Watumishi Wa Bwana Wenye a.k.a Za Nini?

Wa Mjengoni

JF-Expert Member
May 4, 2010
480
128
Naseeb ndiye a.k.a yake Diamond, Ambwene a.k.a yake AY, Marehemu footbalist Ezekiel Grayson aliitwa jujuman n.k.

Nadhani hizi a.k.a wanatumia wasanii na watu wengine wenye vipaji mbalimbali kuvuta hisia za mashabiki wao.

Swali langu ni kwamba tunapokuwa kwenye nyumba za ibada zetu ni ustaarabu kweli Watumishi kuwa na a.k.a kama Transformer, Caterpillar, au a.k.a ya yule mwingine nimesahau yuko Star TV ameanza kuonyesha kipindi karibuni, zinasaidia nini au ili iweje? Ebu nijulisheni.

Tumezoea kusikia tu Askofu Kakobe, Askofu Malasusa, Kardinali Pengo n.k., bila a.k.a. sasa tunakokwenda ndo wapi?
 
Suala ni kuwa a.k.a hizo zisiwe za matusi...ktk BIBLIA..Yesu aliwaongezea majina mengine baadhi ya wanafunzi wake..mfano Petro aliitwa 'KEFA' maana yake jiwe..
 
Siku hizi watu wamezama kwenye miujiza na haja za mwili kuliko ufalme wa Mungu....hivyo hizo a.k.a ni chagizo kwa wapenda miujiza na sio injili ya ule wokovu wa kweli yaani kufa katika hali ya neema (please si zile neema zetu zileee bali Utakatifu).
 
Naseeb ndiye a.k.a yake Diamond, Ambwene a.k.a yake AY, Marehemu footbalist Ezekiel Grayson aliitwa jujuman n.k.

Nadhani hizi a.k.a wanatumia wasanii na watu wengine wenye vipaji mbalimbali kuvuta hisia za mashabiki wao.

Swali langu ni kwamba tunapokuwa kwenye nyumba za ibada zetu ni ustaarabu kweli Watumishi kuwa na a.k.a kama Transformer, Caterpillar, au a.k.a ya yule mwingine nimesahau yuko Star TV ameanza kuonyesha kipindi karibuni, zinasaidia nini au ili iweje? Ebu nijulisheni.

Tumezoea kusikia tu Askofu Kakobe, Askofu Malasusa, Kardinali Pengo n.k., bila a.k.a. sasa tunakokwenda ndo wapi?

Tunaenda na wakati ndg yangu we upo karne ya ngapi
 
Siku hizi wachungaji au wahubiri ni wachache sana, waliojaa ni matapeli ambao labda haikuwa nia yao kabla kutapeli au kutumika na Shetani bali wamejikuta wanasombwa na nguvu kubwa ya Mwovu shetani inayotumika hapa duniani na kujikuta tu wamekuwa feki!!

Ishu ni kuwa makini tu na hawa wahubiri wa kisasa. Wengine ni matapeli waziwazi kabisaa, ila sijui kwa nini waTanzania walio wengi wanashindwa kuwatambua na wanawafuata kwa wingi saana.
Naamini walio wengi ni NJAA na matatizo yanayowafanya wawe vipofu kiasi cha kutoona utapeli na injili FEKI wahubiriwayo!!!
 
Suala ni kuwa a.k.a hizo zisiwe za matusi...ktk BIBLIA..Yesu aliwaongezea majina mengine baadhi ya wanafunzi wake..mfano Petro aliitwa 'KEFA' maana yake jiwe..

wale wengine aliwaita wana wa ngurumo.
 
Siku hizi watu wamezama kwenye miujiza na haja za mwili kuliko ufalme wa Mungu....hivyo hizo a.k.a ni chagizo kwa wapenda miujiza na sio injili ya ule wokovu wa kweli yaani kufa katika hali ya neema (please si zile neema zetu zileee bali Utakatifu).

miaka iliyopita, mwinjilist mmoja alijiita mzungu four, sidhani kila mmoja analenga miujiza na haja za mwili.
 
Yesu ndo njia kweli na uzima a.k.a hazimpeleki mtu mbinguni

bila kusahau kuomba kwa makelele njia panda, kutoa sadaka kwenye kipaza sauti waumini wote wakasikia.., wala si kusema Bwana, Bwana bila kusahau kutenda miujiza kwa jina lake vyote hivyo havikuhakikishii mbingu.
 
Naseeb ndiye a.k.a yake Diamond, Ambwene a.k.a yake AY, Marehemu footbalist Ezekiel Grayson aliitwa jujuman n.k.

Nadhani hizi a.k.a wanatumia wasanii na watu wengine wenye vipaji mbalimbali kuvuta hisia za mashabiki wao.

Swali langu ni kwamba tunapokuwa kwenye nyumba za ibada zetu ni ustaarabu kweli Watumishi kuwa na a.k.a kama Transformer, Caterpillar, au a.k.a ya yule mwingine nimesahau yuko Star TV ameanza kuonyesha kipindi karibuni, zinasaidia nini au ili iweje? Ebu nijulisheni.



Unatuuliza mnaenda wapi?? huko mankoenda ni kule mliko chagua wenyewe sisi hatuko huko
 
Naseeb ndiye a.k.a yake Diamond, Ambwene a.k.a yake AY, Marehemu footbalist Ezekiel Grayson aliitwa jujuman n.k.

Nadhani hizi a.k.a wanatumia wasanii na watu wengine wenye vipaji mbalimbali kuvuta hisia za mashabiki wao.

Swali langu ni kwamba tunapokuwa kwenye nyumba za ibada zetu ni ustaarabu kweli Watumishi kuwa na a.k.a kama Transformer, Caterpillar, au a.k.a ya yule mwingine nimesahau yuko Star TV ameanza kuonyesha kipindi karibuni, zinasaidia nini au ili iweje? Ebu nijulisheni.

Tumezoea kusikia tu Askofu Kakobe, Askofu Malasusa, Kardinali Pengo n.k., bila a.k.a. sasa tunakokwenda ndo wapi?

Unatuuliza mnaenda wapi???..... manakoenda ni kule mliko chagua wenyewe.. sisi hatuendi huko kamwe!! sisi si wa huko
 
...nipe maana kamili ya neno a.k.a alafu niambie ubaya wake...
 
Tunaenda na wakati ndg yangu we upo karne ya ngapi

maandiko matakatifu yanasema Yesu ni Alfa na Omega yeye hana wakati,fasheni wala chochote cha kumshinda kwa umaarufu na utakatifu hata ulinganishe matendo yake na kazi za kutengenezwa na wanadamu .

Mkuu Kidogo Chetu nakuunga mkono 100%.

Kazi za akina Diamond ndo zinaenda na wakati, mfano enzi za Mbaraka Mwinshehe sikusikia a.k.a lkn sasa ni fasheni kwa wengi wa Wanamuziki. Sasa Midfield anasapoti hii fasheni ihamie kwenye utumishi wa Mungu si kufuru hiyo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom