A vote of confidence for Mama Anne-Kilango Malecela

To be honest, I find it really strange and utterly naive to dismiss Mama Kilango's point of view on the basis that he did not oppose the parliament's move to punish Zitto. People on this side of the debate are using a wrong premise and therefore their conclusion is definetely flawed.

Sanasana naona mnajaribu kuwagombanisha wabunge wetu "mahiri" kwa wananchi pasipo sababu za msingi. Kazi ya msingi ya mbunge ni kutetea wananchi na nchi yake pale serikali inapojaribu kwenda kinyume na majukumu yake ya msingi. Hivi ndivyo alivyofanya Zitto na ndivyo alivyofanya Mama Kilango na wabunge wengine kadhaa hivi karibuni. Sasa kwa nini tuhoji dhamira ya mama Kilango? Viongozi wa kisiasa wanapimwa kwa maneno na matendo yao; hatuwezi kuwapima kwa yale wanayoyafikiria maana kamwe hatuwezi kuyajua. Ningeelewa hoja hizi kama mama Kilango ali-flopflip. Yaani kama kuna wakati alitetea wizi wa EPA na sasa anapinga. Otherwise, tusije tukajikuta nasi tunaanza kuwashindanisha wabunge wetu kwa umaarufu. Huo utakuwa ni uhuni maana wanayoyafanya akina mama Kilango ndivyo wanavyopaswa kuwa wanafanya siku zote.

Tatizo ninaloliona mimi hapa ni kwamba hatujazoea viongozi wetu, wakiwemo wabunge, wakitekeleza wajibu wao kiasi kwamba siku wakifanya wajibu wao inakuwa taabu kiasi cha kuwa news na kuzaa threads na threads kwenye mitandao ya internet. Yaani viongozi wametufikisha mahala ambapo sasa tunaona kwamba kutekeleza wajibu wao imekuwa ni upendeleo kwa wananchi unaostahili tuzo na pongezi kemukemu. Katika hali ya kawaida hatupaswi kuwa tunajadili na kupongeza au kuhoji dhamira ya mbunge kuibana serikali bungeni maana kwa kweli hii ndio kazi yao. Kwa utaratibu huu itafika mahala wanafunzi watakuwa wanaandamana kumpongeza mwalimu wao kwa kukumbuka kuingia darasani kufundisha kipindi chake!
 
Kama mnachohitaji ili muweze kuwaunga mkono viongozi au wanasiasa ni kuwaona wakisimama na kuongea maneno yanayotia moyo, basi kaeni tayari kusikia mengi tu na mnaweza kukaa mkajiburudisha kwa yale mengine mengi ambayo tayari mmeshayasikia.
Mimi ninaunga mkono wanasiasa baada ya kuona effects za matendo yao.
 
Kama mnachohitaji ili muweze kuwaunga mkono viongozi au wanasiasa ni kuwaona wakisimama na kuongea maneno yanayotia moyo, basi kaeni tayari kusikia mengi tu na mnaweza kukaa mkajiburudisha kwa yale mengine mengi ambayo tayari mmeshayasikia.
Mimi ninaunga mkono wanasiasa baada ya kuona effects za matendo yao.


Ni kweli. Lakini usisahau kuwa uanasiasa sio kama ukulima unaopimwa kwa kuangalia idadi ya magunia yaliyozalishwa. Uanasiasa ni mawazo ambayo ndio msingi wa uongozi. Kama mwanasiasa hana mawazo huyo hafai kuwa mwanasiasa.
 
Ni kweli. Lakini usisahau kuwa uanasiasa sio kama ukulima unaopimwa kwa kuangalia idadi ya magunia yaliyozalishwa. Uanasiasa ni mawazo ambayo ndio msingi wa uongozi. Kama mwanasiasa hana mawazo huyo hafai kuwa mwanasiasa.


Unachosema ni sahihi, lakini iwapo mwanasiasa ameshapewa fursa ya kuongoza basi hakuna haja tena ya kuvutiwa sana na mawazo yake mazuri au maneno yanayoleta faraja iwapo hayaleti mabadiliko yanayopimika kwenye jamii.
 
