Mmh!! mchango mzuri, umejaribu kuelezea hali halisi, lakini ni hali halisi kwa wale wote waliozoea "kawaida", nadhani ni wakati muafaka tukaanza kuzoea hali halisi yaani "mabadiliko".
kama utakumbuka wakati wa uchaguzi wa marekani 2008 (nasikitika sina mfano mwingine rahisi), ni sehemu ndogo sana ya mamia ya wanamageuzi wenye hamu ya ladha ya mageuzi ndani ya marekani waliamini kuwa wangeweza kuiangusha mibepari ya Wall Street. Hata midahalo ya vijiweni hapa Tanzania ilionyesha wazi wazi kuwa wengi walipendelea kuona Obama anaingia ikulu lakini ni nani alikuwa na uhakika wa hilo?
narudia kusema kuwa labda Marekani sio mfano mzuri kwa Tanzania, lakini lengo langu ni kuonyesha kuna idadi kubwa sana ya watanzania wa rika zote na itikadi tofauti tena ndani ya serikali wangependa kuona mabadiliko, lakini kila mmoja wao anaamini "labda ni mimi tu", hili ni jinamizi baya sana na linakandamiza hata wasomi hawapigi kura siku hizi! Jamani! kwapamoja tunaweza kuipeleka Tanzania yetu pale tunapotaka.
Watanzania! hata mlima unaweza kuanguka lakini tusisahau kuna gharama yake na ni vyema kila mmoja wetu akafanya sehemu ya kwa wakati sahihi na sio kwa wakati wake.