Akajibu "Baba hatumpi kura kiongozi kwa kumlipa fadhila, tutaangalia sera na Uwezo wake kutekeleza"

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566
Salaam ndugu yangu,

Ilikuwa mwaka 2019 siku chache kabla ya Uchaguzi, Mzee mmoja aliyekuwa akigombea nafasi ya Uenyekiti alikuwa na ukaribu Mkubwa na mjomba wangu.

Mgombea huyo ilikuwa hakosi kuwaita Jamaa na marafiki (akiwemo Mjomba kwenye vikao vya pombe na bata nyinginezo).

Ghafla Mzee akaanza kujitokeza kusaidia mipira timu za Vijana pale mtaani kwetu kitunda kwa kununua mipira, vuvuzela, kununua maji jambo ambalo kila mtu alishangazwa.

Ilipofika usiku mmoja kabla ya Uchaguzi Mimi na ndugu zangu tukiwepo sebleni. Mjomba alirudi muda wa saa mbili usiku akakaa na Sisi. Baada kama ya dakika kumi akamtuma mdogo wangu awaite dada zangu na Shangazi wake sebleni mara Moja, dogo akafanya hivyo.

Tulipotimia wote sebleni nakumbuka mjomba akasema "Wanangu nimewaita hapa najua si kawaida, poleni sana kwa kuwasumbua. Nina ombi dogo tu ambalo nataka Kila mmoja kwa nafasi yake naomba anitekelezee."

Akauliza, si mnajua kuwa kesho tunachagua Wenyeviti wa Mtaa wetu wapya? Tukajibu "Tunajua Anko"

Akaendelea " Ewaaaah sasa Kuna yule Mzee (Jina namhifadhi) amekuwa mwema sana kwetu, hapiti sehemu akaniacha, amekuwa anatusaidia sana hivi karibuni Hata nyie naamini mmeona.

Tukajibu "Kweli kabisa Anko"

Akaendelea "Kesho ndiyo siku ya kumlipa fadhila ya asante kwa kumpigia kura. Hivyo, kwakuwa wote humu ndani (Watu nane) umri wenu unaruhusu naomba mkampigie kura Mzee yule.

Sauti chache zikasikika zikiitikia Sawa Anko hakuna shida.

Lakini kaka Mkubwa (mtoto wa Anko) aliyemaliza Chuo akajibu

"Baba hatumpigii kura kiongozi kwa kumlipa fadhila, tutaangalia sera na uwezo wake kutekeleza"

Kimoyo moyo nikasema Bro ana pointi hapa, atafika mbali.

Vipi wewe ulimpigia kiongozi wako wa Mtaa kura kwa kuzingatia nini hasa?
 
Salaam ndugu yangu,

Ilikuwa mwaka 2019 siku chache kabla ya Uchaguzi, Mzee mmoja aliyekuwa akigombea nafasi ya Uenyekiti alikuwa na ukaribu Mkubwa na mjomba wangu.
Mimi kwa kweli ni sera na kwakuwa ni wa mtaa huwa nafuatilia mwenendo. Vipi huyo mgombea wa Mjomba alishinda?
 
Hakika Mzee
Chadema mnashida sana

Kimsingi uchaguzi ulikuwepo serikali mitaa ila mchakato ulikuwa batili

Nilitarajia uulize ,kwann anko alikimbilia kusema anawaomba wale(ankoz)wakapige kura wakati hajawahi wala hajui kama walijiandikisha? Kwasababu uchaguzi pia serikali za mitaa sio umri pekee miaka 18 kuendelea ndo wapiga kura ni lazima ukajiandikishe na jina kurudi libandikwe eneo la kituo husika

Kwa msingi huo ,CCM na mjomba mtu wanauwezo mkubwa kubeba watu kwenda kupiga kura vituo visivyo vyao wahusika hasa uchaguzi serikali mitaa ,chadema mnajitahidi changamoto kama hizo fanyieni kazi
 
