Washawasha
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 16,652
- 13,077
ni kweli kabisa watz wa sasa si wale wa kale wa kushabikia mtu kujipeleka jela mwenyewe ili wengine waumie.Nalog off
mmezoea kukimbizwa nyie. Askari wasomi hao polisi jamii. utii bila shurti. Vinginevyo hao walikuwa wachaga watawasambaratishaje ndugu zao.Za libya zinakuja taratibu.
Dalili nzuri ya wanajeshi kuwaunga mkono wananchi.
Siwezi nikawa ivyo unavyosema coz nimekesha mpaka saa kumi na moja kasoro chini ya bendera ya CDM.Unamaanisha wewe ni moja ya gamba?
Jioni ya leo Arusha ni shwari kabisa wafuasi wa Chadema hawana lao wameanza kulala mapema na Mji umetawaliwa na Shangwe za vijajana wa UVCCM. Chadema Kwishenei Arusha vijana wanaimba nyimbo za kukiponda chama kwa kushindwa kuwaunganisha na kuwatelekeza hivyo kwa ufupi ni ushindi wa CCM dhidi ya CDM
Kwenda huko PUMBAVU wee!!Hivi lini vijana mtaacha ushabiki wa siasa za vyama hivi ambavyo haviwapi maslahi yeyote?
CCM wamekula nchi wamevimbewa, CHADEMA siyo wakombozi wa kweli wa taifa hili pindi watakapopata watakua ni zamu yao kula nchi.
Demokrasia katika nchi maskini yenye ujinga ni mchezo wa wajanja wachache wenye upeo huu au ule, walio nje wanapigana kuwatoa walio ndani ili wapate nafasi ya kumiliki nguvu za dola na faida zake kuzibinafsisha huku nyie mkitumiwa tu.
baada ya kupata madaraka vijana hutemwa na ukamanda huu upambanaji utupya nje kwa sababu hauna tija tena ukiwa mtawala, harakati ni pale ukiwa nje ya utawala kwa sababu ya kuona mabaya mengi na kutokuwepo kwako kwenye serikali.
Mimi ni mwanaharakati siyo shabiki wa kisiasa wa chama chochote, kuna mazuri na mabaya katika vyama vyote, na ubaya wa CCM ni obvious kwa sababu wametawala nchi na wameonekana walichoshindwa kufanya, ila tatizo linakuja kwa vijana kujipa matumaini ya hali juu sana juu ya uwezo wa CHADEMA kuleta mabadiliko ya kiuchumi, kijamii, na kisiasa hapa nina matatizo napo kwani hili lina nafasi finyu sana angalieni nchi karibu zote za kiafrica wapinzani wamefanya nini baada ya kushinda na sisi siyo tofauti na hao)
kuweni na matumaini ya kawaida ya kupunguza hizi kero za CCM na siyo kushabikia kitu mpaka mnakua paranoid mkisia tu mtu anaisema CHADEMA mnahamaki, mishipa inawachachamaa na jasho la ghadhabu kuwatoka
Hizi nguvu ni vizuri mngezitumia pia katika ufahamu wa mambo na kuanzisha na kujiunga kwenye vyama vya kijamii ili tukuze zaidi demokrasia yetu na siyo ushabiki huu wa kihisia hisia unazuia mantiki kushika nafasi yake. Mtaendelea kutumia mpaka lini?
Nafikri hawa moderators hawatoitoa na hii thread maana wamekua PARTISAN sana bila ya kua na Uhakika na kilichoandikwa ni kinagusa nini haswa
Bravo Mkuu,asante saana....!!CCM inaamua kutumia ubabe kwa CDM na wananchi wa Arusha. Lakini CCM itambue kwamba wanazidi kujipalia makaa ya mawe. Wananchi wa sasa sio wa ile miaka ya zamani ambao walikuwa wanajua CCM tu. Watu sasa wanaona na wanatambua nini kinaendelea nchini.
CCM itambue kwamba inazidi kuimarisha umaarufu wa CDM.
Hongera CDM.
I want to cry with happiness -- BYE BYE CCM Arusha. Ingefaa muyaondoe makao yenu hapo -- hamna kitu kabisa mlichobaki nacho ni vituko tu wat msio na haya. Mnashindwa hoja mnakimbilia polisi, pambana kiume, ebo!!!!