Rijali jandoni
JF-Expert Member
- Apr 5, 2018
- 2,165
- 2,251
"Najua nitakufa sitapona ugonjwa huu nawaacha watanzania wangu najua watalia sana nami nitawaombea kwa Mungu, naondoka nikiwa nime waachia taifa moja lenye umoja na amani. Wosia wangu kwao waipende nchi yao kama wanavyo penda mama zao, wajue hawana nchi nyingine zaidi ya Tanzania" Mwisho wa maneno ya baba wa Taifa na akafariki.
Katika nchi zote za Africa naweza diriki kusema hakuna taifa lenye watu wazalendo, upendo na imani juu ya taifa lao kama watanzania.
Umoja huu na upendo tulio nao juu ya ardhi hii, si kwasababu ni waoga ila tumekuzwa katika misingi ya umoja, ushirikiano na upendo baina yetu na nchi yetu kwa ujumla.
Wenye ridhaa katika nafasi tofauti ndani na nnje ya Tanzania tambueni hamna nchi nyingine ispokuwa Tanzania, kwenye amani Tanzania ni mtoto tumlinde kwenye shida na mateso Tanzania ni mama tutamlilia..
Kwa namna hii viongozi kwa wananchi haina haja ya kusahau kuijenga nchi yetu kwa upendo maana haileti amani pale ambapo kila kitu kuhusu mradi au tenda kinatoka lakini hakuna utekelezaji inafika wakati hata kukaa na kutembelea maeneo ya nchi inatupa wasiwasi kwa sababu ya miundombinu isio malizika, na huduma nyingine ambazo hazija fanyika kabisa ila ni ahadi na paper works kutoka kwa viongozi wenye weledi usio tosha.
Wewe kama kiongozi wa ngazi fulani mbunge, waziri, mkurugenzi hata mtendaji barabara unayo acha kwenye vumbi na matope kesho utapita hapo ina maana gani na italeta hisia zipi kama umepokea hela na huku fanikisha mradi husika?
Kwenye hospitali au kituo cha afya ulicho omba na kukabidhiwa hela ukala kesho kuna jamaa na ndugu zako watakosa huduma na kufariki hapo je utakuwa na amani baada ya haya yote?
Vivyo hivyo miradi ya shule ni mingapi haija kamilika kwa sababu hela hazijafika eneo husika? mataifa yote tunayo ona huko nnje yana ustaarabu, maendeleo, usafii na amani kama tulio nayo kwasababu wananchi wao wamepewa mazingira mazuri juu ya elimu zote za darasani na kijamii, Tanzania tunajitahidi ila kwa kasi ya dunia ya sasa bado tunahitajika kuendelea zaidi.
Kwenye mazingira ya biashara ni eneo zito ila tuwape na tuwalinde wawekezaji wa ndani na wafanya biashara naelewa ni ngumu kuanzisha viwanda vikubwa kwa sababu ya sera na mikataba ya mataifa makubwa juu ya nchi za africa, lakini basi hata kwa vitu vinavyo ingia tuvifikirie kwenye utaratibu wake wa kuingizwa nchini ili vilete unafuu au vichache vizalishwe ndani hiyo nayo itakuwa upendo kwa taifa lako
Hatusemi kwamba hakuna viongozi watendaji hapana wapo japo tunahitaji uwajibikaji halisi juu ya nchi na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa kipindi hiki na vingine vinavyokuja mifumo na taasisi husika zitengeneze na kuleta watendaji wenye nia ya kweli juu ya nchi, nafasi zikaliwe na watu weledi na wenye ujuzi wa eneo husika ili kuleta utendaji bora na wenye ufanisi
Nafasi wasipewe watu sababu ya ubini, ujamaa au undugu tutaweza zorotesha Tanzania yetu, kwa miaka 75 maximum ya Uhuru tunatamani kusiwepo na shida ya umeme, maji, barabara, uhaba wa shule itakuwa ni huzuni na aibu kwetu sisi watanzania kama bado haya mambo yataitesa hii nchi
Tunaelewa nafasi na majukumu ya uongozi ni magumu sana mnakutana na changamoto nyingi kwenye mikataba na mambo mengine tuna tambua dunia ya huko nje haina huruma japo hawapendi wananchi wajue hilo, mnajitahidi lakini tunahitaji utendaji mkubwa zaidi maana uwezo tunao wa kuyafanya yote haya ila tutangulize upendo na utanzania kwenye kila fursa tunazo pata tusifikirie kwa ubinafsi bali tuweke kila kitu kwa maslahi mapana ya Taifa
Tukiwa na hospitali nzuri na mfumo wa elimu tuka uongezea vitendo zaidi, waziri atatibiwa hapo hakuna haja ya kwenda nnje, mbunge vivyo hivyo polisi wataenda pia wao na familia zao wakulima wafugaji na wafanya biashara wote watafika hapo tuipende Tanzania
Nchi ijengwe kwanza ndio watu waanze kula matunda mataifa mengi ya huko ndio yafanyavyo Singapore, Malaysia, China, Korea na Japan viongozi wanakula matunda ya utendaji wao baada ya ujenzi ila kwetu kwanini ni ngumu?
