Dini ni mawazo ya wanadamu ya namna ya kumtafuta Mungu. Yesu hakuja kuhubiri mawazo ya wanadamu bali alihubiri wokovu na msamaha wa dhambi. Yesu hakuja kuanzisha dini bali alileta msamaha wa dhambi duniani. Hicho ndicho mimi ninachohubiri, wokovu na msamaha wa dhambi tulioletewa ba Bwana Yesu...
Narudia tena, Yesu Kristo pekee ndiye mpatanishi kati mwanadamu na Mungu, tena ndiye anayetuombea kwa Baba. Acheni utapeli wa kuwafanya watu watoe sadaka ya ukombozi, huo ni wizi.
Pole sana, kwa hiyo wewe unazini kwa sababu una mtumishi wa kukuombea na unatoa sadaka ya ukombozi!
Mimi nimeokoka, huo ujinga uko mbali nami. Ninawafundisha watu njia ya kweli, ambayo ni Yesu Kristo.
Acha kuwadanganya watu, eti watoe sadaka ya ukombozi wakati Yesu alishatoa uhai wake kwa ajili yao.
Siamini kabisa katika hilo. Ninachokiamini ni kwamba, mpatanishi kati ya mwanadamu na Mungu ni Yesu tu. Leo hatuhitaji mpatanishi mwingine zaidi ya Yesu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.