Waziri Makamba na Bodi TANESCO mnasubiri nini?

Waziri Makamba na Bodi TANESCO mnasubiri nini?

voicer

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2020
Posts
5,545
Reaction score
11,943
Punde tu baada ya kuingia,uliivunja bodi iliyokuwepo "Tanesco" na Ukaunda yako ya "Tan-Escrow"
25/Sep/2021.

Baadhi ya tambo zenu zilikuwa hizi.

"Tunataka baada ya miaka mitatu Shirika liingie katika orodha ya mashirika bora, yenye thamani na yanayoheshimika Afrika" alisema Mhe. January Makamba"

"Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO, Bw. Omari Issa, amesema atahakikisha Bodi inafanya kazi na kutimiza malengo yake kwa kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa malengo na uwajibikaji."

"Nimhakikishie Mhe. Waziri tutahakikisha tunarudisha heshima ya Shirika na ufanisi kupitia ushirikiano wenu, hakuna Shirika lolote linalotoa huduma ya umeme zaidi yetu sisi, yamkini tuwape wateja wetu huduma wanayostahili", " alisema Bw. Maharage Chande"

Na wajumbe uliowateua ni hawa.

"Taarifa kwa umma ya leo Jumamosi Septemba 25, 2021 iliyotolewa na Waziri imewataja wajumbe hao ni Nehemia Mchechu, Zawadia Nanyaro, Lawrence Mafuru, Eng Cosmas Masawe, Abubakar Bakhresa, Eng. Abdallah Hashim, Balozi Mwanaidi Maajar, Christopher Mwita Gachuma."

Ebu tufananishe na wajumbe waliokuwepo awali,kabla ya Makamba!

"Balozi Dk James Nzagi (alikuwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO iliyomaliza muda wake) na Dkt. John Kihamba (Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Saam - DUCE).

Wengine ni Dk Lugano Wilson (Mkurugenzi wa Maendeleo ya Uhandisi na Mkuu wa Teknolojia za Nishati - TIRDO), John Kulwa (Mkuu wa Idara ya Ukaguzi Chuo Kikuu Kishiriki cha Afya na Sayansi Shirikishi - MUHAS) na Denis Munumbu (Mchunguzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa - TAKUKURU).

Wengine ni Dk Gemma Modu (Mkurugenzi NACTE), Mathew Kirama (Mkurugenzi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma) na Gilay Shamika (Mjumbe katika bodi iliyopita)"

Halafu tujiulize Rasmi

#Makamba Na Bodi yako ya Kubumba,yenye wajumbe wenye kutia shaka,kuanzia "kitaaluma" mpaka "kimaadili."

Mnakotupeleka ni wapi?
Mnachotufanyia wananchi ni kwa maslahi yenu au yetu?

Dalili zenu kushindwa kazi ziko wazi kabisaaaa!

Mnasubiri nini hapo Maofisini?

Alamsikhi!


makamba%2Bpic.jpg
Screenshot_20210925-180245.jpg
IMG-20221121-WA0007_remastered.jpg
 
Wapo ofisini kutekeleza majukumu yao ya kila siku, hata ukipewa wewe hio nafasi huwezi kumaliza matatizo yote.
Tuache kuwa watu wa kulaumu tu.
 
Watanzania hamna shukrani. 2025 lazima watu tuwe na hela za uchaguzi. Ama tukishindwa uchaguzi na kukaa benchi basi lazima tuwe na hela za kutosha maana tukiachia madaraka halafu tuwe hatuna hela mtatucheka vicheko vya dharau eti alikuwa waziri na hana hela, hakuna anayeitaka hiyo aibu kabisa.

Hii nchi mwenye nayo hayupo lazima ukipata nafasi ibaaa maana nyie watanzania hakuna shukrani maana ona tu kwa Dkt Magufuli au Dkt Kikwete kila siku matusi matusi mara ohh Dkt Magufuli fisadi oh mara sijui miradi.

Sasa hii safari lazima kuwakomesha kabisa na uzuri hakuna mwenye kuweza kuitoa CCM madarakani
 
Watanzania hamna shukrani. 2025 lazima watu tuwe na hela za uchaguzi. Ama tukishindwa uchaguzi na kukaa benchi basi lazima tuwe na hela za kutosha maana tukiachia madaraka halafu tuwe hatuna hela mtatucheka vicheko vya dharau eti alikuwa waziri na hana hela, hakuna anayeitaka hiyo aibu kabisa. Hii nchi mwenye nayo hayupo lazima ukipata nafasi ibaaa maana nyie watanzania hakuna shukrani maana ona tu kwa Dkt Magufuli au Dkt Kikwete kila siku matusi matusi mara ohh Dkt Magufuli fisadi oh mara sijui miradi. Sasa hii safari lazima kuwakomesha kabisa na uzuri hakuna mwenye kuweza kuitoa CCM madarakani
Sawa mkuu Empty Skull Minded mwingine
JamiiForums1689545919.jpg
 
Watanzania hamna shukrani. 2025 lazima watu tuwe na hela za uchaguzi. Ama tukishindwa uchaguzi na kukaa benchi basi lazima tuwe na hela za kutosha maana tukiachia madaraka halafu tuwe hatuna hela mtatucheka vicheko vya dharau eti alikuwa waziri na hana hela, hakuna anayeitaka hiyo aibu kabisa. Hii nchi mwenye nayo hayupo lazima ukipata nafasi ibaaa maana nyie watanzania hakuna shukrani maana ona tu kwa Dkt Magufuli au Dkt Kikwete kila siku matusi matusi mara ohh Dkt Magufuli fisadi oh mara sijui miradi. Sasa hii safari lazima kuwakomesha kabisa na uzuri hakuna mwenye kuweza kuitoa CCM madarakani
Kwa sababu unawaza kwa kutumia utumbo!

Nimekuelewa!

Kwa sababu,ujinga ni moja ya sifa kuu pale Lumumba!

Nimekuelewa!

Kwamba wewe nae ni walewale...
Empty Skull Minded mliojazana huko Green-Guard
JamiiForums1689545919.jpg
 
TUSUBIRI TUUNDE KIKOSI KAZI kwa sasa ni Mwendo wa Vikosi kazi
 
Wapo ofisini kutekeleza majukumu yao ya kila siku, hata ukipewa wewe hio nafasi huwezi kumaliza matatizo yote.
Tuache kuwa watu wa kulaumu tu.
Wewe huna akili, hii wanayo ifanya jmakamba na board member wake, ni hopeless kabisa......weledi ni mdogo kuliko board member yoyote iliyo wai kuundwa na
Maziri walio pita... kwa ufupi hii wizara ni kubwa kuliko uwezo wa huyo jamaaa
Kwa nn wasimpe zile wizara za kutali na kutembea nchi za nje kwa maana ndiyo hulka yake
Mm kwa upande wangu wampe waziri wa utali kidogo not tangible sana wananchi wa chini
 
Hicho ni kikundi kwa ajili ya kusapoti urais wa makamba. Hakuna jipya hapo zaidi ya kukusanya pesa ya kampeni.

Ukiwa na akili timamu, mwenye aibu na una lengo la kutatua shida za watu huwezi kuthubutu kuweka hao jamaa hapo.

Kweli yule mzee Magu aliposema ipo siku mtanikumbuka alinena haswa. Aliyokuwa anayajua na kuyaona kwetu sisi ilikuwa ni ardhi na mbingu. Tulikuwa hatuelewi kitu kabisa. Ila muda unatuhukumu
 
Ni mwendo wa vibatari na mishumaa.
Natanga tanga na Tanzagiza.

Mama tumekomaa🙏
 
Hicho ni kikundi kwa ajili ya kusapoti urais wa makamba. Hakuna jipya hapo zaidi ya kukusanya pesa ya kampeni.

Ukiwa na akili timamu, mwenye aibu na una lengo la kutatua shida za watu huwezi kuthubutu kuweka hao jamaa hapo.

Kweli yule mzee Magu aliposema ipo siku mtanikumbuka alinena haswa. Aliyokuwa anayajua na kuyaona kwetu sisi ilikuwa ni ardhi na mbingu. Tulikuwa hatuelewi kitu kabisa. Ila muda unatuhukumu
Kwa uhakika kabisaa!
 
Back
Top Bottom