Napenda kutumia nafasi hii kutoa dukuduku langu. ni miaka kadhaa sasa tangu mheshiwa Magufuri kuitenga kwa makusudi wilaya ya Biharamulo kwa kuinyang'anya barabara ya rami na hatimaye kuiacha katika lindi kubwa la umasikini kwani hata barabara iliyopo kwa sasa ni aibu tupu. ukisafiri kwa gari ikitokea mkoa wa Geita mwisho wa uhai huishia "Bwanga" ambapo barabara ya rami huchepuka kuelekea Chato na hatimaye Bukoba na kuiacha ile ya Biharamulo katika hali tete, kwani ukiingia kule utadhani umeingia Dunia nyingine tofauti, na Dunia hii ni ya watu waliotengwa tena kwa makusudi, sasa sijui tuiite "The Repulic of Biharamulo" au la! Barabara hii ilichepushwa na muheshiwa toka enzi za Mkapa na kufuatiwa na ahadi lukuki za kumalizia kipande hicho zilizotolewa Bungeni na aliyekuwa waziri mkuu enzi hizo baada ya mheshiwa huyu kubanwa na wabunge. sasa ni takribani miaka kumi na miwili na ushee tangu uongozi wa JK bado kimya!! najipa moyo kuwa hiki si kisasi kwa watu wa Biharamulo Magharibi bali ni sababu tofauti. nilidhani baada ya kupewa rungu jipya maheshiwa angetoa upendeleo wa makusudi ili kufuta dhambi hii aliyowatendelea raia wa Biharamulo lakini mmmh!
Nchi ni yetu sote na hivyo kubaguana si sawa.
Nchi ni yetu sote na hivyo kubaguana si sawa.