A vote of confidence for Mama Anne-Kilango Malecela

JF Senior Expert Member Join Date: Tue Feb 2007

Re: A vote of confidence for Mama Anne-Kilango Malecela

Nipe popote ANNE alipowahi kusema lolote juu ya hili jambo kama ulivyosema hapo awali.....But naamini kuwa binadamu huwa wanabadilika kulingana na wakati, matukio, mazingira, na hata matukio. Ninachosisitiza ni kuwa tunahitaji muda wa kujua na pia anatakiwa kuonyesha dhahiri kuwa hakuna politics of revenge.

Mkuu Mheshimiwa

1. Heshima mbele mkuu wangu, ninaomba kukwambia neno moja muhimu, mimi binafsi nipo hapa JF, na sehemu mbali mbali za taifa za habari kwa wananchi, kwa sababu moja muhimu, nayo ni taifa langu na lako, Tanzania, mimi nina tatizo na viongozi wabovu, wahuni, wezi, na wasiokuwa na heshima kwa wananchi, na the most important of all, sipendi unafiki, kuanzia kwa viongozi mpaka sisi wananchi wenyewe.

2. Sasa ninaomba nikuambie wazi kuwa ninajua nyuma ya jina lako kuna nani, sasa kama wewe kweli ni mkweli, na usiyependa unafiki, unayelipenda taifa lako kama ninavyofahamu unavyopenda kufahamika:-

Naomba useme wazi hapa JF, mbele ya wananchi wakiwa mashahidi, kwamba nguvu unayoitumia kumshambulia Mama Kilango kwa kutetea wanyonge, mbona toka uingie hii forum JF, hujawahi kuwakemea kwa nguvu zote viongozi wafuatao, Mkapa, Chenge na Lowassa? WHY? mbona una nguvu sana ya kumshambulia huyu mama likini huna nguvu ya kuwashambulia hao niliowataja huko juu? Kwa nini Mkapa, Chenge, na Lowassa, wakishambuliwa huonekani kabisaaa hata comment? WHY? Je katika uhai wa maisha yako, kuna wakati wowote uliwahi kuwa mbunge? Ulifanya nini hasa?

3. Ninaomba kuwakumbusha wale wote ambao pamoja na wewe, mnaomshambulia Mbunge Shujaa Mama Kilango, ninasema hivi Mama Kilango, na wabunge kama Zitto, Dr. Slaaa, na Dr. Mwakyembe, kuna kitu kiomoja cha maana wanachotufanyia wa-Tanzania, ni kwamba wametupandia mbegu za mapinduzi, ambazo huenda hawataishi long enough kuona matunda yake, lakini ninawahakikishia kuwa hakuna atakayeweza kuzing'oa, au kuzizima hizi mbegu,

Ni m-Tanzania asiyekuwa na uwezo mkubwa wa kufikiri ndiye anyeweza kuamini kuwa itatokea kwa urahisi viongozi mafisadi kufungwa, au kusumbuliwa na serikali yetu, lakini one thing guaranteeed hapa ni kwamba mbegu wanazozipanda hawa viongozi, Mama Kilango included, tutazipokea na kuziendeleza when the time comes, hawa wametuwekea msingi mzito ambao haukuwepo kwenye taifa letu, leo viongozi wote wa taifa hakuna anayekubali kusaini mkataba wowote kwa urahisi, infact juzi kiongozi mmoja aliniambia kuwa yeye hakubali mkataba wowote mpaka aupitishe kwa mawakili kama watatu kwanza,

alisema "...mambo yamebadilika kijana......."

Kwa wale tunaongalia a big picture ya taifa letu, tunawashangilia, na kuwafagilia, kwa sababu ya mbegu nzito wanazozipanda kwa ajili ya the future ya taifa letu, only small mind people ndio wanajali sifa za kina Mama Kilango, either viongozi hawa wanayafanya haya kwa kujua au kutokujua, lakini matokeo ni makubwa sana ambayo hayawezi kuzimwa na kiongozi yoyote yule hata awe na nguvu au hela kiasi gani hawezi kutununua wa-Tanzania wote, labda hao kina Serukamba tu!

Mungu Awabariki Viongozi Wote Wanaolala Macho Kwa ajili Ya Taifa Letu, na awalegeze wale wote wenye nia mbaya na taifa letu!

Ahsante Mkuu!

Field Marshall ES: Sauti Ya Umeme!
 
MWK tunashukuru umerudi kidogo hapa JF palipooza...

Lakini najiuliza...MWK umepotea muda kidogo halafu ghafla, Mama Shujaa na jasiri Kilango ametoa maneno mazito bungeni na wewe umerudi,is it coincidence au ulikuwa behind the scene ukimpa somo mama? Kama ndivyo basi hongera sana MWK
 
Lakini najiuliza...MWK umepotea muda kidogo halafu ghafla, Mama Shujaa na jasiri Kilango ametoa maneno mazito bungeni na wewe umerudi,is it coincidence au ulikuwa behind the scene ukimpa somo mama? Kama ndivyo basi hongera sana MWK

Mmmmmhhh!....Au MWK ndio Mama Kilango!...
 