Zemarcopolo,
Hivi Mama Kilango kesha pewa fursa ipi ya kuongoza! jamani hivi kazi ya wabunge ni ipi kiasi kwamba mnataka kuona mabadiliko yanayopimika..Hivi kweli hoja za mbunge yeyote hazina uzito wa kupimwa hadi siku zitakapo fanya kazi?..
Duh basi hatuna haja kabisa ya kuwa na bunge maanake wapo kwa mamia na wote hulala usingizi, leo hawa wachache wanaowakilisha mawazo na matakwa ya wananchi wanaambiwa hawafai!.. Kazi kweli kweli!
 
Uanasiasa ni mawazo ambayo ndio msingi wa uongozi. Kama mwanasiasa hana mawazo huyo hafai kuwa mwanasiasa.

Anne Malecela nae mawazo yake yana mushkeli.

Kwa nini hakuthubutu kusema hela za EPA zikirudi watuhumiwa wasiposhitakiwa patakuwa hapatoshi, badala yake karukia ishu rahisi kusema hela za EPA zisiporudi itakuwa kasheshe baada ya Pinda tayari kuahidi zimerudi na uchunguzi unaendelea?

Kwa nini kasema anamkubali Kikwete na nia zake eti kwa sababu alitoa spichi siku anateuliwa kwamba atapitia mikataba ya madini na kwamba hana ubia na mtu wakati tumeona ana ubia na Wazungu wachimba migodi na teuzi zake ni za mafisadi, na anachana ripoti za ufisadi?

Kwa nini Malecela hajatoa wazo hata nusu kuhusu ankra na takwimu za hii bajeti zaidi ya kuongea kwa ukali kuhusu EPA kabla hajapiga kura ya 'Ndio'?

Kwa nini Malecela anaongea ki juu juu kusema mali ya nchi hailindwi badala ya kusema mali inaibiwa, kama sio ku obfuscate mambo kioga oga, kuonyesha hamna fisadi?

Kwa nini Malecela hakutaja kampuni au mtu aliyekopa bila kurudisha madeni miaka ya '90 , kama sio janja ya kudanganya watoto wa chekechea?

Kwa nini Malecela asitoe wazo hata nusu la kurekebisha huo mfumo mbaya anao uongelea wa watu wachache kumiliki mali za nyingi? Tatizo ni nini, Upepari? Malecela ana idea hata robo ya ku fix huu mfumo?

Usitake kufanyia usanii watu wote wakati wote bibie!

Ha ha haaaaaaaaaa!
 
To be honest, I find it really strange and utterly naive to dismiss Mama Kilango's point of view on the basis that he did not oppose the parliament's move to punish Zitto. People on this side of the debate are using a wrong premise and therefore their conclusion is definetely flawed.

Sanasana naona mnajaribu kuwagombanisha wabunge wetu "mahiri" kwa wananchi pasipo sababu za msingi. Kazi ya msingi ya mbunge ni kutetea wananchi na nchi yake pale serikali inapojaribu kwenda kinyume na majukumu yake ya msingi. Hivi ndivyo alivyofanya Zitto na ndivyo alivyofanya Mama Kilango na wabunge wengine kadhaa hivi karibuni. Sasa kwa nini tuhoji dhamira ya mama Kilango? Viongozi wa kisiasa wanapimwa kwa maneno na matendo yao; hatuwezi kuwapima kwa yale wanayoyafikiria maana kamwe hatuwezi kuyajua. Ningeelewa hoja hizi kama mama Kilango ali-flopflip. Yaani kama kuna wakati alitetea wizi wa EPA na sasa anapinga. Otherwise, tusije tukajikuta nasi tunaanza kuwashindanisha wabunge wetu kwa umaarufu. Huo utakuwa ni uhuni maana wanayoyafanya akina mama Kilango ndivyo wanavyopaswa kuwa wanafanya siku zote.