Chadema mnashida sana

Kimsingi uchaguzi ulikuwepo serikali mitaa ila mchakato ulikuwa batili

Nilitarajia uulize ,kwann anko alikimbilia kusema anawaomba wale(ankoz)wakapige kura wakati hajawahi wala hajui kama walijiandikisha? Kwasababu uchaguzi pia serikali za mitaa sio umri pekee miaka 18 kuendelea ndo wapiga kura ni lazima ukajiandikishe na jina kurudi libandikwe eneo la kituo husika

Kwa msingi huo ,CCM na mjomba mtu wanauwezo mkubwa kubeba watu kwenda kupiga kura vituo visivyo vyao wahusika hasa uchaguzi serikali mitaa ,chadema mnajitahidi changamoto kama hizo fanyieni kazi
Mimi sio mfuasi wa chama chochote ndugu, najaribu kusimulia tu tukio lilivyotokea
 
Mimi sio mfuasi wa chama chochote ndugu, najaribu kusimulia tu tukio lilivyotokea
Kama upo mjini jitahidi mwaka huu,kaandikishe jinalako hata mitaa Saba ,au mitano majina Yako
Tofauti tofauti

Mf
Mtaa y ,kajiandikishe nasomi lubigida

Mtaa ,x ,Aly eggs tembele
Mtaa A ,ngengemkeni mitomingi
Mtaa B ,mabala the fisher
Mtaa c, newton trump putin

Ukienda na muda sikuhiyo ,mitaa hiyoyote utapiga kura kama utapigia CCM au Cuf huo ni ujinga wako ,kote huko hutahojiwa kitambulisho ila msimamizi atahoji jina lako tu
 
Salaam ndugu yangu,

Ilikuwa mwaka 2019 siku chache kabla ya Uchaguzi, Mzee mmoja aliyekuwa akigombea nafasi ya Uenyekiti alikuwa na ukaribu Mkubwa na mjomba wangu.

Mgombea huyo ilikuwa hakosi kuwaita Jamaa na marafiki (akiwemo Mjomba kwenye vikao vya pombe na bata nyinginezo).

Ghafla Mzee akaanza kujitokeza kusaidia mipira timu za Vijana pale mtaani kwetu kitunda kwa kununua mipira, vuvuzela, kununua maji jambo ambalo kila mtu alishangazwa.

Ilipofika usiku mmoja kabla ya Uchaguzi Mimi na ndugu zangu tukiwepo sebleni. Mjomba alirudi muda wa saa mbili usiku akakaa na Sisi. Baada kama ya dakika kumi akamtuma mdogo wangu awaite dada zangu na Shangazi wake sebleni mara Moja, dogo akafanya hivyo.

Tulipotimia wote sebleni nakumbuka mjomba akasema "Wanangu nimewaita hapa najua si kawaida, poleni sana kwa kuwasumbua. Nina ombi dogo tu ambalo nataka Kila mmoja kwa nafasi yake naomba anitekelezee."

Akauliza, si mnajua kuwa kesho tunachagua Wenyeviti wa Mtaa wetu wapya? Tukajibu "Tunajua Anko"

Akaendelea " Ewaaaah sasa Kuna yule Mzee (Jina namhifadhi) amekuwa mwema sana kwetu, hapiti sehemu akaniacha, amekuwa anatusaidia sana hivi karibuni Hata nyie naamini mmeona.

Tukajibu "Kweli kabisa Anko"

Akaendelea "Kesho ndiyo siku ya kumlipa fadhila ya asante kwa kumpigia kura. Hivyo, kwakuwa wote humu ndani (Watu nane) umri wenu unaruhusu naomba mkampigie kura Mzee yule.

Sauti chache zikasikika zikiitikia Sawa Anko hakuna shida.

Lakini kaka Mkubwa (mtoto wa Anko) aliyemaliza Chuo akajibu

"Baba hatumpigii kura kiongozi kwa kumlipa fadhila, tutaangalia sera na uwezo wake kutekeleza"

Kimoyo moyo nikasema Bro ana pointi hapa, atafika mbali.

Vipi wewe ulimpigia kiongozi wako wa Mtaa kura kwa kuzingatia nini hasa?
Hii hadithi yako ndio inaitwa fashion simulizi au hadithi inayoishi kama Bibilia
 
Back
Top Bottom