Asilimia 60 ya maafa ya mafuriko Dar es Salaam yanatokana na uzembe wa serikali, Raisi Samia akubali ukweli huu

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Ni kweli maafa ya mafuriko yanaitwa natural disasters, lakini sio lazima natural disasters zilete maafa kwa raia na mali zao.

Asilimia 60 ya maafa ya mafuriko Dar es Salaam yanatokana na uzembe, ubinafsi, kutojali, na uongozi mbovu kwa ujumla wa viongozi wa serikali. Si mara ya kwanza Dar es Salaam inapata mafuriko. Ni zaidi ya miaka 20 tunaishi kwa kudhani kwamba tatizo la mafuriko Dar dawa yake ni kumwomba Mungu atuepushe na vifo na upotevu wa mali, kutia ndani uharibifu wa miundombinu.

Mji wowote ulio pembezoni mwa bahari kuwa na tatizo la mafuriko yanayotokana na mvua kwa zaidi ya miaka 20 hakuna kingine zaidi ya uzembe. Serikali yetu imejisahau mno, hasa wakijua Watanzania sio rahisi kuiondoa serikali iliyopo madarakani kwa kuwa tu inafanya uzembe, ufisadi, ubinafsi nk. Kwa hiyo wanajisahau sana.

Tatizo la mafuriko linahitaji suluhisho ambalo gharama yake huenda hata isifikie gharama ya kununua ndege mbili za dreamliner, au pesa tunayolipa makampuni yanayotushitaki kukiuka mikataba.
  1. Wakusanye wataalamu wa physical geography watengeneze topographical na contour maps za Dar es Salaam na ukanda wa pwani, wakionyesha ilikupata elevation na terrain ya ukanda wote wa Dar na contour lines zinavyokwenda
  2. Kwa kutumia topographical map na contour lines, wakusanye civil engineers wachore line kupitisha maji kwa kutumia channel za ukubwa wa kiasi na kupeleka kwenye channel kubwa ambazo zitaelekeza maji baharini
Sasa, katika kufanya design ya channel za maji, factor of safety isiwe tena historical data, bali iwe projection iliyo informed na modeling za climate change impact scenarios katika masuala ya mvua, na ipigwe factor kubwa zaidi ya standard factors (najua mainjinia tu ndio wataelewa hii paragraph)

Ikibidi, baadhi ya majengo itabidi yaondoke, yabomolewe, hata kama ni mazuri kiasi gani.
1705833748220.png

Ninatamani sana nimpigie Samia simu nimwambia nipe hii kazi nisimamie huu mkakati. Raisi Samia nakuhakikishia kwamba mji wowote uliopo kando ya bahari haupaswi kuwa na mafuriko kama tunayoona Dar. Au mwambie Prof. Tibaijuka asimamie hili.

Tatizo lililop kwako Samia ni kuteua watu ambao wanaona kipao mbele cha Dar ni kushughulika na changudoa na maandamano ya Chadema badala ya matatizo yanayoathiri wananchi na taifa kwa ujumla kwa kiwango cha juu sana. Unapewa sifa kila siku katika mambo ambayo ni routine sana, usiridhike au kudanganywa na hizo sifa. Kutoa hela za kujenga Zahanati na nini sijui sio sifa za kuwa raisi mzuri. Kwanza wengine tunaona hilo ni uongozi mbovu tu, kwa sababau pesa hizo zinapaswa kutolewa kupitia mipango ya maendeleo na bajeti za maeneo hayo. Kwa nini unakubali kuleweshwa na sifa za mambo yanayotakiwa kufanywa na wakuu wa mikoa na wakurgenzi wa miji na majiji? Fanya kazi za kitaifa tukusifie, sio mambo ya vijijini, wilayani na mikoani. Hiyo sio ligi yako.

Bado hatuoni unayofanya katika mambo makubwa ambayo yataacha legacy yako, pamoja na hili la mafuriko Dar. Japo tunaelewa ni suala la majiji haya matatu, Ilala, Kindondoni na Temeke, lakini lichukue sura ya kitaifa ili kuwe na coordination rahisi.
 
Ni kweli maafa ya mafuriko yanaitwa natural disasters, lakini sio lazima natural disasters zilete maafa kwa raia na mali zao.