Tatizo ninaloliona mimi hapa ni kwamba hatujazoea viongozi wetu, wakiwemo wabunge, wakitekeleza wajibu wao kiasi kwamba siku wakifanya wajibu wao inakuwa taabu kiasi cha kuwa news na kuzaa threads na threads kwenye mitandao ya internet. Yaani viongozi wametufikisha mahala ambapo sasa tunaona kwamba kutekeleza wajibu wao imekuwa ni upendeleo kwa wananchi unaostahili tuzo na pongezi kemukemu. Katika hali ya kawaida hatupaswi kuwa tunajadili na kupongeza au kuhoji dhamira ya mbunge kuibana serikali bungeni maana kwa kweli hii ndio kazi yao. Kwa utaratibu huu itafika mahala wanafunzi watakuwa wanaandamana kumpongeza mwalimu wao kwa kukumbuka kuingia darasani kufundisha kipindi chake!

Mkuu Kitila,

Heshima mbele, yaani saafi sana na tuko ukurasa mmoja hapa! Yaani taifa mbele vyama na siasa nyuma!
 
I reserve my comments kuhusu jasho...:) Miye si mmoja wa akina Chagulaga, lakini nilidhani hili la jasho niko pekee yangu kumbe tuko wengi...:) samahani kwa kuchepuka nje ya mjadala.
 
Go go haki za wanawake Malecela juu, mwafrika wa kike juu hizi si zama za mawe ha ha
 
Hawezi zuiwa na mtu yoyote, kila m-Tanzania ana hakli ya kushirki siasa kwa kadri ya uwezo wake mradi havunji sheria, mwaka huu atalia mtu wallahi!
 
Nimeona kichefuchefu niliposoma kwamba Anna Abdallah amempiga kijembe Anna Kilango-Malechela. Atasemaje "sisi tusiojua kupayuka"? Yaani ni kwamba anasema somo wake "anapayuka"?

Aidha Anna Abdallah anataka tufiche wizi na wezi, au anamwonea wivu somo wake kwamba anavuma, au yote mawili. Kwa vyovyote vile, sisi hatutaki watu wanaovumbia macho wizi na wezi.

Hawa Anna wawili ni wake wa vizito. Mmoja Mke wa Waziri Mkuu na Makamu wa Mwenyekiti wa CCM wa zamani, na mwingine ni mke wa Makamu wa Mwenyekiti wa CCM wa sasa. Washirikiane.

Nirudi kwa wenzangu Joka Kuu na Mkandara: Namshukuru sana Joka Kuu kwa kutufahamisha kuhusu kuweko kwa Ripoti ya Kamati ya AYILA. Ni nani kiungo wa JF huko Dodoma ambaye ataweza kutupatia hiyo ripoti? Mwakilishi wetu jikoni, Field Marshal ES, utaweza kutusaidia hili?

Kwenye kitabu changu cha kumbukumbu nimeongeza yafuatavyo:
  1. Mwaka 1992 Taifa lilibiwa 216 bn/=. Wezi walikuwa viongozi wake. Hii habari inaaminika kwa sababu imetoka kwa Mke wa aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo.
  2. Mwaka 2005 taifa hilo hilo likaibiwa 133 bn/=. Wezi walikuwa pia ni viongozi waandamizi wa taifa.
  3. Gilman Rutihinda aliyekuwa Gavana wa BoT mwaka 1992 ni marehemu sasa. Ushahidi wake hauwezi kupatikana. Kigoma Malima aliyekuwa Waziri wa Fedha naye ni marehemu. Balali aliyekuwa Gavana wa BoT wakati zilipoibiwa 133 bn/= naye inasemekena ni marehemu, lakini hakuna ushahidi wa kutosha.
  4. Inasemekeana Gavana wa sasa wa BoT alikuwa mmoja wa Wakurugenzi wa BoT wakati wa wizi wa 1992. Ndugu huyo huyo alikuwa Naibu wa Gavana wa BoT wakati wa wizi wa 2005.
 
Zemarcopolo,
Hivi Mama Kilango kesha pewa fursa ipi ya kuongoza! jamani hivi kazi ya wabunge ni ipi kiasi kwamba mnataka kuona mabadiliko yanayopimika..Hivi kweli hoja za mbunge yeyote hazina uzito wa kupimwa hadi siku zitakapo fanya kazi?..
Duh basi hatuna haja kabisa ya kuwa na bunge maanake wapo kwa mamia na wote hulala usingizi, leo hawa wachache wanaowakilisha mawazo na matakwa ya wananchi wanaambiwa hawafai!.. Kazi kweli kweli!

