Zanzibar: Sukari ni Tshs 1,500/- kwa Kilo

Baraghash

JF-Expert Member
Dec 18, 2012
2,713
1,790
Inahuzunisha, wakati juzi tu tulisheherekea miaka 52 ya muungano wetu, mshirika mmoja wa muungano anawauzia wananchi wake bidhaa adimu na adhimu ya sukari kwa bei nafuu kwa vitendo na mwengine anauza bei rahisi kinadharia.

Serikali zote mbili zinaongozwa na CCM na zina sera sawa kuhusu kulinda viwanda vya ndani. Zanzibar wana kiwanda kimoja cha Sukari wakati mshirika wake ana viwanda kadhaa vya sukari.

Kwa kujali wananchi wake SMZ wameona kwanza walinde hali, maslkahi na mahitaji ya wananchi walio wengi kwanza na hivyo kuhakikisha kila mahitaji muhimu yanapatikana kwa bei nafuu inayomudiwa na wananchi wake.

Jana nilikuta zogo karibu na maduka ya rejareja hapa Zanzibar watu wakilumbana. Eti, wanabishiana aina gani ya sukari kati ya "Brown Sugar na White Sugar" yenye ladha tamu zaidi

Kumbe kweli kipato kina jeuri! Ushauri, tufanye serikali moja na Makao Makuu ya Serikal ya muungano yawe Zanzibar na yale SMZ yahamishiwe Pemba. Uhaba wa bidha adimu na muhimu wa kila mara utakua historia!
 
Uchumi wa Zanzibar ni mdogo sana! Hata Mkoa wa Arusha wanaizidi Zanzibar kukusanya mapato!

Ndo maana hata hawana uwezo kuchangia huu Muungano!

Sasa sukari ikiwa 3,000 kama bara je wataweza?
 
swala la viwanda na biashara sio swala la muungano hivo kujaribu kuingiza zanzibar katika sakata la sukari ni uvivu tuu wa kufikiri na ufinyu wa uelewa wa mambo ya muungano na yasiyo ya muungano
 
Zanzibar yote ukipiga mluzi wananchi wanakusanyika kwa jinsi ilivyokuwa ndogo, tani moja ya sukari inawatosha kwa mwezi mzima.
Usitukane wakunga na uzazi ungalipo. Wanayoilisha bara kibidhaa hasa kutoka nje ya nchi ikiwemo hiyo sukari ni wazanzibari. Hata hivi sasa hatma ya kusambaa sukari bara imo mikononi mwa wazanzibari! Tafakari na uchukue hatua.
 
swala la viwanda na biashara sio swala la muungano hivo kujaribu kuingiza zanzibar katika sakata la sukari ni uvivu tuu wa kufikiri na ufinyu wa uelewa wa mambo ya muungano na yasiyo ya muungano
Hayo unayajua sasa? mbona husemi Michezo sio jambo lka muungano lakini TFF inaikwalisha Jamhuri ya muungano huko FIFA na kuiacha Zanzibar nje? Ni weledi wa kuelewa mambo!
 
Hayo unayajua sasa? mbona husemi Michezo sio jambo lka muungano lakini TFF inaikwalisha Jamhuri ya muungano huko FIFA na kuiacha Zanzibar nje? Ni weledi wa kuelewa mambo!
ungeleta mada ya TFF na FIFA na Zanzibar ningekujibu accordingly! hapa tunajadili nafasi ya zanzibar kwenye sakata la upungufu wa sukari nchini full stop! be consistent and concentrate on the thread which you have established yourself!dont lose focus!
 
Inahuzunisha, wakati juzi tu tulisheherekea miaka 52 ya muungano wetu, mshirika mmoja wa muungano anawauzia wananchi wake bidhaa adimu na adhimu ya sukari kwa bei nafuu kwa vitendo na mwengine anauza bei rahisi kinadharia.

Serikali zote mbili zinaongozwa na CCM na zina sera sawa kuhusu kulinda viwanda vya ndani. Zanzibar wana kiwanda kimoja cha Sukari wakati mshirika wake ana viwanda kadhaa vya sukari.

Kwa kujali wananchi wake SMZ wameona kwanza walinde hali, maslkahi na mahitaji ya wananchi walio wengi kwanza na hivyo kuhakikisha kila mahitaji muhimu yanapatikana kwa bei nafuu inayomudiwa na wananchi wake.

Jana nilikuta zogo karibu na maduka ya rejareja hapa Zanzibar watu wakilumbana. Eti, wanabishiana aina gani ya sukari kati ya "Brown Sugar na White Sugar" yenye ladha tamu zaidi

Kumbe kweli kipato kina jeuri! Ushauri, tufanye serikali moja na Makao Makuu ya Serikal ya muungano yawe Zanzibar na yale SMZ yahamishiwe Pemba. Uhaba wa bidha adimu na muhimu wa kila mara utakua historia!
Watu wenyewe wapo laki 8,zanzibar ukishindwa kuongoza hata kwa mungu hufiki kam sefu anavyoshindwa kuongoza
 
Inahuzunisha, wakati juzi tu tulisheherekea miaka 52 ya muungano wetu, mshirika mmoja wa muungano anawauzia wananchi wake bidhaa adimu na adhimu ya sukari kwa bei nafuu kwa vitendo na mwengine anauza bei rahisi kinadharia.