Mungu awalinde niwatakie majukumu mema.
Mungu Ibariki Tanzania
Katika nchi zote za Africa naweza diriki kusema hakuna taifa lenye watu wazalendo, upendo na imani juu ya taifa lao kama watanzania.
Umoja huu na upendo tulio nao juu ya ardhi hii, si kwasababu ni waoga ila tumekuzwa katika misingi ya umoja, ushirikiano na upendo baina yetu na nchi yetu kwa ujumla.
Wenye ridhaa katika nafasi tofauti ndani na nnje ya Tanzania tambueni hamna nchi nyingine ispokuwa Tanzania, kwenye amani Tanzania ni mtoto tumlinde kwenye shida na mateso Tanzania ni mama tutamlilia..
Kwa namna hii viongozi kwa wananchi haina haja ya kusahau kuijenga nchi yetu kwa upendo maana haileti amani pale ambapo kila kitu kuhusu mradi au tenda kinatoka lakini hakuna utekelezaji inafika wakati hata kukaa na kutembelea maeneo ya nchi inatupa wasiwasi kwa sababu ya miundombinu isio malizika, na huduma nyingine ambazo hazija fanyika kabisa ila ni ahadi na paper works kutoka kwa viongozi wenye weledi usio tosha.
Wewe kama kiongozi wa ngazi fulani mbunge, waziri, mkurugenzi hata mtendaji barabara unayo acha kwenye vumbi na matope kesho utapita hapo ina maana gani na italeta hisia zipi kama umepokea hela na huku fanikisha mradi husika?
Kwenye hospitali au kituo cha afya ulicho omba na kukabidhiwa hela ukala kesho kuna jamaa na ndugu zako watakosa huduma na kufariki hapo je utakuwa na amani baada ya haya yote?
Vivyo hivyo miradi ya shule ni mingapi haija kamilika kwa sababu hela hazijafika eneo husika? mataifa yote tunayo ona huko nnje yana ustaarabu, maendeleo, usafii na amani kama tulio nayo kwasababu wananchi wao wamepewa mazingira mazuri juu ya elimu zote za darasani na kijamii, Tanzania tunajitahidi ila kwa kasi ya dunia ya sasa bado tunahitajika kuendelea zaidi.
Kwenye mazingira ya biashara ni eneo zito ila tuwape na tuwalinde wawekezaji wa ndani na wafanya biashara naelewa ni ngumu kuanzisha viwanda vikubwa kwa sababu ya sera na mikataba ya mataifa makubwa juu ya nchi za africa, lakini basi hata kwa vitu vinavyo ingia tuvifikirie kwenye utaratibu wake wa kuingizwa nchini ili vilete unafuu au vichache vizalishwe ndani hiyo nayo itakuwa upendo kwa taifa lako
Hatusemi kwamba hakuna viongozi watendaji hapana wapo japo tunahitaji uwajibikaji halisi juu ya nchi na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa kipindi hiki na vingine vinavyokuja mifumo na taasisi husika zitengeneze na kuleta watendaji wenye nia ya kweli juu ya nchi, nafasi zikaliwe na watu weledi na wenye ujuzi wa eneo husika ili kuleta utendaji bora na wenye ufanisi
Nafasi wasipewe watu sababu ya ubini, ujamaa au undugu tutaweza zorotesha Tanzania yetu, kwa miaka 75 maximum ya Uhuru tunatamani kusiwepo na shida ya umeme, maji, barabara, uhaba wa shule itakuwa ni huzuni na aibu kwetu sisi watanzania kama bado haya mambo yataitesa hii nchi
Tunaelewa nafasi na majukumu ya uongozi ni magumu sana mnakutana na changamoto nyingi kwenye mikataba na mambo mengine tuna tambua dunia ya huko nje haina huruma japo hawapendi wananchi wajue hilo, mnajitahidi lakini tunahitaji utendaji mkubwa zaidi maana uwezo tunao wa kuyafanya yote haya ila tutangulize upendo na utanzania kwenye kila fursa tunazo pata tusifikirie kwa ubinafsi bali tuweke kila kitu kwa maslahi mapana ya Taifa
Tukiwa na hospitali nzuri na mfumo wa elimu tuka uongezea vitendo zaidi, waziri atatibiwa hapo hakuna haja ya kwenda nnje, mbunge vivyo hivyo polisi wataenda pia wao na familia zao wakulima wafugaji na wafanya biashara wote watafika hapo tuipende Tanzania
Nchi ijengwe kwanza ndio watu waanze kula matunda mataifa mengi ya huko ndio yafanyavyo Singapore, Malaysia, China, Korea na Japan viongozi wanakula matunda ya utendaji wao baada ya ujenzi ila kwetu kwanini ni ngumu?
Mungu awalinde niwatakie majukumu mema.
Mungu Ibariki Tanzania