Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 17,439
- 43,574
Hatimaye Tundu Antipasi Lissu Amerejea Nyumbani:
Mheshimiwa sana, Mzalendo wa Kweli, Mwenye Upendo wa Kweli, Tundu Antipasi Lisu karibu nyumbani Tanzania. Tanzania, nchi ambayo kama siyo kwa mapenzi ya Mungu usingeweza kuiona tena kwa macho ya mwili.
Tundu Antipasi Lisu Dhihirisho la Ushindi wa Mungu
Tundu Antipas Lissu, kuishi kwako mpaka leo siyo ushindi wako bali ni ushindi wa Mungu dhidi ya shetani. Baada ya Mungu kumshinda shetani, na ukuu wake hudhihirika, wewe uliyelala mauti na Mungu, na Mungu kuyashinda mauti ya shetani, itakuwa ni laana kwako nasi tunaosimama na Mungu wa haki, siku moja tukarudi tukaungana na shetani. Tukifanya hivyo, ushindi wa Mungu dhidi ya shetani hautakuwa na maana
Tundu Antipas Lissu ni Mageuzi ya Falsafa ya Siasa za Tanzania
Siasa za Tanzania zimejaa ulaghai, hila, unafiki, uoga, rushwa na hata ushirikina. Lakini siasa ndiyo hutoa wafalme, watawala na viongozi wote Duniani. Je, ni halali anayewaongoza watu kuwa mnafiki, mlaghai, mwongo na mtoa rushwa? Hapana. Siyo sahihi. Imekuwa kama ilivyo kwa sababu katika siasa za Tanzania ndiko shetani anakoishi.
Tundu Lisu unatakiwa kuzigeuza siasa za Tanzania kutoka kwenye hali ya sasa mpaka kuifanya siasa kuwa ni ukweli, uungwana, ujasiri wa kuunena ukweli na usafi dhidi ya kila uchafu ufananao na rushwa. Leo kwenye kura za maoni ndani ya CCM ni kilio. Kwa sababu kila aina ya uchafu vimetumika. Iwe ni wapinzani au CCM, wamechoka siasa za uwongo, unafiki, hila na uoga. Wewe ndiye utayaongoza mabadiliko haya.
Tundu Antipasi Lissu ni Kifutio cha Dhulma na Upendeleo
Tanzania ya leo, watu wanalia kwa uonevu, chuki na upendeleo. Watu wanalalamikia upendeleo wa ukanda, undugu, na kwa mbali udini. Watu wanalia kwa kudhulumiwa mali zao walizositafuta kwa haki. Watu wanalia kwa kubambikiwa kesi za uhujumu uchumi bila ya kuhujumu uchumi, kutakatisha fedha bila ya kuwa na hela za kutakatisha. Lakini kosa lao kubwa ni ama hawasifu juhudi, au wanakosoa juhudi au hawalambi nyayo za watawala.
Wewe ndiye sauti yao, wewe ndiye mkombozi uliyetumwa kwaajili ya wote. Wanaohitaji msaada wako siyo CHADEMA, ACT, au wapinzani tu, lakini wapo wengi ndani ya CCM pia. Wanalazimika kusifu mpaka kufikia kukufuru. Wengine mpaka wanafikia kumwita mwanadamu mwenzao ni Yesu Kristo (kufuru kubwa!). Hawa wote hawafanyi hivyo kwa kupenda bali kwa sababu ya hofu. Wamekuwa na hofu na uoga wa kupitiliza. Hawa wanahitaji msaada wako zaidi kuliko wafuasi wa vyama vya upinzani.
Tundu Antipas Lissu Umeshindishwa ili Umshinde Shetani, Siyo CCM.
Adui wa Watanzania siyo wanaCCM, siyo CCM wala siyo viongozi wa CCM bali ni Shetani aishiye ndani ya CCM. Ukisoma falsafa ya CCM na ya mwasisi wa CCM ipo wazi sana, ni kuheshimu utu na uhai wa binadamu, kulinda uhuru wa raia, kuheshimu uhuru wa maoni LAKINI lakini CCM ya leo inaua, inatesa, inapoteza watu, inajeruhi, inaonea, inapendelea na kubagua. Haya siyo ya CCM bali ni shetani aishiye ndani ya CCM. Mh. Tundu Lisu unganisha Watanzania wote wenye dhamira njema bila ya kujali vyama vyao, makabila yao, kanda zao, dini zao au tofauti zingine zozote ziwazo.
Tundu Lisu Antipasi Lissu Ishara ya Amani
Amani ya kweli ni tunda la haki, usawa na ukweli. Shetani haishi CCM tu bali kwa yeyote mwenye kumkaribisha. Popote uwapo tetea na usimamie haki maana huo ndio ushindi wa Mungu aliopenda audhihirishe kwako.
Mkono wa Bwana Ukasimame nawe popote, na ghadhabu ya Mshindi Mkuu ikawe juu ya Wenye kuikanyaga Haki.
