Boran Jakutay
Senior Member
- Apr 8, 2023
- 110
- 260
Takriban watu 78 wameuawa katika mkanyagano katika shule moja katika mji mkuu wa Yemen, Sanaa wakati wa ugawaji wa misaada kwa ajili ya Ramadhani, maafisa wanasema.
Kanda za video kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha matukio ya fujo baada ya tukio hilo katika eneo la Bab-al-Yemen mjini humo. Shirika la habari la Reuters linaripoti kwamba mamia ya watu walimiminika katika shule hiyo kupokea michango ambayo ilikuwa takriban $9 (£7) kwa kila mtu.
Waasi wa Houthi wameendesha mji huo tangu walipoiondoa serikali mwaka wa 2015. Wale waliohusika na usambazaji huo wamezuiliwa na uchunguzi unaendelea, wizara ya mambo ya ndani ilisema.
Msemaji wa wizara hiyo alilaumu mkanyagano huo "usiokuwa na mpangilio" wa kutoa fedha bila kuwa na utaratibu na viongozi wa eneo hilo.
Watu wengi pia walijeruhiwa huku 13 wakiwa katika hali mbaya, afisa wa afya mjini Sanaa alisema
Shirika la habari la Associated Press linawanukuu watu wawili walioshuhudia ambao walisema wapiganaji wa Houthi walifyatua risasi hewani katika kujaribu kudhibiti umati wa watu, wakionekana kugonga waya wa umeme ambao ulisababisha mlipuko.
Hii ilisababisha hofu iliyosababisha kukanyagana, waliongeza.
Tukio hilo lilitokea wakati wa siku za mwisho za mwezi mtukufu wa Waislamu wa Ramadhani, ambao huadhimishwa na kipindi cha mfungo.
Yemen imeathirika na mzozo ulioongezeka tangu mwaka wa 2015, wakati Wahouthi walipochukua udhibiti wa maeneo makubwa ya magharibi mwa nchi hiyo.
Kanda za video kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha matukio ya fujo baada ya tukio hilo katika eneo la Bab-al-Yemen mjini humo. Shirika la habari la Reuters linaripoti kwamba mamia ya watu walimiminika katika shule hiyo kupokea michango ambayo ilikuwa takriban $9 (£7) kwa kila mtu.
Waasi wa Houthi wameendesha mji huo tangu walipoiondoa serikali mwaka wa 2015. Wale waliohusika na usambazaji huo wamezuiliwa na uchunguzi unaendelea, wizara ya mambo ya ndani ilisema.
Msemaji wa wizara hiyo alilaumu mkanyagano huo "usiokuwa na mpangilio" wa kutoa fedha bila kuwa na utaratibu na viongozi wa eneo hilo.
Watu wengi pia walijeruhiwa huku 13 wakiwa katika hali mbaya, afisa wa afya mjini Sanaa alisema
Shirika la habari la Associated Press linawanukuu watu wawili walioshuhudia ambao walisema wapiganaji wa Houthi walifyatua risasi hewani katika kujaribu kudhibiti umati wa watu, wakionekana kugonga waya wa umeme ambao ulisababisha mlipuko.
Hii ilisababisha hofu iliyosababisha kukanyagana, waliongeza.
Tukio hilo lilitokea wakati wa siku za mwisho za mwezi mtukufu wa Waislamu wa Ramadhani, ambao huadhimishwa na kipindi cha mfungo.
Yemen imeathirika na mzozo ulioongezeka tangu mwaka wa 2015, wakati Wahouthi walipochukua udhibiti wa maeneo makubwa ya magharibi mwa nchi hiyo.