Mkandara, je unajaribu kumaanisha kuwa Ubunge sio uongozi?Au kwako wewe uongozi ni urais tu? Unauliza mabadiliko gani tunataka kuona, jibu ni rahisi tu: mabadiliko yanayotakiwa ni yale yaliyoahidiwa wakati wa uchaguzi.

Wabunge ni legislators basi na mafanikio yao tuyapima kwa kuangalia idadi ya useful legislations wanazowezesha zipitishwe, sio kwa kuwa machachari wa kufokafoka.

Halafu sijui umetoa wapi hiyo nukuu ya mimi kusema kuwa mama Malecela hafai, maana hata mimi mwenyewe sikumbuki kuandika kitu kama hicho. Unaweza kunikumbusha lini na wapi nimesema mama Malecela hafai? Ninachokumbuka kuandika ni kwamba sitakaa nikimshabikia mwanasiasa ambaye ameshapewa nafasi ya uongozi iwapo atakuwa na maneno mazuri au matamu na mawazo "mazuri" yasiyoleta mabadiliko yanayopimika.

In this case mama Malecela tayari ni mbunge, hivyo basi nitamuona machachari na kuanzisha thread ya kumpa vote of confidence iwapo atasimama kidete kuhakikisha bajeti ya nchi inakidhi mahitaji ya walipa kodi, iwapo atahakikisha sera ya afya inawezesha kupunguza vifo vya watoto. iwapo atahakikisha wanafunzi wanawezeshwa kupata elimu ya ubora unahostahili, iwapo atahakikisha bunge linapitisha sheria ya kutokuvumilia wasaliti wa taifa etc. Sitaanzisha thread ya kumpa vote of confidence kwa sababu kafoka kuhusu EPA. Just to remind you kuna rafiki yangu alifoka sana kuhusu mikataba ya madini na aliahidi itabadilishwa mara moja, be informed that hakuna mkataba utakaobadilishwa in this phase government.

Mnataka nini kitokee ili mjifunze jinsi ya kudeal na wanasiasa?
 
Kama mume wako au mke wako ni mfisadi halafu unaenda kuhutubia watu kuhusu ufisadi ni umbeya. Huyu mama anatafuta umashuhuri tu ni mnafiki mkubwa. Mwafrika wa kike tofuta mtu mwingine kwenye harakati zako za mapinduzi lakini huo ndiyo ukweli mama kaoa fisadi.

Kwa hiyo kama wewe ni Padri au Sheikh usihubiri watu waache uzinzi kwa sabau mkeo/mumeo ni mzinzi? Watu wengine bwana...
 
Nyie watu mnanichekesha.... CHECK ur SUsceptibility to BUlshit and lear n to recognise real integrity and differentiate it from political acrobatics... JF amkeni.
 
Huyu Anna Abdalaah nayeye ana issue yake ambayo mpaka leo inasumbua wizara ya afya ila magazeti waga hawamtaji kuusika pampja na kuwa mchezo mchafu wa vifaa vya kupimia ukimwi ulianzia kwake, kwahiyo hawezi kuacha kutete mafisadi wezake wakati akijua kuwa na yake yako njiani.
 
Nimeona kichefuchefu niliposoma kwamba Anna Abdallah amempiga kijembe Anna Kilango-Malechela. Atasemaje "sisi tusiojua kupayuka"? Yaani ni kwamba anasema somo wake "anapayuka"?


