Yaliyojiri mkutano wa CHADEMA Kigoma

Mpangawangu

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2014
Posts
887
Reaction score
965
Jahazi la chadema limezidi kuzama,hii ni baada ya wananchi wa kigoma kusisitiza msimamo wao wa kuikataa chadema. Haya ndiyo yaliyojiri mkutano wa leo.

Benson Kigaila azomewa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mwanga center kigoma mjini baada ya kusema Zitto Kabwe alipewa hoja ya Bunzwagi na sekratarieti ya CDM na kwamba hoja wanazotoa wabunge wa CDM bungeni si zao ni za chama watu wa Kigoma wamepata mshituko mkubwa Kigaila aliposema CDM makao makuu huwa inateuwa viongozi toka Kigoma kwa kuwasaidia na kwa upendeleo maalumu kwani wanakuwa hawana sifa na vigezo akatolea mfano Dr.Kaborou,Zitto,Shaban Mambo na Sabrina Sungura na akaeleza sababu ya kupendelewa kasema ni kura ambazo chadema hupata Kigoma kwenye chaguzi mbalimbali nchini alipozungumza kauli hiyo ndiyo zomeazomea ikazidi.

Na leo ndio ametangaza timu mpya aliyoisimika Kigoma kwenye mkutano huo wa hadhara na kuacha majonzi mjini Kigoma baada ya
kuwa viongozi wote walioteuliwa hawakubaliki kabisa na Watu wa Kigoma.

Na watu wa Kigoma wakaanza kuzomea tena na huku wakisema watu hao hawana uwezo wa kuvaa viatu vya Alhaji Kasisiko,Shabaani Mambo na Msafiri Wamalwa. Ni majonzi makubwa Kigaila Leo Kigoma.

Watu wa Kigoma wameomba viongozi wa ACT-Tanzania waende na kadi za kutosha kwenye mkutano wa hadhara utakaofanyika kesho Ujiji "Cine Atlas" na gari linalotangaza huo mkutano mjini Kigoma linashangiliwa sana kila eneo linakopita.
 
kigailla asije akasahau ile fomu fake ya mbowe.Mbowe anaisubir kwa hamu ufipa
 
Vipi mchina wako hana kakamera utupie kapicha au ushabiki
 
KIFO cha CDM kinatokana na tamaa na uchu wa madaraka wa Wachaga na Waarusha. Wanadai hicho ni chama chao kama alivyokianzisha Mchaga Mtei. Mungu akilaze mahala pema peponi. Wana Kigoma sasa tumeamka, tutawamaliza!
 
... Hakuna Ukweli Wowote Hapo, Mimi Mbna Niko Kgm Na Cjaona Hayo Unayoyasema
 
Mara viongozi waliochaguliwa hawakubaliki,hawana uwezo.
Mlitaka makamanda wasimike vibaraka sio ?
 

peleka upumbavu huu ka wapumbavu wenzio
 
Huyu ni kati ya wale kura hazikutosha tusimlaumu bali tumpe nafasi atume salamu hata kwa watu watatu tu
anza na Yuda na wengine ...
 
Huyu ni kati ya wale kura hazikutosha tusimlaumu bali tumpe nafasi atume salamu hata kwa watu watatu tu
anza na Yuda na wengine ...

Weka pichaF jinsi walivyokuwa wakizomea mbea wewe kama c changu
 

Weka picha hapa punguza kuweweseka,na itakuwa unaumwa ugonjwa unaoitwa kitaalam chademaphobia huu ni ugonjwa mbaya uliwahi kumpata Wassira,Lukuvi,Presidaa.Huu ugonjwa ukikupata unakusababishia upungufu wa akili kichwani(UPAKI) Nakushauri tafuta tiba mapema kabla hujazidi kuharibika kichwani.
 
Duuuh ccm kumbe ina vibaraka hadi jf

mimi si mwanasiasa ila uongo aliotunga huyu jamaa hauingii akilini hata chembe hata kama mtu hajui siasa hawezi kutoa hotuba kama hiyo

Tatizo hii project imeajili watu wengi mno na wengine hawajitambui
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…