Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
- Thread starter
- #41
WanaArusha wanaweka historia ya ukombozi wa pili wa nchi hii. Hongereni sana.
Sidhani hata uwezo wa kukwepa risasi unao? Amani ikitoweka ndipo utajua nini maana ya kuwa na Amani! CCM endeleeni kulinda Amani Tanzania, Amani bado ipo ya kutosha ila kuna watoto wa shetani wanataka Amani itoweke!
Lakini mie nauliza -- kosa la Lema ni lipi? Mie nadhani polisi waliweke suala hili wazi.
Hivi mtu akienda kusikiliza kesi yake atangaze kwamba watu wengine wasiende kusikiliza kesi yake? Sheria hiyo imeanza lini?
Hivi mtu akitoka mahakamani kusikiliza kesi yake ni lazima aondoke hapo kwa gari? Sheria hii nayo imeanza lini?
Hivi mtu akikataa dhamana na kukubali kwenda rumande ni kosa? Sheria hii imeanza lini?
Hivi iwapo dhamana iko wazi na wadhamni wanataka kumtoa hakimu anakataa ni kosa? Hii sheria imeanza lini?
Matukio ya jana na leo katika mji wa Ukombozi wa Arusha umeianika serikali ya CCM bila nguo mbele ya mgeni wao kutoka nchi tunakotembezea bakuli hali nchi yetu ni tajiri.
Kikubwa zaidi yanaonyesha mji huo ni kama vile CCM imekwisha kabisa hali iliyojitokeza tangu uchaguzi wa mwaka jana. Wanachofanya ni kutumia polisi kujaribu eti waonekane CCM bado ipo hapo.
Ni aibu kubwa sana kwa CCM kupoteza mji waliokuwa wanaringa nao wa kitalii na mikutano ya kimataifa.
Serikali ya magamba imejaribu kutumia nguvu kubwa tangu uchaguzi mkuu, uchaguzi wa meya, na hadi sasa lakini wanaArusha wako imara sana.