A Parody of Presidential Eloquence - Kejeli ya Umahiri wa Rais katika Lugha

kwanza sasa hivi hayupo nchini, kama mna maswali waliulizeni waliopo nchini,......YEYE HAJUI
 
Nimecheka hadi nimechoka kwa kweli ni uandishi wa shairi ulotulia. Hongera mtunzi!
 
hii alileta mwanakijiji siku moja baada ya jk kuongea siku ile ya besidei ya chama...........
 
We Dada mbona hujamtaja Author? Mzee Mwanakijiji anaweza kukubana na issue ya copyrights hapo....
 
Kwanza sasa hivi sijui yuko wapi huko naye pia hajui! hajui hata kitu gani kilitokea ongo la Mboto wala hajui! na hata hajui kuwa yeye pia ni Dk! na kuna uwezekana pia hajui kuwa yeye ni President wa TZ! Loss of Self Identity!! because if you are unconscious then unfortunately that you will be losing your identity! heheheh!
 
Swali: Mheshimiwa Rais je unawajua wamiliki wa kampuni ya Dowans?


Jibu:
Nasema mimi sijui, ni kina nani sijui,
Wanatoka wapi sijui, walifikaje sijui,
Kama nawafahamu sijui, kama wananijua sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Mheshimiwa Rais, lakini waliingia nchini na kupata Mkataba wa Richmond na kuleta majenereta katika kutekeleza mpango wako wa kupunguza tatizo la umeme nchini kweli huwajui?


Jibu:
Nasema mimi sijui!, kwanini walikuja sijui,
Uhusiano wao siujui, Kama nao Richmond sijui,
Waliingia kwa lipi sijui, na walirithishana vipi sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini ulisema kuwa Richmond ni kampuni Hewa kama Kamati ya Mwakyembe ilivyoonesha na kudai, na ukatoa pongezi! Unawaeleza vipi Watanzania kuwa Taifa liko tayari kuheshimu mkataba wa kampuni ya kitapeli?


Jibu:
Nasema tena sijui!Kama kampuni hewa sijui,
Kama ni matapeli sijui, Kama walibebwa sijui,
Wahusika kina nani sijui, Mwakyembe alijuaje sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Tulikoanzia sijui, tumefika vipi sijui,
Nahusika vipi sijui, nimuulize nani sijui,
Niwaridhishe vipi sijui, nianzie wapi sijui!
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini Rostam Aziz ametajwa kuhusika kuanzia mwanzo wa sakata hili na yeye mwenye amekiri kuhusika na hili kwanini usimuulize ili ujue?


Jibu:


Nitamuanza vipi sijui, Rostam huyu sijui,
Kama mwingine sijui, anahusika vipi sijui
Nimuamini nani sijui, kama ni kweli sijui!
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini, inawezekana vipi usijue wakati una vyombo vingi vya usalama ambavyo vingeweza kukupata taarifa mbalimbali za kiinteligensia kama walivyoweza kuzipata kule Arusha na kuvunja maandamano ya Chadema? Kwanini hujapatiwa taarifa za kiinteligensia kuhusu Dowans?


Jibu:


Intelligensia mimi sijui, nani anipe sijui,
Kwanini wanipe sijui, nifanye nayo nini sijui,
Wasiponipa sijui, kama nadaganywa sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Nani awaagize sijui, kama nini mimi sijui,
Au makamu sijui, Waziri Mkuu sijui,
Wajitolee tu sijui, au ni Bunge mimi sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Sasa msimamo wako wewe binafsi kama Rais ni upi, Dowans walipwe au wasilipwe?


Jibu:


Msimamo gani sijui! Kama ninao sijui,
Nilikuwa nao sijui, nitakuwa nao sijui,
Kama walipwe sijui, na wasilipwe sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Wizara ilipe sijui, Au Tanesco sijui,
Au huko hazina sijui, au hapa Ikulu sijui,
Bunge litenge fedha sijui, au Mahakama sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Sasa mheshimiwa inaonekana hujui mambo mengi tu; kuna mambo mengine yoyote unayoyajua?


Jibu:
Kwanini masikini sijui, Kagoda ni nani sijui,
Meremeta nani sijui, Dipu Grini nani sijui,
Mbona elimu duni sijui, wanagomea nini sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Sijui mimi sijui, mengine mengi sijui,
Ya kilimo siyajui, ya Sayansi siyajui,
Mambo ya maji sijui, umeme ndiyo sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Kama napendwa sijui, kama nachukiwa sijui,
Nafurahiwa sijui, au nakejeliwa sijui,
Kama ninachekewa sijui, au nakebehiwa sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Mheshimiwa swali la mwisho; asante sana kwa kutupa nafasi hii na kwa hakika umetuelewesha na tumeelewa kuwa hujui mambo mengi sana. Labda uwaambie Watanzania, je wewe ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?


Jibu:


Sijui mimi sijui, ninarudia sijui,
Kama miye sijijui, mtajuaje sijui
Kama najua sijui, kama sijui sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!

SASA WANAJAMII TUNAFIKA KWELI NA TANZANIA YETU HII??




STOP PLAGIARISM!! Hii ni kazi ya Mwanakijiji, ni vema ukasema hivyo!


A Parody* of Presidential Eloquence – Kejeli ya Umahiri wa Majibu ya Rais
Na. M. M. Mwanakijjii

A Parody: (Dictionary.com)
–noun 1. a humorous or satirical imitation of a serious piece of literature or writing: his hilarious parody of Hamlet's soliloquy.

2. the genre of literary composition represented by such imitations.

3. a burlesque imitation of a musical composition.

4. any humorous, satirical, or burlesque imitation, as of a person, event, etc.

5. the use in the 16th century of borrowed material in a musical setting of the mass (parody Mass).

6. a poor or feeble imitation or semblance; travesty: His acting is a parody of his past greatness.





Swali: Mheshimiwa Rais je unawajua wamiliki wa kampuni ya Dowans?


Jibu:
Nasema mimi sijui, ni kina nani sijui,
Wanatoka wapi sijui, walifikaje sijui,
Kama nawafahamu sijui, kama wananijua sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Mheshimiwa Rais, lakini waliingia nchini na kupata Mkataba wa Richmond na kuleta majenereta katika kutekeleza mpango wako wa kupunguza tatizo la umeme nchini kweli huwajui?


Jibu:
Nasema mimi sijui!, kwanini walikuja sijui,
Uhusiano wao siujui, Kama nao Richmond sijui,
Waliingia kwa lipi sijui, na walirithishana vipi sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini ulisema kuwa Richmond ni kampuni Hewa kama Kamati ya Mwakyembe ilivyoonesha na kudai, na ukatoa pongezi! Unawaeleza vipi Watanzania kuwa Taifa liko tayari kuheshimu mkataba wa kampuni ya kitapeli?


Jibu:
Nasema tena sijui!Kama kampuni hewa sijui,
Kama ni matapeli sijui, Kama walibebwa sijui,
Wahusika kina nani sijui, Mwakyembe alijuaje sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!




Tulikoanzia sijui, tumefika vipi sijui,
Nahusika vipi sijui, nimuulize nani sijui,
Niwaridhishe vipi sijui, nianzie wapi sijui!
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini Rostam Aziz ametajwa kuhusika kuanzia mwanzo wa sakata hili na yeye mwenye amekiri kuhusika na hili kwanini usimuulize ili ujue?


Jibu:


Nitamuanza vipi sijui, Rostam huyu sijui,
Kama mwingine sijui, anahusika vipi sijui
Nimuamini nani sijui, kama ni kweli sijui!
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Lakini, inawezekana vipi usijue wakati una vyombo vingi vya usalama ambavyo vingeweza kukupata taarifa mbalimbali za kiinteligensia kama walivyoweza kuzipata kule Arusha na kuvunja maandamano ya Chadema? Kwanini hujapatiwa taarifa za kiinteligensia kuhusu Dowans?


Jibu:


Intelligensia mimi sijui, nani anipe sijui,
Kwanini wanipe sijui, nifanye nayo nini sijui,
Wasiponipa sijui, kama nadaganywa sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Nani awaagize sijui, kama nini mimi sijui,
Au makamu sijui, Waziri Mkuu sijui,
Wajitolee tu sijui, au ni Bunge mimi sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Sasa msimamo wako wewe binafsi kama Rais ni upi, Dowans walipwe au wasilipwe?


Jibu:


Msimamo gani sijui! Kama ninao sijui,
Nilikuwa nao sijui, nitakuwa nao sijui,
Kama walipwe sijui, na wasilipwe sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Wizara ilipe sijui, Au Tanesco sijui,
Au huko hazina sijui, au hapa Ikulu sijui,
Bunge litenge fedha sijui, au Mahakama sijui,
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Sasa mheshimiwa inaonekana hujui mambo mengi tu; kuna mambo mengine yoyote unayoyajua?


Jibu:
Kwanini masikini sijui, Kagoda ni nani sijui,
Meremeta nani sijui, Dipu Grini nani sijui,
Mbona elimu duni sijui, wanagomea nini sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Sijui mimi sijui, mengine mengi sijui,
Ya kilimo siyajui, ya Sayansi siyajui,
Mambo ya maji sijui, umeme ndiyo sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!




Kama napendwa sijui, kama nachukiwa sijui,
Nafurahiwa sijui, au nakejeliwa sijui,
Kama ninachekewa sijui, au nakebehiwa sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Swali: Mheshimiwa swali la mwisho; asante sana kwa kutupa nafasi hii na kwa hakika umetuelewesha na tumeelewa kuwa hujui mambo mengi sana. Labda uwaambie Watanzania, je wewe ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?


Jibu:


Sijui mimi sijui, ninarudia sijui,
Kama miye sijijui, mtajuaje sijui
Kama najua sijui, kama sijui sijui
Nasema mimi sijui, tena nasema sijui!


Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji -BGM)
 
Du, haya ni majibu au mashairi? People are very creative. But all in all, the answers depict the truth about mkwere.
 
STOP PLAGIARISM!! Hii ni kazi ya Mwanakijiji, ni vema ukasema hivyo!

Huenda yeye aliikuta kwenye blogu ya mtu mwingine aliyekopi hapa bila ku-acknowledge, halafu akachukua kopi ya hiyo kopi na kuirudisha hapa ilikoanzia kama vile ndiyo inaanza upya kwa mara ya kwanza. That is a serious academic misconduct, punishable by expulsion or by extended suspension.
 
Back
Top Bottom