Hawa wabunge wawili hawana uhusiano mzuri toka siku nyingi, Anna Abdallah ni mmoja wa viongozi walionufaika sana na utawala wa Mkapa, na ni mmoja wa viongozi ambao siku zote wamekuwa na tatizo na Makamu wa ccm mstaafu, ndiye aliyehusika na kumfanyia rafu Malecela kwenye ubunge wa mwaka 1985 akiwa RC Dodoma, kwa kushirikiana na hawara wake wa wakati ule Mzee Kawawa, baadaye mama Kilango akiwa mwenyekiti wa UWT Kinondoni alidhani kuwa huenda nia yake ni kugombea uenyekiti wa taifa ambao yeye alikuwa anautaka then, akampiga sana vijembe kule cc mpaka jina la mama Kilango likatolewa kugombea NEC na ubunge, na pia Anna Abdallah anaamini kuwa huenda Malecela alihusika na faulo ya mumewe kupigwa chini uSpika, sasa hivi kuna mkakati mkubwa na mzito wa kumchagua mama Kahama kuchukua nafasi hiyo ya mwenyekiti wa UWT,

Na besides ndio hasa maana ya Mkapa kuhudhuria hiki kikao cha NEC alishuariwa kuwa wafuasi wake wanashindwa kum-support kwa sababu yeye mwenyewe hayupo na kwamba akikosa hiki kikao atakuwa kwenye matatizo makubwa sana, ndio maana akaenda kule Dodoma, na kweli kuwepo kwake kumesaidia sana ndio maana sasa unaona kina Anna Abdalalh wameanza kusimama, lakini besides all this behind the scene ishus, bado ni haki ya kila mbunge kusema anachoamini ndani ya bunge,

Ni mwana siasa mjinga asiyekuwa na future ndiye anayeweza kuogopa mijadala inayomuhusu, kwa sababu ni mijadala kama hii ndio inampa nafasi ya kujiangalia kwa makini tena kwenye kioo, Mama Anna Abdallah hana future tena kwenye siasa kwa sababu umri umepita na hana hata huo uwezo wa siasa, yeye siku zote amekuwa na siasa za kubebwa na wakubwa, lakini Mama Kilango ndio kwanza nyota inawaka, bungeni ni mahali pa "kupayuka" sidhani kama ni mahali pa kusali kimya kimya, sasa Zitto angenyamaza kimyaaa tungejuaje kuwa kuna mikataba ya Buzwagi imesainiwa Hotelini London kwa siri?

Binafsi nimeiangalia kwa makini sana mijadala ya Mama Kilango, ikiwa ni pamoja na huu, kwa kweli nothing major au serious against, zaidi tu ya the usual cynics za online politics ambazo kwa kweli hazijawahi kuchagua au kutomchagua kiongozi yoyote wa siasa nchini kwetu, ingawa zinasaidia sana kuikosesha usingizi serikali na uozo wake, kwa sababu kama kweli tungekuwa na hiyo power as some of us wangependa tuamini, basi wabunge wa upinzani wangekuwa ni wengi sana kuliko tulionao sasa, maana tumekuwa hapa kwa muda mrefu sana lakini bado wabunge wa CCM wanapita kila siku,
Siasa za Tanzania sio za majuu, za kwetu ni slow na very rough lakini ni wananchi wachache sana wanaosoma mtandao, na hata wakisoma kuna ile hisia ya Afriacn Conservatism kuwa hawa vijana ni watoto wadogo,

Siasa za Tanzania zimeshabadilika, hazitakuja kuwa kama zamani tena sasa wananchi wameanza kuamka na hata viongozi wetu pia, kupayuka bungeni kuna faida na hasara zake, lakini so far tumejionea faida kwa sababu ndiko kulikomshinikiza Lowassaa na wenziwe kujiuzulu baada ya kupayukiwa sana na wabunge wengi, labda huko mbele ya safari kuna siku tutakuja kuona hasara zake, lakini nirudie tena kuwa binafsi ninaheshimu hii mijadala hasa inayomuhusu mama Kilango, kwa sababu pamoja na yote mengi yalioysemwa kisiasa mama hana tatizo kubwa au major zaidi tu ya kwamba amenunua maadui wengi sana wa mumewe, lakini naamini anafahamu hilo kuwa pia amenunua marafiki wengi pia wa mumwewe, so far anashitakiwa kwa sababu ya makosa ya kina Kasaka Njeru, na Mzindakaya, ambao wamekuwa wanasiasa hata yeye akiwa bado kuingia kwenye siasa,

