Afande Sele awa-beep Sugu na Vinega!

matumbo

JF-Expert Member
Jul 9, 2011
7,225
3,944
Msanii wa kizazi kipya Afande Sele ambae kwa sasa anavuma mtaani kwa jina la Yuda Eskariot,ameongelea kuhusu ishu yake ya kupafom pale Leaderz,akiojiwa Mlimani Radio alisema.

Namnukuu..." kwanza napenda kusema nasikitishwa sana na mambo yanayoendelea hivi sasa,ninatukanwa na kudhalilishwa nikiitwa msaliti,lakini ukweli sijasaliti,mimi ni mpambanaji na siku zote nimepigana vita hii nimejitolea sana wakati huo wenzangu walianza kufanya mambo yao bila kunishirikisha,na hii ilikuja baada ya mimi kukataa kushiriki kuimba kwenye album ya antivirus volume 2,niliwaambia mimi nina familia na watu wengine wananiangalia so siwezi kutukana..kitu kingine MIMI NINA IMANI YA KIRASTA NA WENZANGU WANA IMANI ZA KI-HUSTLER ndio maana tunapishana sana maamuzi,niliwaambia wenzangu kuwa msimamo wangu mimi ni KUWAPATANISHA HAWA WATU WAWILI(Sugu&Ruge),kwa kuwa Sugu sasa ni mtu mkubwa nchi hii naweza kumuita jamaa na kumuweka chini wakanyoosha penye makosa"

SABABU ZA KUPAFOMU LEADERZ,anasema "kukosa mwaliko wa Antivirus,wenzangu hawakunitaarifu na hata kwenye matangazo yao hawakuniweka ndio maana nilipoitwa uku nikakubali,mimi naishi kwa kutegemea muziki,sasa siwezi kukataa kazi wakati nina shida ya pesa ndio maana nilipoitwa uku nilikubari LAKINI HAIMAANISHI KUWA NIMEACHANA NA HARAKATI AU SIWAUNGI MKONO WENZANGU..hata hivyo BADO NAENDELEA KUWASILIANA NA SUGU ILI TUZUNGUMZE..
 
Wengine huwa hatufautilii sana kinachoendelea ktk hii tasnia ya muziki wa hapa bongo hivyo naomba ufafanuzi kidogo huo upande wa ANTIVIRUS una kina nani na VINEGA kuna kina nani maana kila siku naona post humu lkn sizielewi kabisa
 
Wengine huwa hatufautilii sana kinachoendelea ktk hii tasnia ya muziki wa hapa bongo hivyo naomba ufafanuzi kidogo huo upande wa ANTIVIRUS una kina nani na VINEGA kuna kina nani maana kila siku naona post humu lkn sizielewi kabisa

ANTIVIRUS ni harakati(movement) inayopigania mabadiliko kwenye mfumo mzima wa tasnia ya sanaa,ili mwisho wa siku msanii yoyote wa kitanzania anufaike na jasho lake,tofauti na ilivyo sasa..kama wewe una hali/mtazamo wa kuboresha/kufanikisha mapinduzi kwenye sanaa ya hapa nyumbani,na wewe ni member wa Antivirus,haijalishi..

Vinega ni genge la watu mbalimbali (ikiwemo wasanii wa bongofleva waliochoshwa na unyonyaji kwenye sanaa ya bongo) wanaofanikisha mission ya Antivirus..nafikiri umenisoma Myhem.
 
Afande ni msaliti tu,hawezi kutukana? Wadau natumia cm ningekuwa kwenye pc ningeweka hile clip ya afande akiwatukana wafu fm!!! Akumbuke sugu ndo kamtoa kimuziki,afande wew ni mnafiki na msaliti haufai kabisa kuwepo kwenye genge la vinega.
 
Wengine huwa hatufautilii sana kinachoendelea ktk hii tasnia ya muziki wa hapa bongo hivyo naomba ufafanuzi kidogo huo upande wa ANTIVIRUS una kina nani na VINEGA kuna kina nani maana kila siku naona post humu lkn sizielewi kabisa

Mkuu VINEGA ni wanamziki wanaotumia ANT-VIRUS kuscan VIRUS Zinazo wanyonya WASANII. Unakuta msanii wa Bongo anafanya show lakini malipo yake inakuwa ni chakula, Nguo za kupandia jukwaani na nyimbo zake kupigwa kwenye station za clouds media. mia
 
