Watanzania wanastahili pongezi

Watanzania wanastahili pongezi

Mariswaga

JF-Expert Member
Joined
Aug 25, 2015
Posts
201
Reaction score
2
Hata kama upinzani ukishamiri namna gani lakini Watanzania wengi wanautambua umuhimu wa nchi yao kuongozwa na Rais wa Chama Cha Mapinduzi; wako radhi kumchagua Mbunge wa chama chochote cha upinzani lakini hawako tayari kuongozwa na Rais toka nje ya CCM.

Siyo kama hawayaoni mapungufu yaliyopo ndani ya CCM, la hasha bali wanatazama maandalizi hafifu na uwezo mdogo wa vyama vya upinzani kuiongoza nchi yao. Hivyo ni vema wakiendelea kuongozwa na CCM yenye mapungufu ambayo yanaweza kurekebishwa kuliko kuongozwa na upinzani wenye maandalizi hafifu na uwezo mdogo.

Haya ndiyo mapenzi ya Watanzania kwa nchi yao. Hawako tayari kuuweka madarakani uongozi usio na hatima njema kwa nchi yao.

Hali ilivyo hivi sasa Watanzania wameamua kumchagua Dr. John Pombe Magufuli kwakua ndiye mwenye uwezo na dhamira ya dhati ya kuifikisha nchi yetu sehemu nzuri.

Tafadhali usikose kwenda kupiga kura ifikapo Oct 25, usiende peke yako; ondoka na wanafamilia wako na rafiki zako mukampigie kura Dr. John Pombe Magufuli akutumikie kwa uadilifu na uchapakazi
 
Heko kwa Wananchi wa Tanzania. Sisi ndio mabadiliko tuliyokuwa tunayasubiri. Pongezi kubwa kwa Wananchi wa Tanzania kwa kuamka baada ya usingizi wa muda mrefu. Serikali ya Tano, iwe Lowassa au Magufuli mambo hayatakuwa kama kawaida miaka ya nyuma.

hata kwa wale waoofia Lowassa ataendeleza rushwa, HILO HALITATOKEA serikali ijayo maana wananchi, Bunge wameamka.

Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Afrika.
 
Watanzania wanastahili pongezi mwaka huu, kwa kudhamiria kuitoa CCM madarakani. HONGERENI SANA!!!!!!! TUFANYE KWELI 25.10.
 
Back
Top Bottom