mchillo
JF-Expert Member
- Oct 13, 2010
- 500
- 224
Mimi ni mteja wa Kampuni hiyo ya simu toka iingie nchini kama Celtel, Zain na sasa Airtel lakini hakuna wakati niliokwazwa nao kama safari hii wanapojiita Airtel.
Nilianza kukwazwa na tangazo lao lililonihamasisha "kujirusha" kwa Tsh. 250/= ili nipate muda wa hewani wa Dk 15 au Tsh. 500/= kwa muda wa Dk 30. Mara kadhaa nilipojaribu kujiunga niliishia kukatwa fedha bila ya kupata huduma husika, yaani licha ya kukatwa fedha na kutumiwa msg ya kuthibitisha kujiunga na huduma ya "Piga Simu bure Airtel kwenda Airtel" waliendelea kunikata fedha zilizoko katika salio la simu yangu hadi zilipokwisha waliponijibu kwa ujumbe wa "Salio lako halitoshi kupiga simu unayotaka... tafadhali ongeza salio...". Nimejaribu kujiunga mara kadhaa na kuishia hivyo hivyo!
Kama kwamba hiyo haitoshi tatizo kubwa zaidi huja pale unapotaka kuwasiliana na wahudumu kuwaarifu yaliyokusibu simu itakuchukua kati ya nusu saa hadi saa nzima kumpata opereta wa kukujibu kama una bahati.
Hali hii ya kuchelewa kujibu simu imewakatisha tamaa maajenti na wanakataa au kutoza bei kubwa zaidi kwa wanaotaka kurejesha namba zao za zain zilizopotea au kuandikisha laini za simu.
Kuna mwana JF yeyote aliyekwazika kama mimi? Kilio chetu tukipeleke wapi?
Nilianza kukwazwa na tangazo lao lililonihamasisha "kujirusha" kwa Tsh. 250/= ili nipate muda wa hewani wa Dk 15 au Tsh. 500/= kwa muda wa Dk 30. Mara kadhaa nilipojaribu kujiunga niliishia kukatwa fedha bila ya kupata huduma husika, yaani licha ya kukatwa fedha na kutumiwa msg ya kuthibitisha kujiunga na huduma ya "Piga Simu bure Airtel kwenda Airtel" waliendelea kunikata fedha zilizoko katika salio la simu yangu hadi zilipokwisha waliponijibu kwa ujumbe wa "Salio lako halitoshi kupiga simu unayotaka... tafadhali ongeza salio...". Nimejaribu kujiunga mara kadhaa na kuishia hivyo hivyo!
Kama kwamba hiyo haitoshi tatizo kubwa zaidi huja pale unapotaka kuwasiliana na wahudumu kuwaarifu yaliyokusibu simu itakuchukua kati ya nusu saa hadi saa nzima kumpata opereta wa kukujibu kama una bahati.
Hali hii ya kuchelewa kujibu simu imewakatisha tamaa maajenti na wanakataa au kutoza bei kubwa zaidi kwa wanaotaka kurejesha namba zao za zain zilizopotea au kuandikisha laini za simu.
Kuna mwana JF yeyote aliyekwazika kama mimi? Kilio chetu tukipeleke wapi?