Yaaa Ilahi

Yaaa Ilahi

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
1,041
Reaction score
1,294
Yaaa Ilahi

Mola wangu nibariki
Niongezee ridhiki
Unitoe kwenye dhiki

Si wa moja wala mbili
Kama vile pilipili
Naomba nipe kibali

Siitafuti huruma
Hata nikiwa kiguma
Ningali najisukuma

Na wala sitaogopa
Halafu sitaongopa
Nitayagawa makopa

Miye si mtu dhaifu
Baidi na isirafu
Sinao ubabaifu

Kupata ni majaliwa
Wala sijabaguliwa
Kesho nitainuliwa

Abuuabdillah
0744883353
 
well done! jaribu kufanya maboresho hapo kwenye 'si mtu dhaifu' weka 'ni mtu dhaifu' ili ipendeze zaidi. nasema hivyo kwasababu hiki ulichoandika kipo katika mfumo wa dua; na taratibu za kuomba dua ni kukiri makosa na mapungufu yote tuliyonayo wanadamu, kumsifu mola kwa sifa nzuri nzuri zote za ukamilifu pamoja na kumwomba mola atujaalie mambo mema mbalimbali
 

Nyingine hii kenge imeandika
 
Yaaa Ilahi

Mola wangu nibariki
Niongezee ridhiki
Unitoe kwenye dhiki

Si wa moja wala mbili
Kama vile pilipili
Naomba nipe kibali

Siitafuti huruma
Hata nikiwa kiguma
Ningali najisukuma

Na wala sitaogopa
Halafu sitaongopa
Nitayagawa makopa

Miye si mtu dhaifu
Baidi na isirafu
Sinao ubabaifu

Kupata ni majaliwa
Wala sijabaguliwa
Kesho nitainuliwa

Abuuabdillah
0744883353
Mashallah mungu akuhifadhi ww na kalam yako akupe tahshifa ya tunu ilonayo iliyotukuka
 
Back
Top Bottom