sitakuwafisadi
Member
- Jan 23, 2011
- 62
- 13
Ng'anza leo imefunika kila kitu... Wana mwanza wamesema wanaka kuingia mtaani kama Libya
Mkuu uyasemayo ni ya kweli kabisaHakika kwa mtawala makini akiona mabango haya na aina ya watu walioyabeba hatapata usingizi kama anataka chama chake kitawale milele kama wanavyojidanganya. Hii inaashiria kuwa kuna kimbunga cha vijana kinakuja kufuta uchafu wa ufisadi, watu wamechoka na hii si dalili nzuri kwa wate yaani viongozi, middle class na walalahoi. Ni wakati wa kuacha kufanya biashara binafsi sasa na kufanya biashara ya umma. Vinginevyo 2015 ni mbali sana ninavyoona, kama yanayoendelea sasa hayatapatiwa ufumbuzi.
Ni jambo la kusikitisha pale kiongozi wa nchi anapokuja kutamka waziwazi kuwa kupanda kwa umeme ni maamuzi ya kibiashara siyo ya kisiasa, ina maana mtumiaji leo hii hana mtetezi kwa kuwa hachangii mamilioni ya kampeni za CCM?. Freedom is coming tomorrow, na kuanzia sasa kuzuia maandamano ya wananchi ni kama vile kuzuia mvua isinyeshe wakati ni masika. Watawala wasome alama za nyakati. Ningekuwa ni mimi ningeanzia na kumtaka spika wa bunge aruhusu mijadala bungeni vinginevyo atakuwa amewapatia CDM kibali cha kupeleka bunge kwa wananchi kwa njia ya maandamano.