Waziri wa Elimu, Naibu katibu mkuu hana msaada wowote

Zygot

JF-Expert Member
Apr 14, 2016
2,238
2,866
Waziri Ndalichako, bila kuelewa baada ya hilo la divisheni na GPA utaibuka na nini, sielewi ni kwa jinsi gani utafanyakazi na Naibu katibu mkuu wako anayeshughulikia elimu ya juu. Yaonekana ameshindwa kabisa kuelewa kwamba sasa hivi ana nguvu ya utawala kwa elimu ya juu na watendaji wake. Badala yake anafanya urafiki na viongozi hao kama officemates wake.

Kwa sasa yuko katika juhudi za kukwamisha utatuzi wa matatizo ya uongozi yanayokikabili chuo kikuu cha kilimo cha Sokoine. Hivi karibuni alitembelea chuo baada ya kuwasiliana na uongozi tu! Hapo Nyuma, Chama cha wanataaluma kilimwandikia barua waziri Ndalichako kikitaka aingilie kati matatizo ya upendeleo, wizi wa pesa za wastaafu, ufisadi, uduni wa majengo yaliyojengwa, watumishi kulipwa mishahara isiyostahili yao, chuo kuwa na watendaji wasioweza kutekeleza kazi zao, nk. Ktk barua hiyo ushahidi uliambatanishwa na kumuomba waziri afike kuzungumza na wanataaluma.

Naibu katibu huyu amelibeba na kuahidi kulishughulikia. Imekuwa ni ajabu kwamba badala ya kuyatatua, amefika chuoni na kuteta na viongozi ambao ndo watuhumiwa kwa uzembe na amegeuka baada ya kufanya party na vinywaji kedekede na viongozi hao. Anasema haoni kibaya. Hajaongea na wanataaluma, hajatembelea au kuuliza kwa walalamikaji juu ya matatizo hayo, amekukuwa sehemu ya utawala na sasa analeta vitisho kwa wanataaluma. Sijui kama anajua mipaka ya kazi zake au kama anaijua kasi ya utawala wa sasa.

Hata kama kapozwa kwa pesa kama tunavyosikia, huyu hastahili kuwa Naibu katibu mkuu wa wizara hii. Sijui uwezo wake wa huko alikotoka lakini kwa mwanzo huu sioni kama una msaidizi ktk kazi.

Waziri ingilia kati maana tunachokiona ni kuendeleza upuuzi katika uongozi.
 
Kama ni Naibu katibu mkuu wa elimu siyo yule kijana laiyewahi kufukuzwa kazi UD? Ndo makosa ya kubeba waliowahi kufukuzwa halafu leo eti anafaa kuwa Naibu katibu mkuu. Atawaponza huyu! Lazima ana njaa zake.
 
ni km umeandika ukiwa na jazba/mhemko mkuu.

Talia ipange vizuri utasomeka.
Hata mimi sijamuelewa hasa

Naweza kuwa sikueleweka. Samahani! Maelezo ni kwamba, SUA kuna matatizo kama nilivyoyaandika. Uongozi wa wana taaluma wakayafikisha kwa waziri baada ya kikao kuamua hivyo. Hayo yote ni baada ya uongozi wa chuo kushindwa kabisa kueleza suluhu ya matatizo hayo. Waziri alipoyapokea, akamuomba Naibu waziri huyu aongee na viongozi wa wanataaluma.

Alipoongea nao akasema atayafanyia kazi. Siku chache zilizopita amefika chuoni na badala ya kuongea na wanataaluma, akaongea na viongozi wa chuo tu. Akapiga bufee na kujiondokea pamoja na conclusion kwamba hakuna lolote baya. Nasikia pia alionwa pia na kupewa kibahasha cha safari. Huko wizarani hatujui alipeleka taarifa gani sasa maana matatizo ni yale yale.
 
Naibu katibu mkuu ni matatizo tupu
Mi ni mdau wa hawa watu wa vyuo vikuu na hakika huko kuna majipu ya kishenzi! Nayaita ya kishenzi kwa sababu hawana kisingizio chochote cha kufanya mambo ya kipuuzi kama hayo. Vyuo vikuu vya serikali vyote sasa hivi vinajenga majenga ya hovyo kabisa ukilinganisha na uwezo wao. Ukienda UD, SUA, UDOM, kote unakuta majengo ya miaka mitatu minne yana nyufa za kutilia mashaka ubora wa majengo. Wakati huo huo kuna majengo ya tangu kuwepo kwa chuo, yana hali nzuri kabisa!

Vyuo hivi vyote vina wahandisi wazuri ktk ajira zao lakini watawala wanawatumia wa mitaani ili waibe kwa siri bila kujulikana.

Kama huyo Naibu katibu mkuu naye anajiingiza huko, basi ni mtu asiyefaa kwa wadhifa huo. Kama ni njaa basi huo wadhifa siyo wake kwa miaka hii ya majipu. Utaletewaje matatizo halafu wewe unaleta urafiki na watuhumiwa? Kwani hao ni wanafunzi? Wengine wana sifa kubwa kuliko hata yeye huyo naibu.
 
Hao wote ni MAJIPU ,, Waziri na Katibu mkuu wake wote ni MAJIPU yaliyoiva tayari kwa kutumbuliwa.