Mheshimiwa sana, Mzalendo wa Kweli, Mwenye Upendo wa Kweli, Tundu Antipasi Lisu karibu nyumbani Tanzania. Tanzania, nchi ambayo kama siyo kwa mapenzi ya Mungu usingeweza kuiona tena kwa macho ya mwili.
Tundu Antipasi Lisu Dhihirisho la Ushindi wa Mungu
Tundu Antipas Lissu, kuishi kwako mpaka leo siyo ushindi wako bali ni ushindi wa Mungu dhidi ya shetani. Baada ya Mungu kumshinda shetani, na ukuu wake hudhihirika, wewe uliyelala mauti na Mungu, na Mungu kuyashinda mauti ya shetani, itakuwa ni laana kwako nasi tunaosimama na Mungu wa haki, siku moja tukarudi tukaungana na shetani. Tukifanya hivyo, ushindi wa Mungu dhidi ya shetani hautakuwa na maana
Tundu Antipas Lissu ni Mageuzi ya Falsafa ya Siasa za Tanzania
Siasa za Tanzania zimejaa ulaghai, hila, unafiki, uoga, rushwa na hata ushirikina. Lakini siasa ndiyo hutoa wafalme, watawala na viongozi wote Duniani. Je, ni halali anayewaongoza watu kuwa mnafiki, mlaghai, mwongo na mtoa rushwa? Hapana. Siyo sahihi. Imekuwa kama ilivyo kwa sababu katika siasa za Tanzania ndiko shetani anakoishi.
Tundu Lisu unatakiwa kuzigeuza siasa za Tanzania kutoka kwenye hali ya sasa mpaka kuifanya siasa kuwa ni ukweli, uungwana, ujasiri wa kuunena ukweli na usafi dhidi ya kila uchafu ufananao na rushwa. Leo kwenye kura za maoni ndani ya CCM ni kilio. Kwa sababu kila aina ya uchafu vimetumika. Iwe ni wapinzani au CCM, wamechoka siasa za uwongo, unafiki, hila na uoga. Wewe ndiye utayaongoza mabadiliko haya.
Tundu Antipasi Lissu ni Kifutio cha Dhulma na Upendeleo
Tanzania ya leo, watu wanalia kwa uonevu, chuki na upendeleo. Watu wanalalamikia upendeleo wa ukanda, undugu, na kwa mbali udini. Watu wanalia kwa kudhulumiwa mali zao walizositafuta kwa haki. Watu wanalia kwa kubambikiwa kesi za uhujumu uchumi bila ya kuhujumu uchumi, kutakatisha fedha bila ya kuwa na hela za kutakatisha. Lakini kosa lao kubwa ni ama hawasifu juhudi, au wanakosoa juhudi au hawalambi nyayo za watawala.
Wewe ndiye sauti yao, wewe ndiye mkombozi uliyetumwa kwaajili ya wote. Wanaohitaji msaada wako siyo CHADEMA, ACT, au wapinzani tu, lakini wapo wengi ndani ya CCM pia. Wanalazimika kusifu mpaka kufikia kukufuru. Wengine mpaka wanafikia kumwita mwanadamu mwenzao ni Yesu Kristo (kufuru kubwa!). Hawa wote hawafanyi hivyo kwa kupenda bali kwa sababu ya hofu. Wamekuwa na hofu na uoga wa kupitiliza. Hawa wanahitaji msaada wako zaidi kuliko wafuasi wa vyama vya upinzani.
Tundu Antipas Lissu Umeshindishwa ili Umshinde Shetani, Siyo CCM.
Adui wa Watanzania siyo wanaCCM, siyo CCM wala siyo viongozi wa CCM bali ni Shetani aishiye ndani ya CCM. Ukisoma falsafa ya CCM na ya mwasisi wa CCM ipo wazi sana, ni kuheshimu utu na uhai wa binadamu, kulinda uhuru wa raia, kuheshimu uhuru wa maoni LAKINI lakini CCM ya leo inaua, inatesa, inapoteza watu, inajeruhi, inaonea, inapendelea na kubagua. Haya siyo ya CCM bali ni shetani aishiye ndani ya CCM. Mh. Tundu Lisu unganisha Watanzania wote wenye dhamira njema bila ya kujali vyama vyao, makabila yao, kanda zao, dini zao au tofauti zingine zozote ziwazo.
Tundu Lisu Antipasi Lissu Ishara ya Amani
Amani ya kweli ni tunda la haki, usawa na ukweli. Shetani haishi CCM tu bali kwa yeyote mwenye kumkaribisha. Popote uwapo tetea na usimamie haki maana huo ndio ushindi wa Mungu aliopenda audhihirishe kwako.
Mkono wa Bwana Ukasimame nawe popote, na ghadhabu ya Mshindi Mkuu ikawe juu ya Wenye kuikanyaga Haki.