Alifanya kazi saiti kwa pesa yake, sasa simu haipokelewi na bosi haonekani

Zitamfikia taarifa kama ulivyo shaur.,
Ila jamaa ajavurunda kapiga kaz vzur sana tena ontime sema yule mkuru wetu anaroho ya korosho anatuminya had watumish af ashauliki et....

Kuna. Fund mwengine kakalishwa pia na ni mtu wa makamo....sasa akija kidai pale kazn kaweka mikon nyuma had unaona huruma.
Nyie wanakamati inatakiwa jamaa awaroge wote muwe machizi, hivi mnawezaje kumlazimisha mtu afanye kazi bila mkataba wowote?? Mimi majuzi fundi wa welding tulipatana anitengenezee geti kwa sh laki saba tuu lakini tuliandikishiana mkataba, kwenye pesa sitaki kuamini watu hovyo hovyo aiseeee. Ila huyo bosi akiendelea kukaza mwambie aje pm nimpe mbinu chaap ya kumtoa shipa huyo bosi.
 
Umeniwahi,,,, na mm nlikuwa nashauri hivi hivi.
Kuna jamaa huko mikoa ya magharibi alipewa tenda kubadilisha madirisha kwenye kituo cha afya na kuweka ya aluminum, akafanya kazi yake vizuri sana na akamaliza. Sasa kulipwa ikawa issue, jamaa alivyoona usumbufu umezidi akaenda kung'oa madirisha yote ya aluminum aliyoweka. Aisee jamaa wakamfanyia figisu wakamkamata na kumbambikia makosa na akawekwa ndani. Haya mambo yana uonevu mkubwa sana sometimes.
 
Habarini wanajamvi.

Leo nakuja na kisa hiki cha ukweli ambacho mdau anakipitia anaomba ushauri.

Nina jamaa yangu ni mtu fresh sana hanaga makuu kabisa na mtu kwa navyomfahamu mimi.
Sasa juzi kaniita home kwake ananieleza kwa uchungu huku chozi likiwa limejaa kwenye macho nusra kutoka tu nahisi alijikaza kwakuwa ni mwanaume ile situation iliniumiza nikahisi maumivu sana.

Kisa kipo hivi sasa jamaa anafanya kazi kwenye taasisi moja hvi(****) sasa kwenye hiyo taasisi yao ilitokea wakapata pesa ambazo ziliwalenga kufanya maintenance ya eneo lao la kazi na kuboresha mazingira basi bana wakatafuta mkandarasi wa kufanya hiyo kazi kama watatu hivi wakashindwana kwasababu ya huyo boss wa taasisi kusema bei ni kubwa kwavile mwamba ni mpambanaji akajitosa kuomba tenda akiwa na uwezo ataimudu, akiweka nguvu kazi basi bana deal done mwamba akapewa tenda japo boss wake hakuonesha kusapot kivile japo wanakamati wa ujenzi wali sapoti kwa haki jamaa apewe tenda chap kwa haraka wakamuomba aanze kazi huku wakiandaa mikataba n.k ambayo itahusiana na malipo.

Mwamba akasema yeye hawezi kuanza kazi bila kupata mkataba unasemaje na kuhusu malipo lakini kwavile ule mradi kila mwanakamati alihitaji uende kwa kasi wakamuomba sana mwamba aanze kazi kwa haraka asijali juu ya malipo.

Basi mwamba akawambia yeye ataanza kazi ila anaomba malipo yake yawe kwa awamu mbili, awamu ya kutengeneza foundation na alipwe then awamu ya kumaliza na alipwe basi mwamba akaanza kaz bila kuchelewa akaita mafundi sait wakaanza kazi kwa pesa yake akapiga kazi, akamaliza awamu ya kwanza malipo yakaanza kusua sua mara wamwambie malipo yamekwama bank huku na kule mara boss wake huyo anamwambia mpaka mkandarasi aje kukagua, yeye hawezi pitisha malipo wakamuomba aendelee na kazi ya awamu ya pili huku akisubiri malipo, jamaa akawa hana pesa lakini kwa imani akiamini atalipwa akaenda kukopa pesa ili amalizie kaz ili akilipwa alipwe kamili..

Sekeseke linaanza sasa boss wake huyo kila siku anamzungusha juu ya malipo mara yupo semina mara ikaenda ikarudi mpaka jamaa ikabidi awaite wanakamati wote siku hiyo boss wake akagoma kutokea ikabidi jamaa aende hadi kwa boss wake kumfata, akamkuta yupo anaenjoy na familia yake tu ndo kufanya komand pale boss akamwambia asubirie mkandarasi aje akague ikabidi awe mvumilivu baada ya siku kadhaa mkandarasi akaja nae akapiga biti mara kazi mbovu mara rudia porojo kibao mwamba akawa mnyonge akarekebisha palipokuwa na makosa akamaliza.