Asilimia 60 ya maafa ya mafuriko Dar es Salaam yanatokana na uzembe, ubinafsi, kutojali, na uongozi mbovu kwa ujumla wa viongozi wa serikali. Si mara ya kwanza Dar es Salaam inapata mafuriko. Ni zaidi ya miaka 20 tunaishi kwa kudhani kwamba tatizo la mafuriko Dar dawa yake ni kumwomba Mungu atuepushe na vifo na upotevu wa mali, kutia ndani uharibifu wa miundombinu.

Mji wowote ulio pembezoni mwa bahari kuwa na tatizo la mafuriko yanayotokana na mvua kwa zaidi ya miaka 20 hakuna kingine zaidi ya uzembe. Serikali yetu imejisahau mno, hasa wakijua Watanzania sio rahisi kuiondoa serikali iliyopo madarakani kwa kuwa tu inafanya uzembe, ufisadi, ubinafsi nk. Kwa hiyo wanajisahau sana.

Tatizo la mafuriko linahitaji sulugisho ambalo gharama yake huenda hata isifikie gharama ya kununua ndege mbili za dreamliner, au pesa tunayolipa makampuni yanayotushitaki kukiuka mikataba.
  1. Wakusanye wataalamu wa physical geography watengeneze topographical na contour maps za Dar es Salaam na ukanda wa pwani, wakionyesha ilikupata elevation na terrain ya ukanda wote wa Dar na contour lines zinavyokwenda
  2. Kwa kutumia topographical map na contuoar lines, wakusanye civil engineers wachore line kupitisha maji kwa kutumia channel za ukubwa wa kiasi na kupeleka kwenye channel kubwa ambazo zitaelekeza maji baharini
Sasa, katika kufanya design ya channel za maji, factor of safety isiwe tena historika data, bali iwe projection iliyo informed na modeling za climate change impacts katika masuala ya mvua, na ipigwe factor kubwa zaidi ya standard factors (najua mainjinia tu ndio wataelewa hii paragraph)

Ikibidi, baadhi ya majengo itabidi yaondoke, yabomolewe, hata kama ni mazuri kiasi gani.
View attachment 2878486
Ninatamani sana nimpigie Samia simu nimwambia nipe hii kazi nisimamie huu mkakati. Raisi Samia nakuhakikishia kwamba mji wowote uliopo kando ya bahari haupaswi kuwa na mafuriko kama tunayoona Dar. Au mwambie Prof. Tibaijuka asimamie hili.

Tatizo lililop kwako Samia ni kuteua watu ambao wanaona kipao mbele cha Dar ni kushughulika na changudoa na maandamano ya Chadema badala ya matatizo yanayoathiri wananchi na taifa kwa ujumla kwa kiwango cha juu sana. Unapewa sifa kila siku katika mambo ambayo ni routine sana, usiridhike au kudanganywa na hizo sifa. Kutoa hela za kujenga Zahanati na nini sijui sio sifa za kuwa raisi mzuri. Kwanza wengine tunaona hilo ni uongozi mbovu tu, kwa sababau pesa hizo zinapaswa kutolewa kupitia mipango ya maendeleo na bajeti za maeneo hayo. Kwa nini unakubali kuleweshwa na sifa za mambo yanayotakiwa kufanywa na wakuu wa mikoa na wakurgenzi wa miji na majiji? Fanya kazi za kitaifa tukusifie, sio mambo ya vijijini, wilayani na mikoani. Hiyo sio ligi yako.

Bado hatuoni unayofanya katika mambo makubwa ambayo yataacha legacy yako, pamoja na hili la mafuriko Dar. Japo tunaelewa ni suala la majiji haya matatu, Ilala, Kindondoni na Temeke, lakini lichukue sura ya kitaifa ili kuwe na coordination rahisi.
Samia ndio aliwapa viwanja mkajenga huko mabondeni?
 
Sometimes hii nch tunalaumu mno serikali,
Watu wanajenga kwenye mikondo ya maji, wengine hadi wanatoa rushwa ili wajenge, then yakija mafuriko wanakimbilia kusema serikali, hahah
Wanapojenga serikali inakuwa wapi, imelala? Na utakuta wengi wana vibali vya serikali. Ndio maana tunasema bottom-line yote haya ni uzembe wa serikali, japo kuna 20% ya lawama kwa hao watu, na 20% kwa natural disasters
 
Samia ndio aliwapa viwanja mkajenga huko mabondeni?
Serikali yake au ya watangulizi wake ndio waliacha watu wajenge, au hata walitoa hivyo vibali vya kujenga. Kwa hiyo tumlaumu nani sasa?