Mimi ninarudia tena kuwa nina-support wabunge wafuatao tena blindley Zitto, Dr. Slaa, Mwakyembe, Sendeka, Mama Kilango, Seleli, na Manyanya, hawa wabunge mimi ninawashabikia mpaka kwenye mifupa yangu ya mwili kwa sababu ninaridhishwa na wanayoyafanya bungeni na ninaamini kuwa mbegu wanazopanda kwa taifa letu zitalisaidia sana hili taifa mbele ya safari, hakuna m-Tanzania yoyote yule anyeweza kuzuia riziki ya mwingine, siasa ni haki yetu wote wabongo na pia maoni nayo ni haki yetu wote wabongo tena kuwa na maoni toafuti, kama mama Kilango ana any ambitions za politics ana haki zote kama mbongo, na ni kwa any mbongo, tatizo letu kubwa bongo sasa hivi ni ufisadi, yaani viongozi mafisadi na mama sio fisadi, wala sio mwizi wa hela za umma, kiuongozi hawajahi kufanya makosa yoyote sasa ninaamini kuwa njia ni nyeupe, hizi challenge ni muhimu sana kwake kupambana nazo tena ni vizuri zikiwa zinatolewa sasa na mapema, ndio maana nimesema kuwa hii mijadala ni mizuri sana maana inaweza kumpa nafasi nzuri ya ku-adjust kama kuna a serious ishu, ingawa so far sijaziona, mimi ninam-support 100%, na ni haki ya kila m-Tanzania kutom-support pia,

kuhusu kuweko kwa Ripoti ya Kamati ya AYILA. Ni nani kiungo wa JF huko Dodoma ambaye ataweza kutupatia hiyo ripoti? Mwakilishi wetu jikoni, Field Marshal ES, utaweza kutusaidia hili?

Mkuu hii ripoti nadhani ilishawahi kuwekwa hapa JF huko nyuma wasiliana na Invisible.

Ahsante Wakuu!
 
Akizungumza na waandishi wa habari katika Hotel ya Travetaine, iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa kamati hiyo Mchungaji Christopher Mtikila alisema kauli ya Bi. Kilango kwamba kuna kikundi kidogo kimepora fedha za nchini, ni ushindi kwa walala hoi.

Mwanasiasa huyo, alisema wapinzani wameamua kumsifu Bi. Kilango kwa vile amevunja mwiko wa ukiritimba wa chama chake na kuweka mbele maslahi ya Watanzania pale aliposisitiza kwamba ni lazima waliopora fedha za EPA wazirejeshe.

``Kilango ni mbunge bora katika karne hii, anastahili kuungwa mkono na kila Mtanzania, ametoa somo kubwa kwa gharama ya kujitoa mhanga yeye binafsi,`` alisema.

Alisema ushujaa wa mbunge huyo, unaonyesha kwamba hivi sasa nchi inakaribia kukombolewa na wale walioshiriki kuipora na kuwafanya wananchi waishi kimaskini watakamatwa.

Mchungaji Mtikila, alisema ushujaa wa Bi. Anne unaashiria kwamba zama za kuwa na bunge lenye kuburuzwa na wanasiasa, kwa maslahi binafsi sasa zimefikia tamati.

Kwa mantiki hiyo, aliwataka Watanzania kumpuuza Anna Abdallah kwa vile hoja zake zinaonyesha kwamba ana fikra mgando na bado giza la chama kimoja limemjaa.

Aliwakumbusha wana CCM kwamba katika uchaguzi ujao, watakaoshinda ni wale ambao wameonyesha dhamira ya kuwapigania wananchi wanyonge, hata kama kwa kufanya hivyo wataonekana wanakwenda kinyume na vyama vyao.

``Kile tulichokipigania kwa miaka mingi, kwamba wananchi wawe na viongozi huru, wasiofungwa na tabaka lolote, sasa kinaanza kutimia, na Mungu alivyo mkubwa, wanaokianzisha ni CCM wenyewe.

Zama na ukiritimba zimepita tunamsifu Kilango kwa kulikomaza bunge na kulifanya liheshimike kwa wananchi,`` alisema.