Sasahivi akipiga simu ya mkandarasi apokelew wala boss haonekani, mwamba yupo kama kakata tamaa hata akija kazini ni yupo kama mgonjwa, siku moja nikamfuma analia chooni alivyoniona akanawa uso chap. mm nkavunga japo nilielewa kiufupi mwamba anaish kwa mawazo mazito na changamoto za empty pocket hadi anatia huruma.

Anawaza hadi kuroga mtu😃😃.. anasema chanzo cha ubaya na matatizo binadamu wenyewe ndio chanzo.

Ushauri wenu wadau kwa huyu ndugu yetu..
Yote yaliyo andikwa apa ni kwa ruhusa yake. Asanteni.
Life is full of experience. Don't be honest to the world. Kuna mawili au aamue kuipata hiyo hela kimafia na kazi ife au avumilie ni kipindi cha mpito mwambie asiwaze sana atalipwa sema kidogo kidogo. ninamtabiria kuja kuwa tajiri mkubwa mkandarasi Mark ma words.
 
Hii kesi tamu sana , ila inabidi asacrifice kazi. "Ukitaka kuua nyani,usimwangalie usoni"...inawezakana anashindwa kufanya maamuzi sababu hana income nyingine.
Ni unyanganyi wa wazi na usio na woga, aibu kabisa!
 
Life is full of experience. Don't be honest to the world. Kuna mawili au aamue kuipata hiyo hela kimafia na kazi ife au avumilie ni kipindi cha mpito mwambie asiwaze sana atalipwa sema kidogo kidogo. ninamtabiria kuja kuwa tajiri mkubwa mkandarasi Mark ma words.
ntampa hilo tumain nimemark u'r wrd
 
Kuna jamaa huko mikoa ya magharibi alipewa tenda kubadilisha madirisha kwenye kituo cha afya na kuweka ya aluminum, akafanya kazi yake vizuri sana na akamaliza. Sasa kulipwa ikawa issue, jamaa alivyoona usumbufu umezidi akaenda kung'oa madirisha yote ya aluminum aliyoweka. Aisee jamaa wakamfanyia figisu wakamkamata na kumbambikia makosa na akawekwa ndani. Haya mambo yana uonevu mkubwa sana sometimes.
 
Nyie wanakamati inatakiwa jamaa awaroge wote muwe machizi, hivi mnawezaje kumlazimisha mtu afanye kazi bila mkataba wowote?? Mimi majuzi fundi wa welding tulipatana anitengenezee geti kwa sh laki saba tuu lakini tuliandikishiana mkataba, kwenye pesa sitaki kuamini watu hovyo hovyo aiseeee. Ila huyo bosi akiendelea kukaza mwambie aje pm nimpe mbinu chaap ya kumtoa shipa huyo bosi.
mtamrejeshea maan alisema anaiyo nia kbsa kwa mateso anayopitia
 
Atumie akili ya kazi, amfate boss amawambie kwenye hizo pesa anazodai kama boss atazitoa yeye atampa kiasi flan amtangazie dau nono tu, then boss atauvagaa huo mtego akilipa, nae apige kimya
 
Ndio kbsaaa
Naiona changamoto ya conflict of interest. Lakini kwa kuanzia aongee na DED wake kwanza. Akishindwa amcheki RAS akibounce hapo kuna route ntakushauri later.

kwa kuwa jengo limeisha aandike barua ya kukabidhi kazi kwa sababu bila kukabidhi itaonekana kazi haijakubalika na kutoa mwanya wa kuzungushwa kulipwa. Awaandikie sasa kwa sababu shule zinazojengwa kwa mradi wa SEQUIP zinatakiwa kuwa zimekamilika na kuanza kutumika January. Akichelewa kukabidhi msala utakuwa kwake kwa kuwa itaonekana kashindwa kazi. Aongee na Eng. vizuri pia kwa sababu huyo ndie kashikilia kamba hapo.

Na inavyoonekana tayari Mwalimu Mkuu, Engineer na Afisa Elimu walishakula cut bila kumshirikisha kwa kufikiri wa tam fix tu kwa sababu hela za hiyo miradi zipo mashuleni tayari.

Mwambie asiwe mnyonge.
 
Back
Top Bottom