Filipo
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 9,342
- 5,536
Kwa mtazamo wangu, hilo ni pigo kubwa kwa cdm. Mkoa wa Mara ni ngome nyingine ya cdm na yeye kama ndiye alikuwa mwenyekiti, basi alifanya kazi nzuri. Kwahiyo kuondoka kwa staili hii itasumbua kidogo. Cdm wanatakiwa wajipange upya na kumaintain heshima yao huko. Kuhusu kurudi ccm kwa huyo jamaa na hao vijana, mimi sishangai sana. Ccm inawapa watu hela kurudisha kadi ili mikutano i shine! Hali ya nchi ni mbaya, watu hawana uhakika na mlo wa siku, kwahiyo akilipwa akarudishe kadi haoni tabu. Ila rohoni anajua kabisa ccm hakuna tumaini. Poleni sana wanachadema maana ndio walengwa wakubwa wa mpango mzima wa ccm.