Kitila Mkumbo
JF-Expert Member
- Feb 25, 2006
- 3,354
- 1,943
To be honest, I find it really strange and utterly naive to dismiss Mama Kilango's point of view on the basis that he did not oppose the parliament's move to punish Zitto. People on this side of the debate are using a wrong premise and therefore their conclusion is definetely flawed.
Sanasana naona mnajaribu kuwagombanisha wabunge wetu "mahiri" kwa wananchi pasipo sababu za msingi. Kazi ya msingi ya mbunge ni kutetea wananchi na nchi yake pale serikali inapojaribu kwenda kinyume na majukumu yake ya msingi. Hivi ndivyo alivyofanya Zitto na ndivyo alivyofanya Mama Kilango na wabunge wengine kadhaa hivi karibuni. Sasa kwa nini tuhoji dhamira ya mama Kilango? Viongozi wa kisiasa wanapimwa kwa maneno na matendo yao; hatuwezi kuwapima kwa yale wanayoyafikiria maana kamwe hatuwezi kuyajua. Ningeelewa hoja hizi kama mama Kilango ali-flopflip. Yaani kama kuna wakati alitetea wizi wa EPA na sasa anapinga. Otherwise, tusije tukajikuta nasi tunaanza kuwashindanisha wabunge wetu kwa umaarufu. Huo utakuwa ni uhuni maana wanayoyafanya akina mama Kilango ndivyo wanavyopaswa kuwa wanafanya siku zote.
Tatizo ninaloliona mimi hapa ni kwamba hatujazoea viongozi wetu, wakiwemo wabunge, wakitekeleza wajibu wao kiasi kwamba siku wakifanya wajibu wao inakuwa taabu kiasi cha kuwa news na kuzaa threads na threads kwenye mitandao ya internet. Yaani viongozi wametufikisha mahala ambapo sasa tunaona kwamba kutekeleza wajibu wao imekuwa ni upendeleo kwa wananchi unaostahili tuzo na pongezi kemukemu. Katika hali ya kawaida hatupaswi kuwa tunajadili na kupongeza au kuhoji dhamira ya mbunge kuibana serikali bungeni maana kwa kweli hii ndio kazi yao. Kwa utaratibu huu itafika mahala wanafunzi watakuwa wanaandamana kumpongeza mwalimu wao kwa kukumbuka kuingia darasani kufundisha kipindi chake!
Sanasana naona mnajaribu kuwagombanisha wabunge wetu "mahiri" kwa wananchi pasipo sababu za msingi. Kazi ya msingi ya mbunge ni kutetea wananchi na nchi yake pale serikali inapojaribu kwenda kinyume na majukumu yake ya msingi. Hivi ndivyo alivyofanya Zitto na ndivyo alivyofanya Mama Kilango na wabunge wengine kadhaa hivi karibuni. Sasa kwa nini tuhoji dhamira ya mama Kilango? Viongozi wa kisiasa wanapimwa kwa maneno na matendo yao; hatuwezi kuwapima kwa yale wanayoyafikiria maana kamwe hatuwezi kuyajua. Ningeelewa hoja hizi kama mama Kilango ali-flopflip. Yaani kama kuna wakati alitetea wizi wa EPA na sasa anapinga. Otherwise, tusije tukajikuta nasi tunaanza kuwashindanisha wabunge wetu kwa umaarufu. Huo utakuwa ni uhuni maana wanayoyafanya akina mama Kilango ndivyo wanavyopaswa kuwa wanafanya siku zote.
Tatizo ninaloliona mimi hapa ni kwamba hatujazoea viongozi wetu, wakiwemo wabunge, wakitekeleza wajibu wao kiasi kwamba siku wakifanya wajibu wao inakuwa taabu kiasi cha kuwa news na kuzaa threads na threads kwenye mitandao ya internet. Yaani viongozi wametufikisha mahala ambapo sasa tunaona kwamba kutekeleza wajibu wao imekuwa ni upendeleo kwa wananchi unaostahili tuzo na pongezi kemukemu. Katika hali ya kawaida hatupaswi kuwa tunajadili na kupongeza au kuhoji dhamira ya mbunge kuibana serikali bungeni maana kwa kweli hii ndio kazi yao. Kwa utaratibu huu itafika mahala wanafunzi watakuwa wanaandamana kumpongeza mwalimu wao kwa kukumbuka kuingia darasani kufundisha kipindi chake!