Au kwa lojiki zako za chekechea, watu wanapomlilia Samia atoe msaada wa fedha za wodi ya wazazi, yeye ndio anakuwa kawapa mimba na kawazalisha?
 
Machapisho kama adhimu hupata wachangiaji wachache kuliko ya Uchumba wa Manara.
Mkuu, hiyo inatosha kukuambia siku hizi wanachama wengi wa JF ni watu wa aina gani na wana uwezo wa kiasi gani kujadili machapisho yaliyo mazito. Wataishia kutukana tu kwa sababu wameona neno ambalo halimsifii Raisi Samia. Ndio maana watu wengi siku hizi wanaachana na JF.

Angalia pia statement ya signature yangu. Hili nililiona siku nyingi sana, na hata nilishaandika thread kuhusu nani anapiga kura kwenye chaguzi za Tanzania
 
Watu wameshatahadharishwa na mamlaka ya hali ya hewa wahame hawataki, kuna nabii akawaambia wahame wakasusa, sasa tuwasaidieje?.

Mtu unaona kabisa huu ni mkondo wa maji, unalazimisha kujenga, unataka nani apate uchungu wa uhai wako zaidi yako mwenyewe?.

Siipendi sisiemu na watu wake, lakini ktk hili la mafuriko niko na Samia.

Nyie kila mwaka maafa yanawakumba lakini hamkomi, hivi aliyewaambia maisha yanapatikana huko mitaroni ni nani?.

Huku bara ardhi imejaa tele, njooni huku.

Mvua ni baraka, acha iendelee kunyesha maana ni msimu wake.
 
Sio kila kitu unalaumu serikali kijana maeneo yote yenye changamoto ya mafuriko wananchi waliambiwa wahame kwa hiari ila hawakufanya hvyo na wengine walipewa maeneo wameuza wamerudi tena mabondeni serikali inahusikaje na wananchi sikio la kufa kiufupi watanzania hatuamini kitu mpaka kitokee hata kule hanang eneo liliathiriwa walishapewa maeneo mengine wakauza wakarudi tena karibu na milima sasa unataka serikali iwachape viboko mkibolewa mnataka fidia nani atabeba huo mzigo ni kweli serikali ina changamoto zake lakini kuna vitu vingine wananchi wanajitakia.
 
Serikali yake au ya watangulizi wake ndio waliacha watu wajenge, au hata walitoa hivyo vibali vya kujenga. Kwa hiyo tumlaumu nani sasa?

Au kwa lojiki zako za chekechea, watu wanapomlilia Samia atoe msaada wa fedha za wodi ya wazazi, yeye ndio anakuwa kawapa mimba na kawazalisha?
Alaumiwe aliyejipeleka machinjioni wakati sehemu salama zipo nyingi hapa Tanzania.

Hao waliotoa vibali wana makosa yao lakini mwenye kosa zaidi ni yule aliyetoa rushwa ili apate kibali cha kujenga kwenye njia za maji.
 
Sio kila kitu unalaumu serikali kijana maeneo yote yenye changamoto ya mafuriko wananchi waliambiwa wahame kwa hiari ila hawakufanya hvyo na wengine walipewa maeneo wameuza wamerudi tena mabondeni serikali inahusikaje na wananchi sikio la kufa kiufupi watanzania hatuamini kitu mpaka kitokee hata kule hanang eneo liliathiriwa walishapewa maeneo mengine wakauza wakarudi tena karibu na milima sasa unataka serikali iwachape viboko mkibolewa mnataka fidia nani atabeba huo mzigo ni kweli serikali ina changamoto zake lakini kuna vitu vingine wananchi wanajitakia.
Unajua, watu kutohama mambondeni kwa kutii agizo la serikali ni uzembe pia wa serikali. Mbona Ngorongoro wamehama?
 
Alaumiwe aliyejipeleka machinjioni wakati sehemu salama zipo nyingi hapa Tanzania.

Hao waliotoa vibali wana makosa yao lakini mwenye kosa zaidi ni yule aliyetoa rushwa ili apate kibali cha kujenga kwenye njia za maji.
Hizo ni semantics. Kutoa rushwa kwa daktari ili akutibu wa kulaumiwa ni wewe, sivyo? Na trafiki kuomba rushwa wa kulaumiwa ni wewe? Na tuoa rushwa polisi wamfutie mashataka mtuhumiwa wa kulaumiwa ni mtoa rushwa? Hebu jaribu kujifanya una uwezo wa kuchambua mambo angalau kidogo
 
Back
Top Bottom