Namshukuru Mama Kilango kwa kutoboa kwamba kunako 1992, (sio 1996) wako viongozi waliochota 216bn/= kupitia BoT. Kumbe labda hii kuchota mabilioni mengi kupitia BoT ni kazi ya kawaida ya viongozi, ya kila mwaka?

Nani alikuwa Gavana wa BoT 1992? Kama si Marehemu basi labda aanze kuangalia kuna nini mbele.

Hizi data Mama Kilango anazipataje? Ni kwa kupitia mwenzie? Kwa vile mwenzie alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala, lazima anajua siri kali kama hizi. Labda anammegea Mama kidogo? Hii itamjenga sana Mama. Ni urithi mzuri.

Tukumbuke kwenye 1992, 216 bn/= zilikuwa ni fedha za kutosha bajezi za wizara mbili za nguvu! Mwinyi owes us an explanation!

Augustine Moshi
 
Namshukuru Mama Kilango kwa kutoboa kwamba kunako 1992, (sio 1996) wako viongozi waliochota 216bn/= kupitia BoT. Kumbe labda hii kuchota mablioni mengi kupitia BoT ni kazi ya kawaida ya viongozi, ya kila mwaka?

Nani alikuwa Gavana wa BoT 1992? Kama si Marehemu basi labda aanze kuangalia kuna nini mbele.

Hizi data Mama Kilango anazipataje? Ni kwa kupitia mwenzie? Kwa vile mwenzie alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala, lazima anajua siri kali kama hizi. Labda anammegea Mama kidogo? Hii itamjenga sana Mama. Ni urithi mzuri.

Tukumbuke kwenye 1992, 216 bn/= zilikuwa ni fedha za kutosha bajezi za wizara mbili za nguvu! Mwinyi owes us an explanation!

Augustine Moshi

Mwl. Moshi
Kwa hiyo Mwinyi naye ajitokeze aelezee ufisadi wake? Gavana alipotelea UK na huyo mwenza alikuwa Lowassa aka Pinda aka Waziri Mkuu.. 1990 - 1994. Ngoja niendelee kula nyama huku Kilimani.
 
Sam,

Kama kweli Mwinyi aligawa mabilioni yetu kwa wenzake kishenzi hivyo, basi kwanza tufahamu pasi yake iko wapi. Na auditors watafutwe haraka kuangalia akaunti za BoT za wakati huo.

Wakati sawa, Mwakyembe atayarishwe kusimamia kamati ya kuchunguza kilitokea nini. Tuanataka majibu, tena haraka! Mashahidi wengine ni wazee, inabidi tuchunguze wakati bado tunao!

Tumechoka kuibiwa jamani!
 
Sam,

Kama kweli Mwinyi aligawa mabilioni yetu kwa wenzake kishenzi hivyo, basi kwanza tufahamu pasi yake iko wapi. Na auditors watafutwe haraka kuangalia akaunti za BoT za wakati huo.

Wakati sawa, Mwakyembe atayarishwe kusimamia kamati ya kuchunguza kilitokea nini. Tuanataka majibu, tena haraka! Mashahidi wengine ni wazee, inabidi tuchunguze wakati bado tunao!

Tumechoka kuibiwa jamani!

Mwl.
Nimesha ongelea hili jambo kwamba haya matatizo hayawezi kuisha tutaondoa watu na kuwaingiza wengine nao watafanya hivyo hivyo hata kama hukumu yao itakuwa kifo mtaua mpaka mtachoka. We have to solve the problem not the result of the problem. Wewe najua ni mwalimu wa hisabati najua unaeleza sana juu ya haya mambo.
 
Sam,

Nakubaliana nawe kwamba inabidi kutatua tatizo toka mzizi wake, na sio kushughulikia matokeo yake tu.

Sasa tatizo la msingi ni mfumo mbaya wa utawala wa kulindana, na kukosekana uajibikaji. Yalipochotwa hayo mabilioni 216 lazima walifahamu au kuidhinisha Rais, Waziri Mkuu, Mkuu wa Usalama wa Taifa, Waziri wa Fedha, Gavana wa BoT, Katibu Mkuu wa Fedha, na wakuu wengne wachache. Wote hao wamelindana. Kama sio Mama Kilango kutoboa siri, huenda hatungekaa tujue.

Sasa uhujumu kama huo umeshafanyika mara ngapi? Na hao wahujumu wamekuwa wakijifanya watu wanaopenda sana Tanzania!

We need a new beginning. Inabidi CCM ikae benchi kwa kipindi cha miaka 5 au 10. La sivyo hakuna la kweli litakalofanyika. Kama Watanzania hawatakuwa na ung'amuzi wa kutosha kuona ulazima wa kuiweka CCM benchi, basi wajue wataendelea kuibiwa kishenzi hivi hivi kila mwaka. There will never be an end to it.
 
Mmmmmhhh!....Au MWK ndio Mama Kilango!...

A fantastic analogy!

And may be I should add:

The two of you are completely opposite to What I saw from Anna Abdalah. Trying to oppose all what Kilango was in to... Maneno ya Anna Abdala kwa Kilango was very demoralising ...

She said what?

Generalised frase "... Wabunge wote hatupendi ufisadi...tusitengane katika kupambana nao...hata wale tusioweza kupayuka..tunawapinga mafisadi pia..." something like that. And it was all directed to Anne Kilango.
 
Azimio Jipya,
Mkuu huyu Mama Anna Abdallah labda wambie watu wengine sio sisi wa kisiwani!...Yaani sina hata la kusema.
 
Anna Abdallah ni Fisadi huyo, alisha kula saana wizara ya Afya , kwa hiyo hawezi kusema kwanguvu, wenzie watamrudi, ndio maana anasemea kichininchini. Ili na yeye wamkatie, na waendele kumlinda.
 
Mkandara.

Ni kama tukio la pili hivi....namuona anatamka na kuelekeza maongezi kusikotakiwa... na kulikopitwa na wakati. The other time ..alijaribu ku-mcover Chenge...sikumbuki vema...lakini as if mwanga wa mapinduzi dhidi ya giza nene liliigubika nchi yetu unamuumiza na kumpofua huyu mwana Mama. I ditect something very seriouse there...Rigidness and old fashion style to do things .. kulindana..kwenda pamoja thing....kufichiana maovu nk. Uzamani mtupu uliovunda fungus of all types.

She got to be carefull! Nyakati isnt on her Favour.

Reasons?

The strong beam of light shining on this national at the moment wil not be stoped, its too positive, its powerfull, its so intense...will not hold any rubish anexposed...

Kama ni uchawi umejazana humu Tanzania utafumuliwa kuanzia nyumba ya Bunge mpaka muhimbili kijana kitafuna vichwa vya watu. Kama Giza lilificha wizi hapo BOT for several years ..all will be openly exposed...Kuanzai Kifo cha utata cha balali mpaka kurudisha Hela za EPA kwa viroba..That is the property on the MWANGA Na azimio jipya leading to the New Nation of Tanzania...Anna abdalah et al should learn this and stay aside...! Wataalamu wanasisitiza ..Usiende counter Mkondo ..hasa ukiwa wa ukombozi wa haki za watu..better swim in its favour.

Nothing Negative on the land of Tanzania will not be exposed to its extinction this time!

We always say..Mwenye macho na masikio ..should get to use them properly before its too late.
 
Augustino Moshi said:
Namshukuru Mama Kilango kwa kutoboa kwamba kunako 1992, (sio 1996) wako viongozi waliochota 216bn/= kupitia BoT. Kumbe labda hii kuchota mabilioni mengi kupitia BoT ni kazi ya kawaida ya viongozi, ya kila mwaka?

Nani alikuwa Gavana wa BoT 1992? Kama si Marehemu basi labda aanze kuangalia kuna nini mbele.

Hizi data Mama Kilango anazipataje? Ni kwa kupitia mwenzie? Kwa vile mwenzie alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama Tawala, lazima anajua siri kali kama hizi. Labda anammegea Mama kidogo? Hii itamjenga sana Mama. Ni urithi mzuri.

Tukumbuke kwenye 1992, 216 bn/= zilikuwa ni fedha za kutosha bajezi za wizara mbili za nguvu! Mwinyi owes us an explanation!

Dr.Moshi,

..nadhani kuna mafungu mawili ya fedha hizi. kuna lile la wakati wa Mzee Mwinyi na lingine la majuzi wakati Mkapa.

..pia kwa lile fungu la 1992 wabunge wa wakati ule wakiongozwa na EDWARD OYOMBE AYILA, mbunge wa Rorya, walilipigia kelele sana.

..kamati ya Bunge iliundwa kuchunguza suala hilo, iliitwa kamati ya AYILA. kamati iliwasilisha ripoti yake Bungeni na mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa.

..mwenye connection atusaidie hapa jamboforums tupate RIPOTI YA KAMATI YA BUNGE YA EDWARD AYILA. pia tupate 1992 HANSARD tujue kulizungumzwa nini huko Bungeni.

..viongozi waliokuwepo 1992 wengine sasa ni marehemu ni hawa hapa:

...Raisi Ally Hassan-- Mwinyi, Waziri Mkuu-- John Malecela, Waziri wa Fedha-- Steven Kibona/ Kighoma Malima, Gavana BOT-- Gilman Rutihinda/ Dr.Idris Rashid.

..Hata huyu Gavana wa sasa wa BOT naamini alikuwa member wa bodi ya wakurugenzi BOT ya wakati ule.
 
Jokakuu,
Tatizo la Wadanganyika ni KUSAHAU....
Sasa nadhani wanaipata picha tunapozungumzia swala la EPA na Balila kuwa halikuwa bahati mbaya.....Rutihinda yalimkuta lakini bado watu walijenga ukuta kulindana.
Mkuu NDIVYO TULIVYO!
 
Women rule!! I love strong women ....

Utajua Msukuma on the spot! Ngosha vipi unataka Mama aliyeshamiri kuyakamata "manumbu" ili mkishikana kwenye Chagulaga usikie utamu na harufu ya jasho, Sweet Nectar kama Mjomba wako Ruckus alivyosema?;)
 
Back
Top Bottom