Serikali zote mbili zinaongozwa na CCM na zina sera sawa kuhusu kulinda viwanda vya ndani. Zanzibar wana kiwanda kimoja cha Sukari wakati mshirika wake ana viwanda kadhaa vya sukari.

Kwa kujali wananchi wake SMZ wameona kwanza walinde hali, maslkahi na mahitaji ya wananchi walio wengi kwanza na hivyo kuhakikisha kila mahitaji muhimu yanapatikana kwa bei nafuu inayomudiwa na wananchi wake.

Jana nilikuta zogo karibu na maduka ya rejareja hapa Zanzibar watu wakilumbana. Eti, wanabishiana aina gani ya sukari kati ya "Brown Sugar na White Sugar" yenye ladha tamu zaidi

Kumbe kweli kipato kina jeuri! Ushauri, tufanye serikali moja na Makao Makuu ya Serikal ya muungano yawe Zanzibar na yale SMZ yahamishiwe Pemba. Uhaba wa bidha adimu na muhimu wa kila mara utakua historia!

Baraghash umeeleza vizuri ila nianze kwa majibu kuwa sukari brown inayotengenezwa na viwanda vyetu hapa nchini ni tamu na bora zaidi kuliko nyeupe zitokazo nje.Mawazo yako ya serikali moja na makao makuu ya serikali hiyo yawe Zanzibar na yaliyoko Zanzibar yahamishiwe Pemba kwamba uamuzi huo ndio suluhu ya uhaba wa bidhaa sukari bara wasubiri waliokuelewa waendelee kuchangia.Sijakuelewa na pia sijui uliwaza nini au kuamkia wapi.
 
ungeleta mada ya TFF na FIFA na Zanzibar ningekujibu accordingly! hapa tunajadili nafasi ya zanzibar kwenye sakata la upungufu wa sukari nchini full stop! be consistent and concentrate on the thread which you have established yourself!dont lose focus!
Pole, inaonekana umechomwa na kukugusa ndipo, mpaka na lugha ukabadilisha! Inachekesha lakini inafurahisha mtu alietaka kuhalalisha hoja yake kuingiza masuala ya muungano na akapewa mfano wa jambo la muungano, kaghadhibika kama mbogo, nifanye nini ?ni kusema tu,pole!
 
Zanzibar asilimia kubwa ni waislamu hivyo hawauzi bidhaa kwa kutafuta faida kubwa kama ilivyo kwenye mabenki ya kiislam hawataki riba.
 
Watu wenyewe wapo laki 8,zanzibar ukishindwa kuongoza hata kwa mungu hufiki kam sefu anavyoshindwa kuongoza
Ni kweli, watu wenyewe kidogo, lakini mambo yao ........ mpaka kukaja na fumbo maarufu, lisemalo: "When you play the flute in Zanzibar all Africa dances."
 
Ndo maana hata hawana uwezo kuchangia huu Muungano!
Hatuwezi kuchangia shughuli za muungano zisioeleweka, kumbuka mambo mangapi ya muungano tulioungana 1964, na mkayaongeza kinyemela mpaka sijui mangapi (20), unatufanya sisi mazuzu tukulipeni mambo ambayo hatujakubaliana na hatufaidiki. Nakwambia nadhani ulikuwa hujui, maisha na hali ya mtu mmoja mmoja huwezi kulinganisha ya kwenu na ya Zanzibar. Hayo makusanyo makubwa unayoyapata yagawanye na watu huo wa mkoa wako, halafu yachukue hayo mapato machache ya Zanzibar, yagawanye na watu wa Zanzibar, ndio utajua Zanzibar kiuchumi iko juu. Bye the way, who is your last headmistress?
 
Hivi visiwa vitatawaliwa na Bara kwa nguvu Wazanzibari watake wasitake!

Visiwa vyote duniani vilivyo karibu na mataifa makubwa hutawaliwa na mataifa hayo!

Mambo ya demokrasia, kura n.k sii msingi katka visiwa hivi!
Angalia Taiwani kwa China!

Muungano ni geresha tu!

Viongozi wa visiwa hivi ni lazima wateuliwe na Watu wa bara na watii mamlaka ya bara!

Habari ndo hiyo!


Hatuwezi kuchangia shughuli za muungano zisioeleweka, kumbuka mambo mangapi ya muungano tulioungana 1964, na mkayaongeza kinyemela mpaka sijui mangapi (20), unatufanya sisi mazuzu tukulipeni mambo ambayo hatujakubaliana na hatufaidiki. Nakwambia nadhani ulikuwa hujui, maisha na hali ya mtu mmoja mmoja huwezi kulinganisha ya kwenu na ya Zanzibar. Hayo makusanyo makubwa unayoyapata yagawanye na watu huo wa mkoa wako, halafu yachukue hayo mapato machache ya Zanzibar, yagawanye na watu wa Zanzibar, ndio utajua Zanzibar kiuchumi iko juu. Bye the way, who is your last headmistress?
 
Zanzibar asilimia kubwa ni waislamu hivyo hawauzi bidhaa kwa kutafuta faida kubwa kama ilivyo kwenye mabenki ya kiislam hawataki riba.
Hivi wa bara walioficha sukari kule mbagala sijui wapi si waislamu wale au?
 
Back
Top Bottom