Wivu si katai lakini ukifikia hapa....!

Wivu si katai lakini ukifikia hapa....!

yamoyoni mwangu

Senior Member
Joined
Oct 25, 2013
Posts
106
Reaction score
31
Daa...! wivu huu hatari mno, hivi uliwahi kuambiwa na your lover kuwa anajisikia vibaya anapokuta simu yako ipo busy...? sasa sikiliza hii, jamaa angu mmoja alikuwa na mpenzi wake ambaye kiukweli alikuwa ame fall in love kinoma, yaani yule kadadaa alikuwa hapendi kabisa simu ya jamaa iwe busy hata siku moja, hata akiikuta kwa bahati mbaya,jamaa lazima awe na kesi ya kujibu kwa mpenziwe, basi jamaa akawa anawaza namna ya kufanya, baada ya kufikiri sana kaona bora aweke huduma ya waiting call. lengo la jamaa ilkuwa endapo atapigiwa simu atajua. Basi yule mdada hakuiishia hapo akamforce jamaa afute namba zote za wadada kwenye simu yake, pamoja na hayo yote kadadaa akamtaka jamaa kila anapoigiwa simu wakiwa wote lazima aweke loudspeker, haikuwa kazi rahisi kwa wadada wengine kuongea na jamaa zaidi ya dakika 3...!JAMAA akaniomba ushauri et afanyeje me nikamwambia aachane nae kwani msichana yupo yeye mweyewe...? ET wadau nyinyi mgemshauri vipi jamaa..? NAOMBA KUWASILISHA....
 
Kuwa na mpenzi asiejiamini ni janga sana na nitatizo kubwa linalofuata baada ya tatizo la ajira na umaskini tanzania...
kwa akili zangu hizi angebadilika kwa lazma na kama hayuko tayar tungepeana jina la Ex muda c muda
 
Khaaa!!! huyo shemeji yako anakaba kama Anti Virus vile...
 
Daa...! wivu huu hatari mno, hivi uliwahi kuambiwa na your lover kuwa anajisikia vibaya anapokuta simu yako ipo busy...? sasa sikiliza hii, jamaa angu mmoja alikuwa na mpenzi wake ambaye kiukweli alikuwa ame fall in love kinoma, yaani yule kadadaa alikuwa hapendi kabisa simu ya jamaa iwe busy hata siku moja, hata akiikuta kwa bahati mbaya,jamaa lazima awe na kesi ya kujibu kwa mpenziwe, basi jamaa akawa anawaza namna ya kufanya, baada ya kufikiri sana kaona bora aweke huduma ya waiting call. lengo la jamaa ilkuwa endapo atapigiwa simu atajua. Basi yule mdada hakuiishia hapo akamforce jamaa afute namba zote za wadada kwenye simu yake, pamoja na hayo yote kadadaa akamtaka jamaa kila anapoigiwa simu wakiwa wote lazima aweke loudspeker, haikuwa kazi rahisi kwa wadada wengine kuongea na jamaa zaidi ya dakika 3...!JAMAA akaniomba ushauri et afanyeje me nikamwambia aachane nae kwani msichana yupo yeye mweyewe...? ET wadau nyinyi mgemshauri vipi jamaa..? NAOMBA KUWASILISHA....


kwa maisha ya watu wa afrika mashari na kati 86% ya matumizi ya simu ni kwa ajili ya mahusiano ya upenzitamaa na ngono tu kwa hiyo ushauri wangu ni kwamba huyo dada avumilie tu maana huo ni ugonjwa wa wengi na hata katika dunia ya kwanza pia takwimu za kuvunjika kwa ndoa nyingi na uchumba ni simu ;ktk nchi ya uingereza ni sababu ya udanganyifu unaofanywa kupitia simu au tumesahau ya marekani ya bill clinton's sexual scandal?

akiwa ''my girl and because I am an East african don't touch my phone and yours I don't touch too''
sina sababu ya kubadili wasichana.
 
Hahahaa haaaa
Ametishaaa
Ila too much
Wakae chini wayaongee
 
kuwa na mpenzi asiejiamini ni janga sana na nitatizo kubwa linalofuata baada ya tatizo la ajira na umaskini tanzania...
Kwa akili zangu hizi angebadilika kwa lazma na kama hayuko tayar tungepeana jina la ex muda c muda

wapo wengi je, utafanya kwa wangap?
 
Wanaume wa sampuli ya huyo jamaa hawatufai katika jamii,kwanini anakuwa zobaaaaa kiasi hicho?
Nalog off
 
Jamaa afanye mambo yake kwa sms tu huyo shem c hashuuliki na sms but anachosha mbaya au labda ndo kashikilia uchumi wote hawo home itabidi jamaa awe mpole tu
 
Huko ni kukosa uhuru katika mahusiano, me naamini hata amchunge vipi jamaa, akiamua kumsaliti ata msaliti tuuu.
 
Back
Top Bottom