Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 876
- 4,101
Zitto Kabwe amedai wamepenyeza watu ndani ya CCM sijui lengo la hao watu ni nini ila ninachofahamu mimi chama chake kimekuwa CCM B kwa muda sasa.
ACT Wazalendo iliundwa baada ya Zito na Kitila Mkumbo kubainika kwamba wametumwa na CCM kwa ajili ya kuivuruga Chadema. Zitto ni mwanasiasa pekee nchni wa ngazi ya juu kutoka upinzani ambaye katika historia ya maisha yake hajawahi kukamatwa na kutiwa ndani kisa kubambikiwa kesi.
Ni mwanasiasa ambaye wakati wote upingana na wenzake hasa kuhusu mikakati ya kuitoa CCM madarakani. Aina hii ya mwanasiasa haireflect mpinzani wa kweli bali inareflect mwanaccm aliyejivika ngozi ya upinzani.
Zitto kazi yake haina tofauti na wanayofanya akina Lipumba, Mrema na Selasini. Wanaishi kwa hisani ya tumbo zao na si vinginevyo.
Kuhusu demokrasia ndani ya chama, Zitto anadai anaishi demokrasia. Nataka kujiuliza tafsiri yake ya demokrasia ni ipi? Ameona chama kimekosa nguvu na uungwaji mkono, amebaini anakubalika kigoma mjini pekee na Zanzibar baada ya lipumba kuiua CUF. Leo amekaa pembeni kimwili ila kiroho yupo pale juu.
Mpinzani gani kila kukicha anapambana na wenzake huku akiwasifu watawala? Kama kweli ni mwana demokrasia akae pembeni aache na kugombea Ubunge.
ACT Wazalendo iliundwa baada ya Zito na Kitila Mkumbo kubainika kwamba wametumwa na CCM kwa ajili ya kuivuruga Chadema. Zitto ni mwanasiasa pekee nchni wa ngazi ya juu kutoka upinzani ambaye katika historia ya maisha yake hajawahi kukamatwa na kutiwa ndani kisa kubambikiwa kesi.
Ni mwanasiasa ambaye wakati wote upingana na wenzake hasa kuhusu mikakati ya kuitoa CCM madarakani. Aina hii ya mwanasiasa haireflect mpinzani wa kweli bali inareflect mwanaccm aliyejivika ngozi ya upinzani.
Zitto kazi yake haina tofauti na wanayofanya akina Lipumba, Mrema na Selasini. Wanaishi kwa hisani ya tumbo zao na si vinginevyo.
Kuhusu demokrasia ndani ya chama, Zitto anadai anaishi demokrasia. Nataka kujiuliza tafsiri yake ya demokrasia ni ipi? Ameona chama kimekosa nguvu na uungwaji mkono, amebaini anakubalika kigoma mjini pekee na Zanzibar baada ya lipumba kuiua CUF. Leo amekaa pembeni kimwili ila kiroho yupo pale juu.
Mpinzani gani kila kukicha anapambana na wenzake huku akiwasifu watawala? Kama kweli ni mwana demokrasia akae pembeni aache na kugombea Ubunge.