Afande ni msaliti tu,hawezi kutukana? Wadau natumia cm ningekuwa kwenye pc ningeweka hile clip ya afande akiwatukana wafu fm!!! Akumbuke sugu ndo kamtoa kimuziki,afande wew ni mnafiki na msaliti haufai kabisa kuwepo kwenye genge la vinega.

hebu soma maelezo yake kdgo kijana.ku mtoa kimziki c tatizo,ku2kana kasema awezi hebu kuwa muelewa kdgo
 
hebu soma maelezo yake kdgo kijana.ku mtoa kimziki c tatizo,ku2kana kasema awezi hebu kuwa muelewa kdgo

Afande ni muongo mbona kuna clip youtube ametukana sana wafu fm? Kwani kutukana kwenye anti-virus na jukwaani kwa watu walewale inakua tofauti? Afande ni mnafiki hatumtaki kabisa kwenye genge la vinega atakua snitch tu
 
Afande anasema yeye anafamilia inamtazama,mbona anavua nguo hadharani tena jukwaani,haoni kwa hili anamuaibisha sana mwanae Tunda!?

Na kama mitazamo yao imetofautiana mbona anataka kumtafuta Sugu ili iweje?mbona alishiriki Antivirus vol 1?ina maana hao aliowatukana leo hii wamebadilika,na kila kitu kinaenda sawa.

Rasta gani anaekubali kuwa ngao ya kumkinga muovu?
Pia mbona nae amekubali kueneza PROPAGANDA kuwa hii movement ya antivirus ni beef kati ya Ruge na Sugu?

Mi naona hapa Afande anajaribu kutafuta huruma ya wananchi.
 
hebu soma maelezo yake kdgo kijana.ku mtoa kimziki c tatizo,ku2kana kasema awezi hebu kuwa muelewa kdgo

Mkuu na wewe kuwa muelewa. KUTUKANA ni maneno yanayotumika kupotosha maana. Hawa CLOUDS MEDIA unapotumia maneno makali kuwasema wanasema umewatukana, na kwa sababu wanasehemu ya kuongelea ni lahisi kupotosha Umma. mfano "cluods fm ni wanyonyaji, 26/11/2011 Mtasanda ndo siku ya kifo chenu, tutawascan". tusi liko wapi? Mia
 
Afande ni msaliti asie hitaji huruma. Rasta siku zote hawezi kuungana na wanyonyaji. Rasta ni mpambanaji na mwanaharakati wa kutetea haki. Asitafute huruma kwetu.
 
Mkuu na wewe kuwa muelewa. KUTUKANA ni maneno yanayotumika kupotosha maana. Hawa CLOUDS MEDIA unapotumia maneno makali kuwasema wanasema umewatukana, na kwa sababu wanasehemu ya kuongelea ni lahisi kupotosha Umma. mfano "cluods fm ni wanyonyaji, 26/11/2011 Mtasanda ndo siku ya kifo chenu, tutawascan". tusi liko wapi? Mia

na walivyokuwa wanaimba rugay shoga!rugay shoga! Au co matusi hayo? Na line za sugu zinazosema rugay mother fxxcker?yoo acha ku
tetea upuuzi yoo...
 
na walivyokuwa wanaimba rugay shoga!rugay shoga! Au co matusi hayo? Na line za sugu zinazosema rugay mother fxxcker?yoo acha ku
tetea upuuzi yoo...

mwambie uyo bosi wako ashukuru Mungu sana sasa ivi anatukanwa..kuna siku atazikwa mtu.
 
Alisaini deal wakati amelipuliza baada ya kwisha sasa anaona ajitete..Huyu kuna clips ametukana sana tu!
 
afande hana point katika hoja zake ,,yeye ni rasta ni sawa hawezi kutukana well and good,,lakini mbona alichojoa jukwaani ? kwani huo ndio u rastafalian? point yake ni moja tu njaa kali na ikizingatiwa shoo zimemkaukia....
 
hebu soma maelezo yake kdgo kijana.ku mtoa kimziki c tatizo,ku2kana kasema awezi hebu kuwa muelewa kdgo
Dogo hapa sio Facebook, jifunze kuandika vizuri. watu wanaosoma hapa sio age mate wako na sio wote wanaofahamu hozo lugha zenu za facebook.
 
Hili jamaa ni dunce kwa sababu limedai lilikataa kushiriki kuimba kwenye anti-virus kwa sababu ina matusi, lakini tamasha la anti-virus la wiki iliyopita angekwenda kushiriki kama kina sugu wangemwalika. How absurd.
 
Back
Top Bottom