Loliondo, Mvomero, Kiteto, sasa Monduli
Hofuimetanda katika baadhi ya watu wa kata ya sepeko wilayani Monduli. Hakunaanayejua nini kitatokea. Wala hakuna anayejua ataenda wapi. Hii ni baada yakuambiwa sehemu mnayoishi ni mali asili na saa yoyote mnaweza kupewa notice. Sasawamekua na mgogoro katika nafsi zao, baina yao, na viongozi, na serikali.
Mgogoro hutokea pale pande mbili au zaidi yambili ikihasimiana ikiwa kila upande inafikiri ndo yupo sahihi. Kila upande ikihisihaki yake inapokonywa. Kushindana katika hali kama hii mgogoro hutokea. Naisipopata mwafaka mapigano ya umwagaji damu yaweza kutokea.
Nchiyetu tofauti kama hizi yamekua mengi sana. Migogoro haya yamekua yakihusianishakutofautiana kwenye rasilimali hasa ya ardhi. Migogoro haya yamekua yakitokeabaina ya watu binafisi, jamii Fulani na jamii nyingine ambayo mara nyingiwakulima na wafugaji au jamii Fulani na serikali au mwekezaji. Chanzo yamigogoro haya yamekua ikisababishwa kugombania mipaka au mara nyingine eneozima bila kujali mpaka ikiwa kila upande inahisi ana haki ya kumiliki.
Mifanoni mingi tu, Loliondo wameingiakwenye mgogoro mzito sana na mwekezaji ambaye alikua natetewa na serikali. Watuwalipoteza maisha baada ya kuuwawa na asikari wanaomtii mwekezaji na wenginekupoteza mali kwani maboma yao yalichomwa moto. Na hata kupoteza mifugo yaowakati wa mgogoro.
Mfanomwingine ni ya Kilosa na Kitetoambayo hawa wamefanana. Migogoro yao imetokea baina ya wakulima na wafugaji. Nahapa wengi wamepoteza maisha na mali. Kila mmoja anadai ndo mwenye haki katikasehemu tajwa.
Nihivi majuzi tu wananchi wa sehemu ya Monduli katika kata ya sepeko wameingia katika mgogoro ambao hawajawahikuifikiria. Wamejikuta wakiambiwa sehemu mnayoishi na kufanyia shughuli zenusiyo mali yenu. Ni sehemu ya hifadhi (mali asili). Hawa wananchi wakapigwa nabutwaa.
Taarifawanazozipata ni kwamba kuna siku mnatangaziwa notice ya kuondoka. Khaaa!,wanauliza tumeishi hapa sasa kwa zaidi ya miaka 40. Wanaambiwa Serikalihaitambi hilo ni kwamba sheria ya mwaka 1974 inaosha hili ni sehemu ya maliasili. Zaidi wakaambiwa ukubwa wa eneo unaohitajika ni ekari hekta 3,600.Katika eneo tajwa, wananchi maelfu wanaishi ndani yake.
Hawawananchi wanapewa notice bila kupewa sehemu mbadala ya kwenda. Hawa wananchiwameishi hapo kwa miaka 40. Kuna watu wamezaliwa hapo na kuzeeka hapo. Hawajuipa kwenda, cha kufanya hata pa kujitetea hamna.
Ndiyosheria zipo lakini wenye kutekeleza hizi sheria walikuwa wapi kwa miaka 40sasa, hawa wananchi waligawiwa maeneo husika na serikali zao za vijiji. Uongoziwa hizi vijiji ni halali kabisa na walikua wanawasiliana na serikali yahalimashari ya wilaya.
Sasaeti leo baraza la madiwani wamepitisha azimio, kwamba hawa wananchi wapo kwenyehifadhi. Hawa wapiga kura wenu waendewapi? Kweli tunasikia kuna fidia, ni ya kuifanyia nini?Mtuanapoishi kwa miaka 40 sasa anayo mashamba, makazi ya kudumu na rasilimalimengine mengi yasiyo hamishika. Ghafula bin fuu unamwambia tunakupa notice yakuondoka. Hakuna makubaliano ya kueleweshana ya nini kifanyike. Bali nikuambiwanotice inatolewa.
Kwahali kama hii, kwa usumbufu kama huu, mgogoro utaepukikaje? Hawa watu nimchanganyiko wa wakulima na wafugaji. Kuna watu wana mashamba makubwa sana.Afadhali ya wafugaji wanaweza kuhama na mifugo yao. Je wakulima kama mtu alikuwana zaidi ye ekari 50 atapata wapi huko anakohamishiwa au anakohamia aridhi kubwakiwango hiyo ambayo ni tayari kwa kulima.
Nahisiserikali inatengeneza mgogoro kama wa Loliondomaana inasemekana kuna mwekezaji. Bila kujali madhara itakayotokea kwa wananchina hata usumbufu watakao pata wao kama serikali.
karibuni kwa mjadala!!!
ahsanteni