Jumong S
JF-Expert Member
- Jul 3, 2013
- 7,427
- 10,749
Habari,
ANC ni chama kikongwe na kinachoaminika kuwa na hadhi ya juu kiana harakati pengine kuliko vyama vingi sana Africa. Chama hiki kinapendwa nje na ndani ya South Africa kwa sababu ya sera zake na mfumo imara ulioachwa na Nelson Mandera. Ni chama kilichowatetea wanyonge na kufanikiwa pakubwa sababu ya umahili wa watangulizi na watu makini waliopata kuwepo na waliopo. Kwa wakati huu huwezi kukitaja chama hiki bila kumtaja Julius Malema, mwanasiasa kijana na machachari aliyekuwa na uthubutu wa kuwakoromea hata wakubwa wake pindi walipoenda ndivyo sivyo, kwa bahati mbaya mkubwa hakosei na alitimuliwa chamani kwa taratibu kama zilizochukuliwa kwa Zito kabwe. Alianza kuvuliwa uongozi wote, then alitimuliwa moja kwa moja.
Zitto Kabwe kwa wengi alionekana ni dira hasa ya vijana. Amefanya mengi makubwa na amefanikiwa kuwa na ushawishi mkubwa wa vijana wengi kuingia CHADEMA. Nawakumbuka vijana kama Mbunge Moses Machali na Mkosamali, ni baadhi tu ya vijana waliopikwa kwa siasa kali za ZZK. Amejitahidi kuwa mwana harakati wa kupambana na ufisadi papa (na wananchi wengi wamejua wizi wa nchi hii kupitia ZZK) na mbunge mwenye uthubutu lakini leo hii ameishia kuvuliwa madaraka!Sehemu nyingi ukimtaja mbunge huyu alijipatia sifa hata kwa watoto wadogo.
Ni hakika kwamba alikuwa amebeba kura nyingi za CDM na kuna hatari akaondoka nazo kwa wananchi wengi kutoipigia kura CDM (hasa wale wanaochagua chama). Wanaoshabikia kutimuliwa kwake si wengi kama wanaoona kaonewa kama ilivyotokea kwa Malema. Malema bado yupo na hachoki kuitetea nia yake ya ndani.
USHAURI WANGU
Mh Zitto, siasa unayofanya, mwenye kuujua ukweli halisi ni wewe na Mungu wako. Tuhuma zote unazopata sasa unajua zipi ni sahihi na zipi zinatolewa kwa uongo. Nchi hii inahitaji ukombozi halisi zaidi na si chama. Pale ulipokosea pasahihishe na pale unapopatia usikate tamaa. Uliaminika na bado kuna kundi kubwa linauamini utendaji wako. Simama tena na songa mbele kuikomboa Tanzania.
Kumbuka: Mwisho wa siku utaulizwa umeifanyia nini Tanzania na si CHADEMA.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
ANC ni chama kikongwe na kinachoaminika kuwa na hadhi ya juu kiana harakati pengine kuliko vyama vingi sana Africa. Chama hiki kinapendwa nje na ndani ya South Africa kwa sababu ya sera zake na mfumo imara ulioachwa na Nelson Mandera. Ni chama kilichowatetea wanyonge na kufanikiwa pakubwa sababu ya umahili wa watangulizi na watu makini waliopata kuwepo na waliopo. Kwa wakati huu huwezi kukitaja chama hiki bila kumtaja Julius Malema, mwanasiasa kijana na machachari aliyekuwa na uthubutu wa kuwakoromea hata wakubwa wake pindi walipoenda ndivyo sivyo, kwa bahati mbaya mkubwa hakosei na alitimuliwa chamani kwa taratibu kama zilizochukuliwa kwa Zito kabwe. Alianza kuvuliwa uongozi wote, then alitimuliwa moja kwa moja.
Zitto Kabwe kwa wengi alionekana ni dira hasa ya vijana. Amefanya mengi makubwa na amefanikiwa kuwa na ushawishi mkubwa wa vijana wengi kuingia CHADEMA. Nawakumbuka vijana kama Mbunge Moses Machali na Mkosamali, ni baadhi tu ya vijana waliopikwa kwa siasa kali za ZZK. Amejitahidi kuwa mwana harakati wa kupambana na ufisadi papa (na wananchi wengi wamejua wizi wa nchi hii kupitia ZZK) na mbunge mwenye uthubutu lakini leo hii ameishia kuvuliwa madaraka!Sehemu nyingi ukimtaja mbunge huyu alijipatia sifa hata kwa watoto wadogo.
Ni hakika kwamba alikuwa amebeba kura nyingi za CDM na kuna hatari akaondoka nazo kwa wananchi wengi kutoipigia kura CDM (hasa wale wanaochagua chama). Wanaoshabikia kutimuliwa kwake si wengi kama wanaoona kaonewa kama ilivyotokea kwa Malema. Malema bado yupo na hachoki kuitetea nia yake ya ndani.
USHAURI WANGU
Mh Zitto, siasa unayofanya, mwenye kuujua ukweli halisi ni wewe na Mungu wako. Tuhuma zote unazopata sasa unajua zipi ni sahihi na zipi zinatolewa kwa uongo. Nchi hii inahitaji ukombozi halisi zaidi na si chama. Pale ulipokosea pasahihishe na pale unapopatia usikate tamaa. Uliaminika na bado kuna kundi kubwa linauamini utendaji wako. Simama tena na songa mbele kuikomboa Tanzania.
Kumbuka: Mwisho wa siku utaulizwa umeifanyia nini Tanzania na si CHADEMA.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums