Mokaze
JF-Expert Member
- Aug 3, 2018
- 14,375
- 14,870
Imesomeka mkuu.
Vipi huyu mtume anapokea vipi wahyi ilhali haji na kitu kipya katika uislamu ?
Wahyi anaoupokea hasa ni Wahyi wa kusoma na kufundisha Qur'an tukufu. (7:35)
Maana yake ni hii; wakati ambapo Umma wa kiislamu utakapogawanyika katika makundi 73 na yote yatakuwa ya motoni isipokuwa kundi moja, hapo utaona kwamba makundi 72 yote yatakuwa yamepotea hii ni sawa na 98.63% na 1.36% ndio watu wa kundi litakalokuwa limeongoka, kupotea kwa umma wa Kiislamu ni kutokana na kuacha mafundisho sahihi ya Uisilamu.
Kundi hilo lenye 1.36% ni lipi??, Angalia; Madhehebu yote ya Waisilamu mfano Sunni, Ismailia , Shia, Shia athnashara, Bohora, Barelwi, Nakshband, Ibadhi, Answar sunna nk (yapo makundi 72 kwa majina), yote hayo wakiwa wao kwa wao ni maadui na wanakufurishana lakini mbele yao akitokea Muisilamu wa Ahmadiyya WOTE wanaungana na kuwa kitu kimoja dhidi ya Ahmadiyya, yaani makundi 72 yanaungana dhidi ya kundi moja, sasa hiyo ni wazi kabisa Ahnadiyya ndio lile kundi moja;
alilosema Mtukufu Mtume (saw)
ستفترق أمتي على ثلاث و سبيعين فرقة كلهم في النار الا واحدة
الا واحدة isipokuwa moja.
Mafundisho ya Uisilamu safi aliokuja nao mtukufu Mtume Muhammad (saw) yanapatikana katika Jumuiyya ya Ahmadiyya.