Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,933
Habari za jioni Wanajamiiforum? Nimekuwa nikifuatilia session ya jioni ya Bunge,kubwa likiwa ni mjadala wa mabadiliko ya sheria mbalimbali.Mchangiaji wa kwanza, baada ya hotuba ya kambi rasmi ya upinzani,alitoa hoja ya kuahirishwa kwa mjadala,kutokana na mapungufu mengi,lakini kubwa ni pale A.G aliposimama na kusema anapenda mjadala uendelee kwa kuruhusu mabaya yaliopo yaachwe na mazuri yachuliwe,ili hali hoja ni moja tu.
Jana wakati wa mjadala wa bunge Jaji Werema kama mwanasheria Mkuu wa serikali, alipewa nafasi kutoa maoni kama mwanasheria mkuu kuhusu kuahirishwa kwa muswada wa marekebisho ya sheria. Nilishuhudia uelewa mdogo (low reasoning ) ya Werema. Alitoa ushauri ambao uliona kabisa kuwa huyu sawa anaitwa jaji lakini ana mapungufu makubwa. Na nilishatoa thread humu niki-doubt weredi (intelectuality) ya huyu bwana. Niligusia hukumu zake kushindwa kwenye appeal. His professionalism is highly questionable!!!!!!! Bunge zima aliyetoa kauli ya kisheria ni Tundu Lisu ambaye alimshauri naibu spika kanuni za kudumu za bunge zinasemaje kuhusu kuhairisha muswada wa sheria. Na Ndugai alikubali ushauri wa Lisu ingawa hakutaka kuonyesha wazi uwezo wa Lisu. Vinginevyo bunge lingetoa maamuzi kinyume cha taratibu. Hata Waziri wa sheria alitoa maoni kama laywoman wakati ni mwanasheria???.
Werema alitaka viahirishwe vipengele tu vya muswada ambavyo vina utata! Wakati kanuni za kudumu za bunge zinaeleza wazi kuwa mbunge akitoa hoja ya kuahirisha muswada either spika anakubali hoja au anaikataa in totality, basi na si vinginevyo kukata vipande vipande muswada.Hata wewe hujaeleweka ni kitu gani hicho ambachp huyo Jaji na AG hakukitolea ufafanuzi yakinifu? To update you, Waziri wa Sheria wa sasa sio Manasheria!
Habari za jioni Wanajamiiforum? Nimekuwa nikifuatilia session ya jioni ya Bunge,kubwa likiwa ni mjadala wa mabadiliko ya sheria mbalimbali.Mchangiaji wa kwanza, baada ya hotuba ya kambi rasmi ya upinzani,alitoa hoja ya kuahirishwa kwa mjadala,kutokana na mapungufu mengi,lakini kubwa ni pale A.G aliposimama na kusema anapenda mjadala uendelee kwa kuruhusu mabaya yaliopo yaachwe na mazuri yachuliwe,ili hali hoja ni moja tu.
madaraka ya kupeana ndio madhara yake