Ada elekezi walisema kwa sasa itumike ile ile ya Mwaka jana,, Wenye Shule zao wamewatunishia msuri wanatukamua kwa Ada zao mpya,, hakuna ufuatiliaji wa maagizo yao wamekaa tu ofisini kula upepo wa AC ofisini.

Wenzao sasa hivi hawakai ofsn kufuatilia maafizo yao wao kimya tu wenye shule wanatukamua wananchi.
 
Mi ni mdau wa hawa watu wa vyuo vikuu na hakika huko kuna majipu ya kishenzi! Nayaita ya kishenzi kwa sababu hawana kisingizio chochote cha kufanya mambo ya kipuuzi kama hayo. Vyuo vikuu vya serikali vyote sasa hivi vinajenga majenga ya hovyo kabisa ukilinganisha na uwezo wao. Ukienda UD, SUA, UDOM, kote unakuta majengo ya miaka mitatu minne yana nyufa za kutilia mashaka ubora wa majengo. Wakati huo huo kuna majengo ya tangu kuwepo kwa chuo, yana hali nzuri kabisa!

Vyuo hivi vyote vina wahandisi wazuri ktk ajira zao lakini watawala wanawatumia wa mitaani ili waibe kwa siri bila kujulikana.

Kama huyo Naibu katibu mkuu naye anajiingiza huko, basi ni mtu asiyefaa kwa wadhifa huo. Kama ni njaa basi huo wadhifa siyo wake kwa miaka hii ya majipu. Utaletewaje matatizo halafu wewe unaleta urafiki na watuhumiwa? Kwani hao ni wanafunzi? Wengine wana sifa kubwa kuliko hata yeye huyo naibu.

Mkuu ulichosema ni kweli tupu. Kwa nyongeza siyo tu Vyuo vikuu kama ulivyoahinisha hapo juu hata hizi Tertiary Institutions zote za serikali viongozi wa baadhi ya vyuo hivi ni majipu tu. Wengi hawafuati taratibu za kiuongozi, ni wizi wa fedha za serikali ufisadi wa kila aina. Na ufisadi mwingi umekuwa ukifanywa kwa kushirikiana na wenyeviti wa bodi za wakurugenzi, Makatibu wakuu au manaibu katibu Mkuu wa Wizara na hata sehemu zingine Mawaziri nao wamekuwa wakijihusisha na ufisadi kwenye taasisi hizi.
Nadhani Majipu ya sehemu za Taaluma yalipaswa yatumbuliwe mapema kabisa.
 
Je Ndalichako kapoozwa au kajipoozesha?
Hata mimi nimekuwa na wasiwasi juu ya utendaji wa waziri wa Elimu. Yawezekana alikuwa fundi kule baraza la mitihani, sasa kapewa uwaziri kwa sifa kubwa imekuwa vigumu kuonyesha uwezo huo. Isije ikawa ni kama enzi zile za Keenja wa jiji alivyovuna sifa baadaye uwaziri akapwaya.
 
Naweza kuwa sikueleweka. Samahani! Maelezo ni kwamba, SUA kuna matatizo kama nilivyoyaandika. Uongozi wa wana taaluma wakayafikisha kwa waziri baada ya kikao kuamua hivyo. Hayo yote ni baada ya uongozi wa chuo kushindwa kabisa kueleza suluhu ya matatizo hayo. Waziri alipoyapokea, akamuomba Naibu waziri huyu aongee na viongozi wa wanataaluma.

Alipoongea nao akasema atayafanyia kazi. Siku chache zilizopita amefika chuoni na badala ya kuongea na wanataaluma, akaongea na viongozi wa chuo tu. Akapiga bufee na kujiondokea pamoja na conclusion kwamba hakuna lolote baya. Nasikia pia alionwa pia na kupewa kibahasha cha safari. Huko wizarani hatujui alipeleka taarifa gani sasa maana matatizo ni yale yale.

Naibu Katibu, Naibu waziri, sielewi!
 
Naweza kuwa sikueleweka. Samahani! Maelezo ni kwamba, SUA kuna matatizo kama nilivyoyaandika. Uongozi wa wana taaluma wakayafikisha kwa waziri baada ya kikao kuamua hivyo. Hayo yote ni baada ya uongozi wa chuo kushindwa kabisa kueleza suluhu ya matatizo hayo. Waziri alipoyapokea, akamuomba Naibu waziri huyu aongee na viongozi wa wanataaluma.

Alipoongea nao akasema atayafanyia kazi. Siku chache zilizopita amefika chuoni na badala ya kuongea na wanataaluma, akaongea na viongozi wa chuo tu. Akapiga bufee na kujiondokea pamoja na conclusion kwamba hakuna lolote baya. Nasikia pia alionwa pia na kupewa kibahasha cha safari. Huko wizarani hatujui alipeleka taarifa gani sasa maana matatizo ni yale yale.

Hili ni jukwaa la GREAT THINKERS mkuu. Hebu analyse tatizo moja baada jingine kwa ufasaha na namna naibu katibu mkuu huyo alivyoshughulikia au alivyoshindwa kushughulikia.

Then, sema ni kwa nini unadhani Waziri aingilie kati. Vinginevyo mimi bado tu sijakuelewa kwa sababu nilichoona ni kimoja tu kuwa baadhi ya watu kulipwa mishahara wasiyostahili lakini bila kueleza in detail!!
 
Back
Top Bottom