Waziri Dkt. Dorothy Gwajima amesema ukitaka kumchapa mtoto umuombe ruhusa. Hili linawezekana vipi?

FURY BORN

JF-Expert Member
Jul 11, 2020
638
1,145
Wanajamii forums, nisiwachoshe nimekutana na hili tamko la waziri afya Dr Gwajima ya kwamba ukitaka kumchapa Mtoto muombe ruhusa Kwa sababu ana haki zake.

Nikabaki najiuliza kwamba nikitaka kumwadhibu mwanangu nimuite fulani njoo, alafu Kisha nimwambie mwanangu naomba nikuchape, akikataa namwacha au sasa ndo nafanyaje? Alafu baadae viongozi mtarudi kutwambia maadili yameporoka.

======

Kauli hiyo imetolewa na Dkt. Gwajima mnamo Juni 9, 2021 jijini Dodoma wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu maadhimisho ya Mtoto wa Afrika ambayo yataenda sambamba na uzinduzi wa Makao ya Taifa watoto katika eneo la Kikombo.

"Akili ya toto inabidi iandaliwe iweze kukubali na kukataa mafunzo ya kuficha vitendo vya ukatili. Ukimfanyia nyumbani ataenda kuvisema shuleni. Ukimfanyia nyumbani anajua kabisa kuwa mimi haifai kupigwa, kufinywa bila utaratibu. Maana ifike mahala hata kumpiga umuombe ruhusa; naomba nikuchape kidogo. Mtoto ana haki zake!"

Sasa wewe unataka kumpiga tu, unamuumiza, unamfungia ndani anaugua – atakusema. Tunakwenda kwenye Child Empowerment, yaani kum-empower mtoto tangu akiwa mdogo – kama Watoto wa mataifa mengine.

Alisema Waziri Dkt Dorothy Gwajima.
 
Asitupangie, yeye hakuchapwa? Dogo akizingua anakula bakora za kutosha tu
 
Nadhani alimaanisha kumuelewesha mtoto kwa nini unataka kumchapa, by the way sio mala zote fimbo zimeleta matokeo chanya katika kulea mtoto. Mi wanangu siwachapi ni risala tu za kutosha na wanaelewa,
 
Yani nisimamie ukucha kumpata yeye halafu nimuombe ruhusa ya kumchapa? Hilo haliwezekani, nitamkunyuga tu atake asitake.
 
Yani nisimamie ukucha kumpata yeye halafu nimuombe ruhusa ya kumchapa? Hilo haliwezekani, nitamkunyuga tu atake asitake.
Hiyo ya kusimamia ukucha sio issue kwa sababu hajakutuma usimamie ukucha kumleta duniani.

Point yangu hapa ni mtoto akishazaliwa anatakiwa afundishwe na mzazi/mlezi/jamii kujua wajibu wake ni upi pia nidhamu kwa ujumla asipotimiza lazima mzazi umdhibiti kabla hajaharibika ili taifa na jamii isiwe na raia asiefaa.

Wajibu na haki viende kwa pamoja sio kujikita tu kwenye haki huku wajibu hawazungumzii.
 
Mweleweshe kosa lake na umchape kwa upendo kama mzazi fimbo mbili au tatu makalioni taratibu na sio kumvamia kama kibaka. Baadhi wameingia matatizoni kwa approach mbovu za kuadhibu watoto badala ya kumsaidia unakuwa unazidi kumharibu kama sio kumuumiza au kuua kabisa.
 
Wanajamii forums, nisiwachoshe nimekutana na hili tamko la waziri afya Dr Gwajima ya kwamba ukitaka kumchapa Mtoto muombe ruhusa Kwa sababu ana haki zake.
Nikabaki najiuliza kwamba nikitaka kumwadhibu mwanangu nimuite fulani njoo, alafu Kisha nimwambie mwanangu naomba nikuchape, akikataa namwacha au sasa ndo nafanyaje? Alafu baadae viongozi mtarudi kutwambia maadili yameporoka.
Atuambie kwanza ameanza lini kuiapply nyumbani kwake asije akatulisha matango pori!!!?
 
Nadhani alimaanisha kumuelewesha mtoto kwa nini unataka kumchapa, by the way sio mala zote fimbo zimeleta matokeo chanya katika kulea mtoto. Mi wanangu siwachapi ni risala tu za kutosha na wanaelewa,
Wana miaka mingapi?
 
😂😂😂 Wewe mwanangu mtarajiwa jiandae kwa kula kelebu la hatari mana siwezi kukuomba ruksa ya kipigo
 
Asubiri siku atayotumbuliwa kama Rais atamuomba ruksa ya kumtumbua
 
Hivi Dr gwajima si mtu wa kanda ya ziwa?

Tangu lini watu wa kanda ya ziwa wakalea watoto kimayai namna hii
 
Basi sawa,kwako pia havikukusaidia kukunyoosha?
Viliniharibu sana, nilishawahi kutoroka nyumbani wiki mbili kisa naogopa kipigo, mtu unachapwa kama mwizi kumbe tu hujaosha vyombo au umechelewa kurudi home, nachukia maisha yale na stamani wanangu wapitie huko. siwapigi kabisa hata vibao nooo.
 
Sawa
Viliniharibu sana, nilishawahi kutoroka nyumbani wiki mbili kisa naogopa kipigo, mtu unachapwa kama mwizi kumbe tu hujaosha vyombo au umechelewa kurudi home, nachukia maisha yale na stamani wanangu wapitie huko. siwapigi kabisa hata vibao nooo.
Sawa una sababu ya kuona hivyo, ila isiwe mchelea mwana kulia hulia yeye.
 
Sawa

Sawa una sababu ya kuona hivyo, ila isiwe mchelea mwana kulia hulia yeye.
wananielewa mkuu ndio maana siwapigi, ingekua hawaelewi na ni wakaidi ningewachapa ila sio randomly kama vibaka ningekuwa nawaeleza sababu ndio nawachapa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom