongozi wa makanisa hayo.

hatari kubwa sana, wanakondoo sasa watashtuka
 
Askofu hawa hufanyia brain damage waumini wala hawashtuki na mafungu ya 10 teh teh teh teh
 
Ni Rahisi kwa Ngamia kupita katika Tundu la Sindano kuliko Tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu! Kama mali zako haziwezi kuwapatia Nafuu Wahitaji basi wewe ni bure na hufai mbele za Mungu! Kama Mali zako zinashindwa kuwaeletea watu huduma muhimu kama afya na hospital then Utajiri haumpendezi Mungu!

Watu siku hizi hawatafakari neno la Mungu na Badala yake wanaendesha na Hisia zaidi

Mungu Okoa Taifa lako
 
. ILE GARI ALIPEWA JAPAN, ana branch ya makanisa Korea, Japan na china, na anazungu dunia nzima kama beny hinn, watu wanaopona wanawapa magari na chochote anachotaka. fumba mdomo wako.


nadhani hatuna ugomvi na mtumishi kupewa hummer au hata akipewa helicopter....lakini mbona theories kutoka huko kanisani zinakuja nyingi?? maana kuna aliyekuja hapa kutuambia kuwa ooh ile hummer ni dola 30,000 tu ....sio dola laki 200,000 ,,,,...sasa na wewe unasema alipewa bure...?? tushike lipi??

nadhani kuondoa ubishi ni bora waandishi wa habari waombe appointment na mtumishi mwenyewe kujua ukweli...wamuulize ..kuwa watanzania wanadhani dhamani ya gari lake ni kubwa mno...na angeweza kujenga jengo la kuduma la kanisa lake lililojengwa kwa mabanzi au kusaidia jamii....kwani Yesu tunayemuhubiri alizaliwa kwenye karo la ngombe baba yake na mama yake hawakuweza kulipa gharama ya nyumba ya wageni....tunamuishije kati ya wimbi la umaskini????

na hata basi tukipewa michango si tuchague ...mtu akikupa fuel guzler ..kwa kuwa kwao kuna global warming campagne ...si akupe na dola 200 ya kulihudimia kila siku???? unaweza kupewa gari lakini kila mwaka ukapoteza hadi milioni 50 kulihudumia service na mafuta ......
 
...kabla ya kununua hama ...angejenga kwanza lile banda analoita kanisa ambalo kila siku linahatarisha maisha ya watu wanaoweza kuangukiwa nalo,KUENEZA INJILI SEHEMU HADI ZILE DUNI..[sio mnakazania kueneza injili kwa wenye kipato tu]...,alafu akajenga shule ,hospitali ,kusaidia yatima na wahitaji ...kama neno la mungu linavosema...nilikuwa na njaa ukanilisha ,na kiu....pesa zikibaki ndio anunue HAMMER.....

Umesahau angejenga hata shule kule vijijini ili kuwasaidi kondoo wa kesho. Haijakatazwa kuwa tajiri, but tuangalie hata mitume wote hawakua matajiri kiasi hicho. Wewe utawaongozaje watu walio masikini kwa kiasi hicho na ww unamiliki mahekalu halafu unaona sawa? Halafu unaanza kusema SIRIKALI haiwapendi wananchi. Daaa, hawa jamaa watatumliza, manake asienacho hunyanganywa hata kidogo alicho nacho, MTANZANIA masikini anakamuliwa kodi na serikali halafu mchungaji nae anamkamua za kumchunga. Pepo kazi. Kunawatu wangeweza miliki hayo madude lakini wanaona aibu kuwa nayo kwenye jamii ambayo kunawatu hawana uhakika wakula na kulala. Watoto wa mitaani hawajui watalala wapi, inauma kweli kwelikweli, Tanzania kunawatu hawana pa kulala!!!! wanalala kwenye mitaro usiku na kuanza kuomba asubuhi, halafu sisi tunaona it is ok Mchungaji kumiliki hayo mdude? Basi hamna haja ya kuwaonyeshea vidole MAFISADI manake na wao wanahaki ya kumiliki walivyo navyoooooo!!!!!, Inatia uchungu but Very complex to solve it due to the fact that Watanzania tumeshajengeka kwenye falsafa ya ubinafsi na urohooo, na uongooo.!!!!!!!!
 
Umesahau angejenga hata shule kule vijijini ili kuwasaidi kondoo wa kesho. Haijakatazwa kuwa tajiri, but tuangalie hata mitume wote hawakua matajiri kiasi hicho. Wewe utawaongozaje watu walio masikini kwa kiasi hicho na ww unamiliki mahekalu halafu unaona sawa? Halafu unaanza kusema SIRIKALI haiwapendi wananchi. Daaa, hawa jamaa watatumliza, manake asienacho hunyanganywa hata kidogo alicho nacho, MTANZANIA masikini anakamuliwa kodi na serikali halafu mchungaji nae anamkamua za kumchunga. Pepo kazi. Kunawatu wangeweza miliki hayo madude lakini wanaona aibu kuwa nayo kwenye jamii ambayo kunawatu hawana uhakika wakula na kulala. Watoto wa mitaani hawajui watalala wapi, inauma kweli kwelikweli, Tanzania kunawatu hawana pa kulala!!!! wanalala kwenye mitaro usiku na kuanza kuomba asubuhi, halafu sisi tunaona it is ok Mchungaji kumiliki hayo mdude? Basi hamna haja ya kuwaonyeshea vidole MAFISADI manake na wao wanahaki ya kumiliki walivyo navyoooooo!!!!!, Inatia uchungu but Very complex to solve it due to the fact that Watanzania tumeshajengeka kwenye falsafa ya ubinafsi na urohooo, na uongooo.!!!!!!!!


Hebu fikiria kama waumini wangekuwa na SACCOS zao na kujichangia hayo mabilioni katika SACCOS zao na hatimaye kuweza kukopa na ili kufanyia shughuli za maendeleo yao na familia zaobadala ya kuendelea kuwachangia Viongozi wa makanisa ambao wanaishi maisha ya hali ya juu kupitia migongo ya walalahoi. Waumini mshtuke sasa na kuanza kuwahoji hawa viongozi wa makanisa badala ya kuendelea kuwachangia maisha yao ya kifahari huku nyinyi wenyewe mkiwa hoi kutokana na ugumu wa maisha.
 
Watu bwana mazungu wa unga wakiendesha hammer maneno mafisadi maneno acha watumishi watanue tena wamechelewa
 
Mwacheni mchungaji wa watu,ila nashauri pia haya makanisa ya kiroho yatoe huduma za jamii kama elimu na afya kama katoliki na lutheran.

Maana mbinguni kweli tunaenda lakini elimu na afya hapa duniani ni muhimu kabla hatujafika kwa baba muumba.

Mponjoli si kweli kwamba makanisa ya kiroho huwa hayatoi huduma za kijamii kama inavyotaka kuaminishwa na wengi.
Haya madhehebu yanatoa huduma za kijamii kama ulivyoshauri. fuatilia mwenyewe.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom