A failed assassination plot against Dr. Ulimboka...

Inasikitisha sana
"Ndugu zangu,

Najaribu kutuliza mawazo ili angalau niweze kuwapa kidogo tulipofikia na tunakoelekea juu ya suala hili. Kwa kweli haivumiliki ukimwona ulimboka kwa jinsi alivyotendewa na hali aliyonayo; kwa wale wanaojua hali za kitabibu, "this is a very unstable condition that demands permanent watch 24/7".

Kwa taarifa tulizokusanya, ulimboka na mwenzake waliitwa na Afisa mmoja (Jina linahifadhiwa) ili kuzungumza mambo (fulani) na wakiwa wanaendelea na mazungumzo bila kuwa na mwelekeo wa muafaka, jamaa akawasiliana na watu (fulani) kwa simu. Ghafla wakajitokeza "ASKARI" wakawataka yule (Afisa) na Dr (aliyeongozana na Ulimboka) waendelee na shughuli zao na kuwambia "Tunamtaka huyu". Wakatumia nguvu, wakamburuta na kumtia kwenye gari jeusi na kuondoka naye wakidai wanampeleka Polisi.

Huku wakiwa wanamtesa, walimlazimisha mambo kadhaa (kwa sasa tusiyataje) wakaenda naye asikokujua, wakampiga sana kwa ngumi, mateke na magongo na wakati mwengine wakitumia Bunduki zao. Wakiwa wanampiga pia walikuwa wakisema kuwa amewatesa/wasumbua sana na kuwa anajifanya mjanja mbele ya (Srk) na hivyo wanamalizana naye; akapoteza fahamu...

Wakamtupa eneo la mapori huko Tegeta hadi alipookotwa na wananchi asubuhi na kukabidhiwa mikononi mwa Wanaharakati waliompeleka Hospitali Muhimbili.

Wakati akipokelewa MOI tayari baadhi ya wanaharakati walishafika eneo lile, kumbe kati ya walimpokea alikuwamo kijana anayesadikiwa kuwa ni "Askari". Huyu aligundulika baada ya mda mfupi akiwa amejificha chooni akiwasiliana kwa simu na watu aliokuwa akiwaambia " Hajafa. Bado anahema.... na maneno mengine yaliyoashiria kuwa waliofanya 'kazi' ile hawakukamilisha 'maagizo'. Vijana wakamfundisha adabu kwa hasira na kumkuta akiwa na Redio Call, ambayo baada ya muda mfupi Polisi FFU walifika na gari na vifaa vya vurugu wakiisaka ile Radio.


Nashindwa kuendelea....."
NB: Haya ni maelezo ya mwanaharakati Albanie Marcossy aliyehusika kumsaka kama nilivyoyanukuu Mabadiliko Group.
 
Nini tafsiri ya waziri mkuu kuwa liwalo na liwe? liwe kufanya unyama huu? Kauli hii nini tafsiri yake, Ni muhimu Pinda awajibe kwa hili, naninawaambia watanzania HUKUMU YA MWOVU IPO HAPAHAPA DUNIANI. Damu hii haiwezi potea Bure 2
 
kaka yangu ntatiro sijui ni kwa evidence gani jamani uwe macho na wewe yasije kukukuta tukaanza kusikitikia wawili ilihali huyu mmoja bado
 
Taarifa ulizozipata siyo sahihi. Alikuwa kwenye mjadala na madaktari wenzie wachache. Akaja akabebwa mzobemzobe na watu walijitambulisha kuwa ni polisi, wakapotea naye. Wenzie walienda kutoa taarifa polisi lakini kila walikoulizia waliambiwa polisi hawana taarifa ya tukio hilo. Akakutwa na wananchi alifajiri, wananchi wakatoa taarifa polisi.
Huyo Dr Ulimboka ni msanii,kwanza yeye si mtumishi wa serikali kinachomsukuma akomae ni nini?Awaachie madaktari ambao wako serikalini wadai,yeye amdai anayemfanyia kazi.
Pia inaonekana kuwa alipoitwa kwenye hayo mazungumzo ya 'KUYAMALIZA'alienda yeye na rafiki yake.Hilo suala la mgomo ni la madaktari wote nchi nzima ilikuwaje aende yeye na huyo rafiki yake??hili suala siyo la kirafiki ni la kikazi.HAO WANAPIGA SIASA WAPATE PESA KWA MGONGO WA WENGINE.Kwa hakika inavyoonekana ni mtu anayeweza kununuliwa na akawauza wenzake.NASISITIZA HAFAI NA NDIO MAANA NAPINGA MGOMO HUU INGAWA NA MIMI NIKO IDARA HIYO HIYO.
 
Hao ndiyo watanzania ni vigumu kujua yupi anatetea wanyonge anayedai au anayedaiwa
 
Hizi conclusion ndiO huwa zinachanganya sana,( Ukiuliza source = hakuna) mpaka sasa kuna conclusion zaidi ya 3, we know some people are very good in connecting dots but we should try to be analyitical on this matter,
 
Katika hili Mtatiro Naungana nawewe Haya ni mambo ya hatari yanafanywa bila hata akili, Tumwombe Mungu Sana asife, maana linaloweza likatokea linaweza likaondoa amani kabisa na watu watapoteza maisha
Julius Mtatiro
MICHEZO YA USALAMA WA
TAIFA ITALIINGIZA TAIFA HILI
KWENYE MACHAFUKO. NASEMA
WAZIWAZI KUWA
WALIOMCHUKUA DR. ULIMBOKA
NYUMBANI KWAKE NI USALAMA WA TAIFA NA IGP ANAWAJUA,
NA RAIS ANAJUA MCHEZO WOTE.
HII MIJIZI NA MIUAJI ISIDHANI
HATUNA AKILI TIMAMU.
IKUMBUKWE KUWA VYOMBO
VYOTE VYA ULINZI NA USALAMA VIKO CHINI YA RAIS
ALIYECHAGULIWA KWA TIKETI
YA CCM. KATIKA HILI CCM
HAWAKWEPI LAWAMA. NA
KAMA ILIVYOKUWA KWA
WAKOLONI "CREATING THEIR OWN DESTRUCTION" NA CCM
INAPITIA NJIA HIYOHIYO.
INAJICHIMBIA KABURI
WAZIWAZI.. ONYO TUNALOTAKA
WATAWALA WALIJUE NI KUWA
WANAHARAKATI
HATUTAKUBALI CCM IFE KWA
NJIA YA KUDHURU, KUTISHA NA
HATA KUUA WATU. MTINDO HUU UTATUFANYA TUCHUKUE
MAAMUZI MAGUMU MNO,
VYOMBO VYA DOLA VISIONE
TUMEKAA KIMYA, AMANI HII
NDANI YA TANZANIA
HAILINDWI NA USALAMA WA TAIFA UCHWARA WASIOJUA
NANI KALA HELA ZA EPA ILA
WANAJUA NANI ANAONGOZA
MADAI YA HAKI YA
WAFANYAKAZI WA SEKTA
FULANI. DR ULIMBOKA NA WADAU WOTE
TUSIKATE TAMAA, MAPAMBANO
YA KUITENGEZA TANZANIA YA
WANANCHI NA SIYO YA
VIONGOZI NA WAHUNI
WACHACHE NDIO UNASHIKA KASI. TUNAFUATILIA UVUNJAJI HUU
WA HAKI KWA UKARIBU SANA. JULIUS MTATIRO,
0717 536 759.
 
Busara itumike zaidi. tutawale hisia zaidi. Mungu alitupa macho mawili, masikio mawili na mdomo mmoja, ili tuone mengi, tusikie mengi na tuseme machache.
"Mungu ibariki Tanganyika, Mungu ibariki Zanzibari, rip Tanzania"
 
Kumtesa Dr Ulimboka hakuwezi kumaliza mgogoro wa Madaktari. Hii ni ishara ya ukosefu wa Think tank persons ndani ya serikali na CCM. Poor Tz Government...
 
Back
Top Bottom