Njoo sehemu inaitwa Gikomba, utadhani ni sehemu ya Dar es Salaam, Watanzania wapo hayo maeneo kwa mamia wanapiga mishe zao bila hata kufuatiwa na uhamiaji. Ndio maana nakuambia juhudi zenu za kueneza uwongo hazifui dafu.
Nawafahamu Watanzania wenye daladala nyingi, na hata garage humu. Hata jirani wangu ana ghorofa ya makazi na yupo tu kwenye shughuli zake. Kama una rafiki yeyote kwenye uhamiaji wa Tanzania, kamuulize kwa siku wanapita Watanzania wangapi wakiingia Kenya.
Wacheni kueneza hizi chuki zenu kwa kutumia uwongo, anyway hata wewe kwaheri kama nilivyomuaga mwenzio
bagamoyo ama labda utakua ni yeye unatumia ID moja..... kwaheri.