Mchungaji Mtikila, alisema kauli ya Bi. Anna Abdallah kwamba mchango wa Bi. Kilango ulijaa mbembwe na upayukaji, zinakasirisha hasa ukizingatia kwamba wananchi wana uchungu na uporaji unaoendelea.

``Anna Abdallah wote tunamjua tabia yake, tunamuelewa alipotokea na aliyofanya, hatumshangai kwa vile kilichomfikisha pale sio elimu wala juhudi ya kazi ya mikono yake, ndio maana anamuonea wivu mwenzake,`` alisema.

Kuhusu hoja ya mbunge huyo kwamba kauli ya Bi. Kilango inaleta mgawanyiko, Mchungaji Mtikila alisema mwana mama huyo amejaa giza la ajabu kichwani pake, kiasi kwamba ameshindwa kuelewa kuwa lengo la kuwa na Bunge ni kutafuta mgawanyiko.

``Huo anaoita mgawanyiko, hasa ndilo kusudi la kuwa na bunge, ili watu wagawanyike katika fikra na mtazamo, wajadiliane kwa hoja, kisha lile jema lichukuliwe, baya liachwe. Bunge lisilo na mgawanyiko, hilo halikidhi haja kwa wakati huu tulio nao,`` alisema.

Wakati huo huo, Mchungaji Mtikila alisema Watanzania wanatakiwa kumpa nguvu Spika wa Bunge Bw. Samwel Sitta, ambaye hivi sasa kuna njama za kumuondoa kwenye wadhifa wake, kutokana na msimamo wake wa kuwa upande wa wananchi.

Alisema kuna Mbunge mmoja tajiri, ambaye hana asili ya `Tanganyika` ndiye anayeongoza vita dhidi ya Spika
.

Alionya kwamba Mbunge huyo pamoja na Rais mstaafu Bw. Benjamin Mkapa, pingu ziko njiani `zinasaka` mikono yao, kwa vile ndio chanzo cha ufisadi nchini.

Kwa kweli Waheshimiwa humu Jamvini
Mtikila hapa nimempa Big Up kwa kuuchokonoa ukweli na kumfumua huyu anna wa abdallah na RA.Naungana nanyi kuwa lazima tuwe na confidence na kilango regardless of her intent ambayo hatuijui ili mradi anayosema ndiyo kutmiza wajibu wake. Ni kweli kwamba ili utamke maneno yale ndani ya CCM unahitaji kuwa ngunguri,kiburi na usiyeogopa.Hayo walikuwa wanajaribu akina Tuntemeke sanga wakati huo, Jeremia Mulyambate, Kuwayawaya S.Kuwayawaya, na kina Mateo Qaresi kabla hawajapata uwaziri na wengine kuliacha bunge lakini sasa hivi?kwa kipindi cha miaka karibu 15 sasa tumeshuhudia bunge butu,lisilo na meno na hatimaye chama kushika patamuaah samahani "hatamu".
 
1. Huo anaoita mgawanyiko, hasa ndilo kusudi la kuwa na bunge, ili watu wagawanyike katika fikra na mtazamo, wajadiliane kwa hoja, kisha lile jema lichukuliwe, baya liachwe. Bunge lisilo na mgawanyiko, hilo halikidhi haja kwa wakati huu tulio nao,`` alisema.

2. Wakati huo huo, Mchungaji Mtikila alisema Watanzania wanatakiwa kumpa nguvu Spika wa Bunge Bw. Samwel Sitta, ambaye hivi sasa kuna njama za kumuondoa kwenye wadhifa wake, kutokana na msimamo wake wa kuwa upande wa wananchi.

3. Alisema kuna Mbunge mmoja tajiri, ambaye hana asili ya `Tanganyika` ndiye anayeongoza vita dhidi ya Spika. Alionya kwamba Mbunge huyo pamoja na Rais mstaafu Bw. Benjamin Mkapa, pingu ziko njiani `zinasaka` mikono yao, kwa vile ndio chanzo cha ufisadi nchini.

Very strong points!
 
ZE PASTOR mbona hajazungumzia uchawi?yeye ni mchunga kondoo na hivyo tulimtegemea atoe onyo la kiroho hapa,.................
 
Back
Top Bottom