Waziri wa Nishati, Biteko: Kwa Tsh. 352 unapika mlo mmoja kwa Umeme. Tanzania bado tuna ziada kubwa ya Umeme

Waziri wa Nishati, Biteko: Kwa Tsh. 352 unapika mlo mmoja kwa Umeme. Tanzania bado tuna ziada kubwa ya Umeme

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Doto Mashaka Biteko akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa programu ya utoaji majiko ya umeme kwa bei ya ruzuku kwa wafanyakazi wa TANESCO katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre, Dodoma amesema bado kuna ziada kubwa ya Umeme nchini ambayo tunaweza kutumia katika matumizi mengine.

Kuhusu hali ya upatikanaji wa Umeme nchini "Hadi kufikia mwezi Julai 2025, Tanzania ilikuwa na uwezo wa kuzalisha Megawatt (MW) 2270 vilevile mahitaji ya juu ya Umeme kwenye Grid ya Taifa yalifika Megawatt (MW) 1921 hii inaonyesha kuwa bado kuna ziada kubwa ya Umeme ukichukua jumla ya Umeme wote tulionao zaidi ya Megawatt (MW) 4000"

 
Back
Top Bottom